Nahitaji Vifaa vya Ujenzi

Unaweza kuniona kama unaitaji mbao na mirunda kwa bei poa. Ninazo mbao za 1x8=3500, 2x4=2800 na mirunda kwa tsh 1000. wasiliana na mimi kwenye kimandolu@hotmail.com. Nipo Mbezi Tanki Bovu. Mbao hizi zitakusaidia sana kwenye gorofa lako kwani gorofa linaitaji mbao nyingi sana.
 

Mkuu hizi mbao na milunda ni kwa ajili ya kuezekea au kushikia zege na kusimamia mafundi?
 
Mazingira and co,
bei za Kerai walau ulinganishe na kwingine

View attachment 29832

Mama Joe kuna hawa watu wanaitwa Framland logistics co. Ltd wako Bahari Beach naona bei zao ni nzuri kuliko hao Kerai. Wanatoa matofali 25 kwa mfuko mmoja. Bei zao ni kama ifuatavyo:-

TOFALI ZA KOKOTO INCHES 6'' ni tshs. 1200 per unit
TOFALI ZA KOKOTO INCHES 5'' ni ths. 1100 per unit

TOFALI ZA KAWAIDA:

6 '' = TSHS. 950.00

5'' = TSHS. 850.00

4'' = TSHS. 750.00

Sasa hiyo ni bei ya pale pale site walipo ila usafiri ni tshs. 200 kwa tofali manake sasa ukitaka kununua tofali moja wanakuletea mpaka site kwako kwa bei hiyo tajwa hapo juu ukiongeza na usafiri POPOTE pale Dar es salaam.

Matofali yao ni imara kwa mfuko mmoja wanatoa tofali 25 tu meaning content ya cement na mchanga ni nzuri na inawiana na hivyo kuwa na tofali gumu na imara.

Kuhusu Mchanga

TANI 18 ni TSHS. 180,000 kokote pale Dar es salaam

Tani 10 ni tshs. 100,000

Tani 7 ni 80,000

Kokoto ni zile za Kunduchi (nyekundu) na wanauza kwa bei kama ifuatavyo:

Tani 18 ni tshs. 150,000

tani 10 ni tshs. 80,000

tani 7 ni 60,000


Simu yao ni +255762089225 kwa maelezo zaidi.
 
Poleni wana JF hasa mlioko kwenye mchakato wa ujenzi na ambao mmetoa ushauri. Kimsingi Ndg yangu Mazingira na Mama Joe ushauri mliopewa ni mzuri sana. Ni kuufanyia kazi kwa umakini na kufanya maamuzi sahihi na usimamizi makini.Kwa suala la nondo kweli KAMAKA ndo muafaka. Pale hakuna uswahili na vibaka hakuna. Utaratibuwao ni mzuri. Nendeni pale. Mahitaji ya nondo kiasi na size ni sensitive kwani ni technical aspect ambayo Engineer vema akakufanyia hesabu. Kuhusiana na na kokoto ushauri mzuri umetolewa. Kwa ghorofa moja kokoto za hapa DSM zinafaa tu. Mimi Nilithubutu, Nikaweza na Nasonga mbele. Mimi nimejenga ghorofa 1 naelekea kuezeka Desemba 2011. Amini usiamini, nilinununu mchanga wa kutosha, nikanunua simenti, nikawa na maji ya uhakika na nikawatafuta wafyatua tofari na kusimamia mfuko 1 tofari 25. Curing nilisimamia mwenyewe. ujenzi ulienda vizuri. Pamoja na Engineer wangu lakini nimejitahidi kuwa karibu na kusimamia kila nilipopata nafasi. Nimejifunza mengi juu ya upatikanaji wa building materials bora na kwa gharama nafuu. Kumbuka construction industry is too complicated like its market. Kuweni makini na mafundi, engineer, suppliers nk. Ndg Mazingira naona unahitaji nondo, kokoto, matofari, n.k. sijui uko wapi hapa DSM nione ninavyoweza kukusaidia. Hali kadhalika mama Joe. Ninaweza kuendelea kutoa ushaui if you think fit. Kila la heri
 
