Nahitaji ushauri wenu wakuu

Nahitaji ushauri wenu wakuu

Habari ndugu zangu JF!

Nipo katika wakati mgumu kuhusu shule.

Nimetoka kupokea matokeo ya test nimepata 0/15. Somo la East African Community law. Sio kwasababu sikuwa na majibu sahihi, Lah! Ni kwasababu nimejibu maswali mawili baadala ya moja kama yalivyokuwa maelekezo. Nikiri kwamba nili overlook instructions.

Binafsi nina mawazo sana wakuu wangu!

Sijawahi kupata “0” tangu nizaliwe.

Nimemfuata mwalimu husika personally na kumueleza tatizo langu. KAKATAA KATU!

Kinachonisumbua, kuingia UE ni kama ngamia kupita tundu la sindano.

Tuna group assignment (10 marks) na kuna test two ( hii bado hatujafanya ina marks 15).

Nishauri wakuu kwa hili.

Asante nawapenda wote!

Ushauri Ni huu: go ahead, una chance, sahau hiyo test Na ondoa hofu! Maana Na hiyo hofu utaharibu zaidi, Tafuta Mda wako msii Mungu akusaidie!
 
Kwa mliopitia saut mwanza. Kuna lecture ni marehemu anaitwa sir Njura Mungu mlaze mahali pazuri.
Nilipata jumla ya maksi 14 hiyo ni cozwok nzima na na kabla ya test alisema hv hakuna make up. Test nilipiga 4/20 Nilikonda sana nikajisemea hv ndio nina carry mazima.
Siku fulani ya kipindi chake cha single pale m10 jioni kabisa tuko watu wachache hatari akafundisha mwishoni akasema haya chukua karatasi. Akadisplay swali ubaoni kwa projector akasema tufanye. Kumbuka hapo tuko wachache balaa.
Baada ya kumaliza akasema karatasi za upande huu ziende upande ule za kule ziende pale. Lengo ni sisi kujisahihishia bila kujuana maana juu ya karatasi ni kukaa registration no tu. Baadaye akasema ya kuwa hii ndio make up
Mjuba nilifanya nakumbuka lilikuwa ni somo la discourse Analysis. Nikawa na uhakika katika yale maswali nimepata 6/10.

Siku aliyotoa feedback ya coursework kama nilivosema hapo juu ni nilijikuta nina 14. Akatoa tangazo kwa whtsap ya kuwa kama una tatizo mfuate. Dah nikakumbuka nilifanya makeup. Huyoo hadi ofisini kwake. Akasema tafuta karatasi yako ya make up hapo usubr folen. Ni kachukua boks langu nikalipa ta karatasi.
Kulicheki nina 6/10 so ukiongeza nakuwa na 20 kamili so ue uhakika nafanya. Nikamplekea karatasi baada ya kufika zamu yangu akalipitia tena asahihishe. Kumbe aliyenisahihishia alinikosesha maksi moja nikajikuta nina 7.
Dah nilishukuru sana kwa yeye kuusikiliza so ue nilifanya.
Juhudi yangu ya kutodoji vipindi ni msaada kwangu ambao najivunia pia.

Something sad ni kwamba haikupita hata mwezi SIR njura akafariki ghafla aisee iliniuma sana yaani mtu katoka kunisaidia Then si muda anafariki.
Anyway nirudi kwako mkuu,

Jitahidi umuone mwalimu na jitahidi kuhudhuria vipindi vya mwsho kwani walimu huweza kuingiwa na huruma So unaweza kuta akatoa make up. Sasa na hiyo make up ukikosa utamlaumu nani. Have confidence mtafute muda wa consultation atakusikiliza.
Malecture nao walikuwa kama sisi so ukijieleza vzr hawezi kubana.

Walimu wa Law wana misimamo na roho mbaya. S

Hongera wewe, hapa nimefanya test two na group assigment. Nangojea majibu!
 
Ushauri Ni huu: go ahead, una chance, sahau hiyo test Na ondoa hofu! Maana Na hiyo hofu utaharibu zaidi, Tafuta Mda wako msii Mungu akusaidie!

Ahsante mkuu. Test nimefanya nangojea majibu.
 
Si umpe hela, ngoja urudi huku uone kama utaeleweka
 
Dar umenikumbusha mbali sana, yaani kipindi icho ndio nimeingia 1st year chuo, test yangu ya kwanza ya Somo la CCC+ (programming language) nilipata 0/10% nilipigwa na butwaaaaaah, nilipata mpaka tumbo la kuhara, kila nikigeuka uku naskia watu sauti zinasema hapa Udsm-Coict watu wana disco sana nikajua nime kwisha ila cha kushangaza nilipata access ya kufanya UE na pia ilo somo siku sup mungu ni mkubwa sasaivi najishughulisha na uuzaji wa chakula cha mifugo ya kuku.
 
Huu Uzi Ni Kama mnataka kunirudisha Mimi Tena shule...na kwa hesabu zangu utakuwa upo Udsm..
 
Wakufunzi wana mambo ya ajabu sana.Sitasahau visa viwili katika maisha ya shule.

