Mkuu prime ina maana siku zingine za wiki kutakuwa hakuna magari?
Huoni kama ni usumbufu mtu alete gari jmosi j2 alifate. Kama halijapata mteja wiki ijayo alipeleke tena?
Na kuhusu kiingilio ina maana kila atakapopeleka gari itabidi alipie haijalishi gari itauzwa au la?
Mkuu hiyo biashara inafanyika only two days in a week yaani jumamosi na jumapili tu. siku nyingine za wiki hakuna biashara due to the fact that magari mengi yanayo uzwa na wenyewe wanayatumia kwa shughuli mbalimbali lakini kwa vile jumamosi na jumapili ni weekend, muhusika anaweka kuleta gari lake sokoni bila kumtumia dalali yeyote. Kuhusu kiingilio ni kila unapoleta gari unalipa due to the fact that muuzaji anarahisishiwa kupata mteja bila usumbufu mkubwa haijalishi gari itauzwa lini. Wanunuzi wa magari wataanzia kwako kabla hawaja enda kwingine. Hakuna usumbufu wa kuleta gari lako sokoni na kulirudisha nyumbani kwanza you may come up with a better idea unapokutana na wauzaji wenzio then you may end up exchanging vehicles according to needs of both parties.
Juu juu inaonekana biashara nzuri lakini angalia adha zake:
1. Kuanzisha kampuni utahangaishwa na manispaa kupata kibali mpaka utakoma. Suala la rushwa litaingia hapo.
2. Gharama za uandikishaji wa kampuni, ikiwa si kampuni bubu.
3. Gharama za kukodi eneo inaweza kuwa kubwa kuliko unavyofikiria.
4. Utahitaji ulinzi wa uhakika. mali za watu (mfano gari), ikiibiwa je?
Ni mawazo yangu tu, kwa kuwa sijawahi kufanya biashara yoyote pengine yote haya hayapo.