Ndugu zangu, Salaam!!
Nipo ktk hatua ya kupiga plasta nyumba yangu. Na kwa kuwa nina fedha kiasi kidogo nimeamua kuanza kupiga plasta kuta za ndani, na baadae nitamalizia upande wa nje.
Ninachoomba kutoka kwenu ni msaada wa kitaalamu, maana mafundi ninaowategemea (fundi wa plasta na wa rangi) wana maoni tofauti.
Fundi wa plasta anasema, plasta nzuri ni ile inayopigwa baada ya kuchanganya cement, mchanga na chokaa. Wakati fundi atakayepaka rangi anashauri kuwa ili aje apake rangi vizuri na kuepuka rangi kubanduka baada ya muda mfupi ni vema plasta iwe inatokana ya mchanganyiko wa mchanga na cement tu.
Ushauri wenu (mafundi na wataalamu wa masuala ya plasta na rangi) ni muhimu sana.
Plasta ipi ni bora??
Nipo ktk hatua ya kupiga plasta nyumba yangu. Na kwa kuwa nina fedha kiasi kidogo nimeamua kuanza kupiga plasta kuta za ndani, na baadae nitamalizia upande wa nje.
Ninachoomba kutoka kwenu ni msaada wa kitaalamu, maana mafundi ninaowategemea (fundi wa plasta na wa rangi) wana maoni tofauti.
Fundi wa plasta anasema, plasta nzuri ni ile inayopigwa baada ya kuchanganya cement, mchanga na chokaa. Wakati fundi atakayepaka rangi anashauri kuwa ili aje apake rangi vizuri na kuepuka rangi kubanduka baada ya muda mfupi ni vema plasta iwe inatokana ya mchanganyiko wa mchanga na cement tu.
Ushauri wenu (mafundi na wataalamu wa masuala ya plasta na rangi) ni muhimu sana.
Plasta ipi ni bora??