Nahitaji uchawi wa kuwaroga wazungu

Nahitaji uchawi wa kuwaroga wazungu

mwehu ndama

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2019
Posts
1,411
Reaction score
5,150
wakuu dunia imechanganya nikama imekata break kwenye mteremko , hata huku ughaibuni tulipo mambo ni patashika, mguu washingo mguu wa roho, kazi nazo zimekuwa gombania goli. Kazi kama kubeba boxi, usafi na delivery ambazo ndizo mkombozi wetu wageni tulio wengi kwa sasa nazo zimevamiwa na wazawa kwa kasi kubwa, maana sasahiv si ajabu kuwakuta wazawa hapa sweden wakikimbizana na mabox, madekio na delivery kwa wingi wa ajabu kuliko ilivyokuwa hapo awali jambo linalosababisha watu kupunguzwa makazini hovyohovyo pasipo mpango.

Hivyo mimi kama mbongo lendi asili, JITU mwitu msitu nimeona nibadili silaha yangu katika vita hii yakusaka maokoto, na rasmi natangaza kuigeukia njia ya ulozi, uchawi na ushirikina kama silaha yangu ya mwisho na kama mpaka ulozi utadunda basi nitarudi bongoland kiroho safi.

Nimekuwa nikisikia kuwa wazungu hawarogeki, Je hili lina ukweli?? Na kama wanarogeka ni njia gani za KUWAROGA kirahisi? maana mpaka hapo navyoandika uzi huu tayari nimeshalitia Shangazi lakiswidi mikononi mwangu, ila nahitaji niliongeze na dozi ya Ulozi juu ili niliongoze kama remote sababu madem waswidi sio rahisi kutoa maokoto, na nikimaliza kuliroga hili nataka nimroge na mtoto wake mkubwa ili asiniletee miyeyusho kwenye harakati zangu za kuchuma vibunda, kabla sijaamia kwa bosi wake na mdogo wake, kwa kifupi nataka cycle yake nzima niipige pigo kuu la kilozi ili nitawale himaya yake yote kama chifu lumanyika.

images%20(2).jpg
 
kama uko serious njoo inbox tuweke mipango sawa... kila kitu kinawezekana
 
Ohooo Wala usiogope wazungu wanalogeka kama wabongo tu jbo lasingi ni wewe kuamua kuwa Mlozi kamili kumbuka nafasi yako itabadilika na kuthami zaidi uchawi automatic sasa ni wewe kuamua.
 
Ohooo Wala usiogope wazungu wanalogeka kama wabongo tu jbo lasingi ni wewe kuamua kuwa Mlozi kamili kumbuka nafasi yako itabadilika na kuthami zaidi uchawi automatic sasa ni wewe kuamua.
Niko tayari kaka nipe maelekezo tu yamsingi
 
Miaka hiyo uliyoishi Sverige unajua kiswedish kiasi cha kuzungumza na shangazi ulilolisema? Una umri gani?
Ki Svenska nakiongea vizuri sana mkuu, in fact ukitaka upate mademu wakiswid usilete ujanja wakuongea kiswidi sana watajua we mjanja, dem mzungu anataka mtu fala so najitaidi kuonekana bwege na mbumbumbu kadri ya uwezo wangu.
 
Uchawi unaaminiwa na watu wajinga na masikini ndo maana ni rahisi mtu wa Chitipa kuamini kalogwa hata akiumwa malaria kuliko mtu wa Masaki let alone wabongo na mizungu.
 
Back
Top Bottom