Nahodha yupo chini, benchi la ufundi mnasemaje?

Nahodha yupo chini, benchi la ufundi mnasemaje?

pansophy

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2011
Posts
502
Reaction score
320
Kila nikiangalia kelele za wanao jiita wanaharakati pamoja na wanasiasa wa vyama vya upinzani wanavyohaha kuibuka na hoja mbalimbali ili kuongeza mitaji yao kisiasa wananikumbusha kipindi cha kwanza cha mechi ya fainali ilivyokuwa yakuvutia.

Benchi la ufundi lilifanya mabadiliko ya dharura kwa kumtoa yule mchezaji wetu mkongwe kwenye dimba la kati na kumuweka mchezaji machachari na mwenye uwezo mkubwa wa kugawa vyumba na kumudu dimba vizuri, mwenye kasi ya ajabu tuliye msajili kwa gharama kubwa 2015 na kumpa unahodha kwenye klabu yetu ya kinondoni iliyokuwa imesheheni wachezaji wenye vipaji kede kede na waliokuwa na usongo pamoja na molari ya juu wakipambwa na mashabiki waliokuwa na uchungu wa timu yao.

Timu ilianza vizuri, safu ya ushambuliaji na kiungo ilikuwa ipo vizuri sana. Nahodha mpya alikuwa yupo kila sehemu kuimarisha safu zote, alizunguka uwanja mzima bila ya kuchoka kwa hakika timu ilikuwa ipo vizuri. Pamoja na umahiri wote wa wachezaji na benchi la ufundi lililokuwa limesheheni wataalam kutoka nje ya nchi, dakika ya kumi na tano mabingwa watetezi walifanikiwa kuandika bao la kwanza lililopigwa kwa mkwaju mkali ndani ya boksi kufuatia shambulio lililopangwa vyema.

Bao hili limeitoa timu yetu kwenye mchezo kabisa, nahodha kashindwa kutuliza mihemuko ya wachezaji wake mpira umekuwa wa rafu nyingi, tumeelemewa kidogo, kelele na shangwe za mashabiki zimepungua sana. Nahodha amepata hitilafu kidogo anapatiwa matibabu na daktari kutoka tarime na hai, tunatumaini ataweza kuendelea na mchezo.

Kwako mwalimu Kashasha......
 
Upande wa Kashasha; " Asante sana Enock Bwigane.. kama kocha wa timu hii pinzani atakuwa na ...good couching decisions ni rahisi sana kubalance football chemistry, ambayo makosa yote yako kwa beki wa left wing. Nidhahiri shahiri forward huyu..wa timu yao ana football skills with alot of game flexibility..ball balance, ball control. Hili ni suala la kocha tu kufanya maamuzi ili kuweza kubalance game hii...

Kwako Enock!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fanyeni kebehi ila hamjui hali ilivyo mbaya huko ndani.
Mkijuacho ni mbwembwe za kulazimisha majukwaani na data msomazo kwenye magazeti kama Tanzanite na Jamvi la wageni.
Mambo ni moto!
 
Kila nikiangalia kelele za wanao jiita wanaharakati pamoja na wanasiasa wa vyama vya upinzani wanavyohaha kuibuka na hoja mbalimbali ili kuongeza mitaji yao kisiasa wananikumbusha kipindi cha kwanza cha mechi ya fainali ilivyokuwa yakuvutia.

Benchi la ufundi lilifanya mabadiliko ya dharura kwa kumtoa yule mchezaji wetu mkongwe kwenye dimba la kati na kumuweka mchezaji machachari na mwenye uwezo mkubwa wa kugawa vyumba na kumudu dimba vizuri, mwenye kasi ya ajabu tuliye msajili kwa gharama kubwa 2015 na kumpa unahodha kwenye klabu yetu ya kinondoni iliyokuwa imesheheni wachezaji wenye vipaji kede kede na waliokuwa na usongo pamoja na molari ya juu wakipambwa na mashabiki waliokuwa na uchungu wa timu yao.

Timu ilianza vizuri, safu ya ushambuliaji na kiungo ilikuwa ipo vizuri sana. Nahodha mpya alikuwa yupo kila sehemu kuimarisha safu zote, alizunguka uwanja mzima bila ya kuchoka kwa hakika timu ilikuwa ipo vizuri. Pamoja na umahiri wote wa wachezaji na benchi la ufundi lililokuwa limesheheni wataalam kutoka nje ya nchi, dakika ya kumi na tano mabingwa watetezi walifanikiwa kuandika bao la kwanza lililopigwa kwa mkwaju mkali ndani ya boksi kufuatia shambulio lililopangwa vyema.

Bao hili limeitoa timu yetu kwenye mchezo kabisa, nahodha kashindwa kutuliza mihemuko ya wachezaji wake mpira umekuwa wa rafu nyingi, tumeelemewa kidogo, kelele na shangwe za mashabiki zimepungua sana. Nahodha amepata hitilafu kidogo anapatiwa matibabu na daktari kutoka tarime na hai, tunatumaini ataweza kuendelea na mchezo.

Kwako mwalimu Kashasha......
Engineer soma hiyooooo...............! haya mwl Kashasha natumai wote tumekuelewa
 
Upande wa Kashasha; " Asante sana Enock Bwigane.. kama kocha wa timu hii pinzani atakuwa na ...good couching decisions ni rahisi sana kubalance football chemistry, ambayo makosa yote yako kwa beki wa left wing. Nidhahiri shahiri forward huyu..wa timu yao ana football skills with alot of game flexibility..ball balance, ball control. Hili ni suala la kocha tu kufanya maamuzi ili kuweza kubalance game hii...

Kwako Enock!

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona kuna kijana kutoka Singida kaskazini ameanza kunyoosha viungo, ni dhahiri benchi la ufundi linakusudia kufanya mabadiliko kabla ya kipindi cha kuanza kuisha.

Mwalimu Kashasha, unaona mabadiliko yanaweza kusaidia timu?
Naona viongozi watimu wanamzonga zonga kamisaa kutoka pale UKonga... Naamini uamuzi wa mpiga kipyenga ndio wa mwisho, mpiga kipyenga huyu anauzoefu wa kutosha kutoka Dodoma hivyo sidhani kama kamisaa ataweza kumbadilisha maamuzi.

Kwako mwalimu Kashasha...
 
Back
Top Bottom