Nahitaji wazo mbadala nifanye nini katika hili

Nahitaji wazo mbadala nifanye nini katika hili

aimi lyatuu

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2015
Posts
755
Reaction score
834
Wakuu amani iwe kwenu!

Nielekee kwenye hoja yangu ndugu zangu. Jana asubuhi wakati nafungua ofisi yangu niliona pochi ya kike karibu na ofisi Nilishtuka kidogo labda kaisahau mdada ama mtego labda ndani ina mihadarati ama. Niliichukua na kuikagua ndani kulikuwa na kadi ya benk (NMB Tanzanite), kadi ya mwendo kasi, passport za watu watatu na salary slip majina nayahifadhi kwa usalama wangu.

Ombi kwenu wanajukwaa ni namna ya kumpatia mwenye pochi yake bila kupata msukosuko. Nawaza nipeleke polisi pochi. Je, wakinikamata kwa madai aliyeibiwa aliuwawa nishirikiane na police kwenye uchunguzi (mimi ni baba mpya hata mwaka sijafika).

Je, nichukue namba ambazo zipo kwenye salary slip niwapigie lakini binadamu kiumbe cha hovyo anaweza kunihusisha moja kwa moja kwenye matatizo yaliyompata ama nikaushe tu.

Msaada wakuu!
 
oohoo ohooo ooo, hiyo ni 'big noma' a.k.a 'big matatizo' shauri yako utaambiwa wewe ndiyo uliye husika na kifo cha marehem, adi uchunguzi ukamilike utajikuta ushakaa lupango kwa miaka7 na familia imeisha umia, polisi wetu wapo hoi kiupelelezi, intalijesia yao ni kukamata wapinzani tuu, aliye uleta apo kwako siyo mjinga…...
 
aiseee haya mambo haya yanaogopesha hata kama ukiwa na nia nzuri
 
Wakuu nimesoma coment zote hizi jibu ni moja nililo lipata kwamba kutokana na "intelijensia" ya nchi yetu hili swala laweza kuwa dogo machoni kwangu ila baada ya kulifanya naweza nikajiachia alama ya kutosha katika maisha yangu yote.
Naitupa usiku kwa wale wafagia barabara kijanja!!
Asanteni wakuu!!
 
Wakuu nimesoma coment zote hizi jibu ni moja nililo lipata kwamba kutokana na "intelijensia" ya nchi yetu hili swala laweza kuwa dogo machoni kwangu ila baada ya kulifanya naweza nikajiachia alama ya kutosha katika maisha yangu yote.
Naitupa usiku kwa wale wafagia barabara kijanja!!
Asanteni wakuu!!
Hapana ni wazo la hovyo kabisa...kumbuka umeshaweka Alama za vidole kwenye hilo Pochi...... Na Kama ni kweli ikitokea aliyelipoteza aliuwawa kwa Alama hizo wewe nawe utahusishwa na tukio hilo na kukupata ni rahisi Kuna kitu Kama Kitambulisho cha Taifa, usajili wa Laini za simu Alama zako za vidole zipo.......
Mimi nakushauri ni Bora Mara 10 nenda polisi waeleze nadhani watakuelewa......
Siku nyingine ukiona kitu kama hicho usikimbilie kushika peleka taarifa Polisi.......
Wachaga bhanaa.......!!!!!
 
Kaitupe sehemu yoyote usiku hata karibu na polisi, walioshika ni wengi hivyo basi sioni kama kujipeleka polisi ni suruhisho. Nawe kaitupe
 
Ichukue nenda pembeni ya mji kaitupe huko alafu kausha, ukijifanya kwenda polis au sijui upige simu umekwisha, utaswekwa ndani hadi ukweli kugundulika ushakaa vya kutosha
 
Tanzania ni nchi mbaya sana kuishi. Nchi nyingine, hapo unampigia simu mwenye pochi, anachukuwa pochi yake ikiwa na kadi na pesa zake kabisa. Ama unaipeleka polisi kama mwenye pochi hapatikani. Akikupa zawadi unaikataa kwa vile hata wewe pia ungeweza kupoteza kitu akakiokota yeye na akakupa bila malipo. Hata polisi hawaaminiki? Eti kisiwa cha amani! Maoni yaliyokwishatolewa yanasikitisha sana. Utaokotaje passport za wenzako halafu unakwenda kuzitupa? Ubinadamu uko wapi? Mungu wetu ataamua mengi siku ya hukumu!
 
