Roho Mbaya
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 777
- 677
Mimi ni kijana wa miaka 26, Ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto sita kwa sasa najitegemea na nina kazi yangu
Wazazi wangu wote asili ya Mkoa wa Mara, Katika maisha yangu yote tangu mtoto nimekuwa nikimuogopa baba mzazi nahii ni kutoka kuwa mkali,vipigo vya mara kwa mara kwa watoto na hata wazazi wangu(mama na wake wengine wadogo wa baba mzazi). Ambapo hawa wake wadogo hawakuweza kuvumilia walikuwa wakiondoka nyumbani baada ya miezi kadhaa na hii ilikuwa inatokana na ukali wa mzee pamoja na vipigo, Kwangu mimi nimeshuhudia zaidi wake saba wakiondoka nyumbani na kuacha watoto.
Nakumbuka kwangu mimi mwenyewe kuchezea kichapo nilikuwa kidato cha nne, tulikuwa shambani tukilima kwa kutumia ng'ombe, ng'ombe waliacha mstari na kutoka nje kidogo mimi nilishitukizwa na mijaredi(fimbo zinazotengenezwa kwa ngozi ya ng'ombe)
Mpaka muda huu baada ya kumaliza masomo yangu na kuajiliwa lakini baba yangu mzazi bado hajabadilika-:
- ukorofi bado upo palepale
- Ugomvi na majirani
- Anazo kesi nyingi mahakamani
- Hataki ushauri kutoka kwa watu
- Ndugu wote wanamuogopa
Hivi sasa ana miaka zaidi ya hamsini lakini haoneshi mabadiliko
Ushauri wako nifanye nini ili abadilike
Wazazi wangu wote asili ya Mkoa wa Mara, Katika maisha yangu yote tangu mtoto nimekuwa nikimuogopa baba mzazi nahii ni kutoka kuwa mkali,vipigo vya mara kwa mara kwa watoto na hata wazazi wangu(mama na wake wengine wadogo wa baba mzazi). Ambapo hawa wake wadogo hawakuweza kuvumilia walikuwa wakiondoka nyumbani baada ya miezi kadhaa na hii ilikuwa inatokana na ukali wa mzee pamoja na vipigo, Kwangu mimi nimeshuhudia zaidi wake saba wakiondoka nyumbani na kuacha watoto.
Nakumbuka kwangu mimi mwenyewe kuchezea kichapo nilikuwa kidato cha nne, tulikuwa shambani tukilima kwa kutumia ng'ombe, ng'ombe waliacha mstari na kutoka nje kidogo mimi nilishitukizwa na mijaredi(fimbo zinazotengenezwa kwa ngozi ya ng'ombe)
Mpaka muda huu baada ya kumaliza masomo yangu na kuajiliwa lakini baba yangu mzazi bado hajabadilika-:
- ukorofi bado upo palepale
- Ugomvi na majirani
- Anazo kesi nyingi mahakamani
- Hataki ushauri kutoka kwa watu
- Ndugu wote wanamuogopa
Hivi sasa ana miaka zaidi ya hamsini lakini haoneshi mabadiliko
Ushauri wako nifanye nini ili abadilike