1.Test ikatangazwa watu tukasoma sanaaa,siku ya test ndani ya hall tukapewa mtihani watu wakaanza fanya kwa speed kuwahi muda.Kumbe bwana mwisho wa karatasi mkufunzi ameweka instruction ya "don't do any question, just read then after a time collect. Watu wamefanyaaaa,wachacheee tulisanukia mambo na ni vile tukitaka ona mtihani wote mdo tukaona hiyo.Maswali yalikiwa ya multiple choice so wengi walikaza A,D,C,B,etc.Ilikuwa ni kimbembeee,maana hakutaka ukisanye hata kama umejaza swali 1 tu.

Wachache tukakusanya baada ya muda wa test tukapata alama 10.

2.Ni mkufunzi kunikuta live band na group mate wangu bin,kumbe anamtakaga halafu dada kakataa.Weee usiombe hii kitu ikukute.Nili carry somo la yule jamaa aisee ktk mazingira ya uonevu kabisaaaa,sitasahau.

Pole,mfuate tena kwa unyenyekevu mwombe msamaha na kujishusha.

Acha tupike chips za jioni huku mtaani maana vyeti vipo sandukuni
 
Pole, anza kumsaidia kubeba briefcase yake kila asubuhi anavoingia kazini, lazima atakufikilia
 
Wakufunzi wana mambo ya ajabu sana.Sitasahau visa viwili katika maisha ya shule.

1.Test ikatangazwa watu tukasoma sanaaa,siku ya test ndani ya hall tukapewa mtihani watu wakaanza fanya kwa speed kuwahi muda.Kumbe bwana mwisho wa karatasi mkufunzi ameweka instruction ya "don't do any question, just read then after a time collect. Watu wamefanyaaaa,wachacheee tulisanukia mambo na ni vile tukitaka ona mtihani wote mdo tukaona hiyo.Maswali yalikiwa ya multiple choice so wengi walikaza A,D,C,B,etc.Ilikuwa ni kimbembeee,maana hakutaka ukisanye hata kama umejaza swali 1 tu.

Wachache tukakusanya baada ya muda wa test tukapata alama 10.

2.Ni mkufunzi kunikuta live band na group mate wangu bin,kumbe anamtakaga halafu dada kakataa.Weee usiombe hii kitu ikukute.Nili carry somo la yule jamaa aisee ktk mazingira ya uonevu kabisaaaa,sitasahau.

Pole,mfuate tena kwa unyenyekevu mwombe msamaha na kujishusha.

Acha tupike chips za jioni huku mtaani maana vyeti vipo sandukuni

Duuh, pole sana mkuu kwa hayo yaliyokukuta.

Kwa kweli, bora chuo kungekuwa na NECTA yake. Hii mifumo ya kutegemea mtu binafsi issue kama hizi hazikwepeki.
 
Pole, anza kumsaidia kubeba briefcase yake kila asubuhi anavoingia kazini, lazima atakufikilia

Ha ha ha, anakuja na gari lake afu hapendagi shobo unaweza kujichoresha balaa
 
Ilo swala tulipitia sana najua situation unayopitia wanaweza tokea comeback ya maana hapo mbele

Najua hali yako hata mm nilikuwa nayo usijali mi nakumbuka yalibaki group na pale teacher ana complicat mambo kinoma nashangaa group letu 8/10 test two 7/10 mzee bonge la come back

Sisi tulikatwa marks kwa vile mtihani ulikuwa umewai kumalizika sio kawaida maswali mengi kakata karibia column mbili chanzo wa kwanza kwenye column anataka kukusanya anasema bado hajamaliza akajua ni wote akakata Marks 3 sasa paper humaliza ukipata tatu una zero anatoa 3 ukipata zero una negative 3 anapunguza kule kwenye coz work ni mkoloni ila alipiga carry robo na wengin alikuwa piga sup kibao kweny UE
Daud G
 
Bilashaka ni first year wewe kupata zilo nikawaida iyo shida ni pale ukipata kale ka NIL ila zero ni number mzee mwalimu anakufikiria kabisa hapo usiwe na shaka mi nilipataga 0/15 business law na mwisho wa siku nilitoboa wala siku sup wala kucarry ingawa li karai langu nalipikia chipsi
 
Bilashaka ni first year wewe kupata zilo nikawaida iyo shida ni pale ukipata kale ka NIL ila zero ni number mzee mwalimu anakufikiria kabisa hapo usiwe na shaka mi nilipataga 0/15 business law na mwisho wa siku nilitoboa wala siku sup wala kucarry ingawa li karai langu nalipikia chipsi

Second year.

Yule sir sidhani, nyie kuna walimu ni nongwa.
 
Second year.

Yule sir sidhani, nyie kuna walimu ni nongwa.
Hata wakwangu alikuwa ivo ivo ila mwisho wa siku nikatoboa na wao ni wanadamu wanaelewaga sema tu mi janafunzi ndio haijiwlewi unamsaidia leo yeye kichwani anamuwaza asha na boom lake akamtoe out kidimbwi au 40.40 lachaz
 
Back
Top Bottom