Mkuu ni Tanzania pekee ambapo unaokota mtu kapigwa nusura kuaea unamsaidia unakamatwa eti ukaisaidie polisi. Yani Tanzania polisi haihutaji ushahidi kukuweka ndani hisia tu inatosha kukuweka ndani.
Tatizo siyo wananchi tatizo ni vyombo vya usalama vinavyofanya kazi vimetufanya tuwe waoga hata wa kutoa msaada
Tanzania ni nchi mbaya sana kuishi. Nchi nyingine, hapo unampigia simu mwenye pochi, anachukuwa pochi yake ikiwa na kadi na pesa zake kabisa. Ama unaipeleka polisi kama mwenye pochi hapatikani. Akikupa zawadi unaikataa kwa vile hata wewe pia ungeweza kupoteza kitu akakiokota yeye na akakupa bila malipo. Hata polisi hawaaminiki. Eti kisiwa cha amani! Maoni yaliyokwishatolewa yanasikitisha sana. Utaokotaje passport za wenzako halafu unakwenda kuzitupa? Ubinadamu uko wapi? Mungu wetu ataamua mengi siku ya hukumu!
 
Ila mkuu mpaka muda huu nimepitia viama mbalimbali pia nimeshuhudia watu waliopitia moto kwangu hiyo ni kitaaolojia...na kweli nimelisachi vya kutosha kama ni alama ya vidole nimeacha kwa kila kitu kilichomo mule kwenye pochi na hili ndilo limenifanya niombe ushauri hapa jamvini
Hapana ni wazo la hovyo kabisa...kumbuka umeshaweka Alama za vidole kwenye hilo Pochi...... Na Kama ni kweli ikitokea aliyelipoteza aliuwawa kwa Alama hizo wewe nawe utahusishwa na tukio hilo na kukupata ni rahisi Kuna kitu Kama Kitambulisho cha Taifa, usajili wa Laini za simu Alama zako za vidole zipo.......
Mimi nakushauri ni Bora Mara 10 nenda polisi waeleze nadhani watakuelewa......
Siku nyingine ukiona kitu kama hicho usikimbilie kushika peleka taarifa Polisi.......
Wachaga bhanaa.......!!!!!
 
Kuwa Raia Mwema peleka polisi toa maelezo yako na Utabarikiwa mkuu tenda wema uende zako
 
So kwa akili zako za vijiweni unadhani hadi sasa hivi polisi hawawezi kukukamata ikiwa watakuwa na hiyo nia?

Hizi ID FEKI zinawadanganya sana ndugu
 
Ila mkuu mpaka muda huu nimepitia viama mbalimbali pia nimeshuhudia watu waliopitia moto kwangu hiyo ni kitaaolojia...na kweli nimelisachi vya kutosha kama ni alama ya vidole nimeacha kwa kila kitu kilichomo mule kwenye pochi na hili ndilo limenifanya niombe ushauri hapa jamvini
Umefanya vizuri kuomba ushauri, achana na hao wanaokuambia nenda katupe kwani Dunia ina mengi unaweza kuona uko peke yako sehemu Kumbe kuna mtu anashuhudia unachofanya na ikitokea ameenda kutoa taarifa polisi na kukutaja wewe hiyo itakula kwako hitakuwa na cha kusema.......ndipo hapo utakapohusishwa na tukio lolote lililompata Mwenye hiyo pochi......
Hisia ndicho kitu cha kwanza katika upelelezi hasa Kama mtuhumiwa uko nae ana kwa ana......kwa hiyo polisi kukushikilia kwa muda kwa ajili ya mahojiano siyo mbaya ni wewe ndiye utajiweka kwenye Hisia za kufikiriwa ya kuwa unadanganya au LA........ Mfano
1.kuna mtu anatoka ushahidi ya kuwa alikuona unatupa Pochi usiku na wakipima Alama za vidole kwenye Pochi ni zako na wewe unakataa yakuwa hujatupa pochi
2. Utajieleza polisi kuwa uliogopa kutoa taarifa kwa kuogopa kusumbuliwa......hii inatia shaka na kufikirisha ya kuwa inawezekana una matukio mengi unayajua au kuyafanya na kuogopa Polisi.... Hivyo polisi watataka wayajue

Kwa sasa naona niishie hapo kwani kumbuka Ukweli hukuweka Huru.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom