Kwa mliopitia saut mwanza. Kuna lecture ni marehemu anaitwa sir Njura Mungu mlaze mahali pazuri.
Nilipata jumla ya maksi 14 hiyo ni cozwok nzima na na kabla ya test alisema hv hakuna make up. Test nilipiga 4/20 Nilikonda sana nikajisemea hv ndio nina carry mazima.
Siku fulani ya kipindi chake cha single pale m10 jioni kabisa tuko watu wachache hatari akafundisha mwishoni akasema haya chukua karatasi. Akadisplay swali ubaoni kwa projector akasema tufanye. Kumbuka hapo tuko wachache balaa.
Baada ya kumaliza akasema karatasi za upande huu ziende upande ule za kule ziende pale. Lengo ni sisi kujisahihishia bila kujuana maana juu ya karatasi ni kukaa registration no tu. Baadaye akasema ya kuwa hii ndio make up
Mjuba nilifanya nakumbuka lilikuwa ni somo la discourse Analysis. Nikawa na uhakika katika yale maswali nimepata 6/10.
Siku aliyotoa feedback ya coursework kama nilivosema hapo juu ni nilijikuta nina 14. Akatoa tangazo kwa whtsap ya kuwa kama una tatizo mfuate. Dah nikakumbuka nilifanya makeup. Huyoo hadi ofisini kwake. Akasema tafuta karatasi yako ya make up hapo usubr folen. Ni kachukua boks langu nikalipa ta karatasi.
Kulicheki nina 6/10 so ukiongeza nakuwa na 20 kamili so ue uhakika nafanya. Nikamplekea karatasi baada ya kufika zamu yangu akalipitia tena asahihishe. Kumbe aliyenisahihishia alinikosesha maksi moja nikajikuta nina 7.
Dah nilishukuru sana kwa yeye kuusikiliza so ue nilifanya.
Juhudi yangu ya kutodoji vipindi ni msaada kwangu ambao najivunia pia.
Something sad ni kwamba haikupita hata mwezi SIR njura akafariki ghafla



aisee iliniuma sana yaani mtu katoka kunisaidia Then si muda anafariki.
Anyway nirudi kwako mkuu,
Jitahidi umuone mwalimu na jitahidi kuhudhuria vipindi vya mwsho kwani walimu huweza kuingiwa na huruma So unaweza kuta akatoa make up. Sasa na hiyo make up ukikosa utamlaumu nani. Have confidence mtafute muda wa consultation atakusikiliza.
Malecture nao walikuwa kama sisi so ukijieleza vzr hawezi kubana.