Poleni wana JF hasa mlioko kwenye mchakato wa ujenzi na ambao mmetoa ushauri. Kimsingi Ndg yangu Mazingira na Mama Joe ushauri mliopewa ni mzuri sana. Ni kuufanyia kazi kwa umakini na kufanya maamuzi sahihi na usimamizi makini.Kwa suala la nondo kweli KAMAKA ndo muafaka. Pale hakuna uswahili na vibaka hakuna. Utaratibuwao ni mzuri. Nendeni pale. Mahitaji ya nondo kiasi na size ni sensitive kwani ni technical aspect ambayo Engineer vema akakufanyia hesabu. Kuhusiana na na kokoto ushauri mzuri umetolewa. Kwa ghorofa moja kokoto za hapa DSM zinafaa tu. Mimi Nilithubutu, Nikaweza na Nasonga mbele. Mimi nimejenga ghorofa 1 naelekea kuezeka Desemba 2011. Amini usiamini, nilinununu mchanga wa kutosha, nikanunua simenti, nikawa na maji ya uhakika na nikawatafuta wafyatua tofari na kusimamia mfuko 1 tofari 25. Curing nilisimamia mwenyewe. ujenzi ulienda vizuri. Pamoja na Engineer wangu lakini nimejitahidi kuwa karibu na kusimamia kila nilipopata nafasi. Nimejifunza mengi juu ya upatikanaji wa building materials bora na kwa gharama nafuu. Kumbuka construction industry is too complicated like its market. Kuweni makini na mafundi, engineer, suppliers nk. Ndg Mazingira naona unahitaji nondo, kokoto, matofari, n.k. sijui uko wapi hapa DSM nione ninavyoweza kukusaidia. Hali kadhalika mama Joe. Ninaweza kuendelea kutoa ushaui if you think fit. Kila la heri
 

Mkuu weka namba yako hapa au nitumie kwenye PM nikupigie kabisa maana sasa mchakato wa ujenzi unaendelea
 

Mkuu nashukuru sana kwa ushauri wako mzuri. Hebu sasa kwa kutumia uzoefu wako nielekeze wapi naweza kupata milunda kwa bei ya chini ya Shs 2000. Pia mbao za kuezekea, floor tiles nzuri ( na zenye BS ya kutosha) n.k. Asante
 
Jamani nashukuru sana kwa maelezo haya yamenifaa sana,
bado nazunguka mikoani nategemea kuanza november au early december ila nitaanza kuwaulizia hawa kwasasa.
Mbarikiwe


 
Thanks mkuu hii inatia moyo tuko nyuma yako, nitakutafuta karibuni,
Blessings,

 
ok for more information!karibu kweny hardware(duka la vifaa vya ujenzi) yetu lipo tabata bonyukwa karibu na mnala wa voda.
 
Ndiyo Mazingira. Nimekupata. Ntakupa jibu kama ulivyoulizia juu ya Milunda na Tiles. Lkn ni simple kuhusu Milunda kama una muda wa kutosha watafute na ongea na wenye maroli wasafirishaji wa milunda au waweza kuagiza. Hata wauza mkaa wa maroli hasa yanayotokea Kisarawe n.k wanaweza kukuelekeza au unaweza kuwaagiza milunda kwa aina na idadi kulingana na idadi unayotaka. Mimi nilizuia roli jamaa wakaniuzi milunda 400 nikashusha yote site. Kumbuka sikuwa na gharama za kusafirisha wala kupakua! Wanderful! Kwa upande wa wauzaji yaani Hardware wanakuwa wamenunua toka kwenye maroli. Therefore unaweza kujua wanaongeza kiasi gani au wewe unatafuta unafuu kiasi gani. Nilichojifunza kwenye ujenzi ka wako, jikusanye unanunua materials in bulky utaiona nafuu yake. Asanteni
 
sijachelewa. kaka tembelea maabara ya ujenzi ya Tanroadsn ama Chuo cha Teknolocha Dsm kwa ushauri maridhawa
 

Asante sana mkuu kwa ushauri maridhawa. Nitaufanyia kazi.
 

Mkuu ulipotelea wapi?
Unaufahamu kuhusu finishing za concrete floor? Namaanisha Polished, na zile za Acid Stains. Tafadhali nifahamishe, ukiweza naomba uni-PM tafadhali!
 
Mkuu ulipotelea wapi?
Unaufahamu kuhusu finishing za concrete floor? Namaanisha Polished, na zile za Acid Stains. Tafadhali nifahamishe, ukiweza naomba uni-PM tafadhali!

Ni vyema akatoa somo hapahapa tukafaidika wote. Haya mkuu LAT toa darasa hapa.
 
Mkuu wa vitu vya U.K, tafadhali toa details zaidi za ubora na vipimo vyake ili wana-ukumbi waweze kuelewa kama madirisha yatakuwa compatible na nyumba zao.

Ahsante
 
Mkuu ulipotelea wapi?
Unaufahamu kuhusu finishing za concrete floor? Namaanisha Polished, na zile za Acid Stains. Tafadhali nifahamishe, ukiweza naomba uni-PM tafadhali!

Amoeba heshima mkuu

as per my experience floor finish of the type you prefer ni porcelain tiles (non-slippery) 10mm , size inategemea space , also marble floor slabs ni nzuri sana kwa floor finish that is naturally shinning, ceramic is polished artificially by applying vitrous material on its surfaces,
mkuu cha kuzingatia kwenye finishing ya floor tiles ni laying pattern (staggered, heringbone, basket etc) joints should be carefully maintained and edges treated
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…