Mimi ni msichana tayari 32yrs sijawahi kuolewa na sina mtoto. Ninahitaji mume Mkristo tayari kupima VVU pia awe amesoma angalau kidato cha sita, awe ameajiriwa au amejiajiri mwenyewe. Mimi nina elimu ya Advance diploma na nimeajiriwa na kampuni fulani hapa Dar es salaam. Samahani najua wengi mtaniponda nakadhalika lakini mimi niko serious kabisa nimeshachoka maisha ya upweke na ubusy wa kazi kiasi kwamba hata muda wa kukutana na watu nakosa. Sitakasirika kwa wale watakaoniponda ila kwa wale walioko serious ni tumie message kwenye profile yangu then tutaendelea kuwasiliana. Naomba tafadhali uelewe niko serious sana kuhusu hili swala na siyo kwamba nina tabia mbaya au labda muhuni au mi mwenyewe sina mvuto hapana, nadhani kwa kadri tutakavyozidi kufahamiana utanifahamu na kunielewa vizuri. Niko nasubiri Private message (PM) kwa wale tu walioko serious karibuni.