jerrytz
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 5,980
- 4,284
Asante kwa uchambuzi wako.
Nina jambo moja tu ambalo naliona kama mtaji wa CCM kwa raia wa Tanzania nalo ni kukosekana kwa elimu ya uraia. Kama una kundi kubwa la wananchi wanaodhani kuwa kujengwa kwa miundo mbinu ya usafiri, shule na zahanati ni asante na ni bei ya uhuru wa kuchagua kiongozi bora basi CCM itaendelea kushinda.
Kwa mtazamo wangu siasa za Africa na za nchi maskini zinajengwa zaidi na vitu vidogo vidogo kwa kuwa pia upeo wa raia wengi wa nchi hizo ni mdogo sana.
Embu fikiria miaka 50 baada ya uhuru je hiki ni kiwango cha maendeleo ambacho tunaweza kuridhika nacho?!
Binafsi nimeona pia namna ambavyo CCM imekuja na namna mpya ya kuwabana watendaji ambao pia ni wanachama wa CCM ili kuleta picha kwa jamii kuwa wanaorudisha nyuma maendeleo ni watendaji na sio CCM kama Chama, ndio maana kwa sasa ni kawaida tu kumsikia Ndugu Kinana akitoa agizo kwa mkuu wa Mkoa au Wilaya.
Vyama vya upinzani bado vina kazi kubwa ya kufanya kwa kuwa inawezekana matokeo ya uchaguzi 2010 yaliitisha CCM kwa hiyo hawako tayari kufanya kosa kama hilo 2015.
Nina jambo moja tu ambalo naliona kama mtaji wa CCM kwa raia wa Tanzania nalo ni kukosekana kwa elimu ya uraia. Kama una kundi kubwa la wananchi wanaodhani kuwa kujengwa kwa miundo mbinu ya usafiri, shule na zahanati ni asante na ni bei ya uhuru wa kuchagua kiongozi bora basi CCM itaendelea kushinda.
Kwa mtazamo wangu siasa za Africa na za nchi maskini zinajengwa zaidi na vitu vidogo vidogo kwa kuwa pia upeo wa raia wengi wa nchi hizo ni mdogo sana.
Embu fikiria miaka 50 baada ya uhuru je hiki ni kiwango cha maendeleo ambacho tunaweza kuridhika nacho?!
Binafsi nimeona pia namna ambavyo CCM imekuja na namna mpya ya kuwabana watendaji ambao pia ni wanachama wa CCM ili kuleta picha kwa jamii kuwa wanaorudisha nyuma maendeleo ni watendaji na sio CCM kama Chama, ndio maana kwa sasa ni kawaida tu kumsikia Ndugu Kinana akitoa agizo kwa mkuu wa Mkoa au Wilaya.
Vyama vya upinzani bado vina kazi kubwa ya kufanya kwa kuwa inawezekana matokeo ya uchaguzi 2010 yaliitisha CCM kwa hiyo hawako tayari kufanya kosa kama hilo 2015.