Dirham
JF-Expert Member
- Dec 26, 2016
- 491
- 536
Naanza kwa kumshukuru Mungu kwa kutupa uzima na afya njema mpka wakati huu. Pili napenda kutoa salam zangu zikufikie wewe unaesoma thread hii popote pale ulipo na mungu akubariki sana.
Mimi ni kijana na nina familia ya mke na watoto wawili. Nimshukuru mungu baada ya kumaliza elimu yangu ya chuo ngazi ya shahada ya kwanza nilipata kazi mkoan Tanga maisha yakaendelea, niliweza kukidhi haja mbalimbali za familia yangu na kuendesha maisha. Baada ya mwaka mmoja wa kazi nilianza kupatwa na hali ya ajabu sana, kwanza kuwa na usingizi mzito sana asubuhi pili kutokuwa na morali ya kazi.
Kwa muda mrefu sana nipipigana na hii hali ambayo ilipelekea kutokuwa na ufanisi mzuri katika utendaji kazi. Nilijaribu kutafuta ushauri kila mtu alisema lake nilojikaza na hatimae miaka miwili ikapita lakini katika hali ngumu sana pesa haikai na niseme tu mimi sina matumizi mabaya ya pesa halafu si mtu wa anasa.
Nikajikuta naingia kwenye madeni ambayo yalipelekea mshahara wangu kupinguwa sana na hata kufikia hatua mshahara hautoshi hali ilikuwa ni mbaya sana. Ni muda mrefu sana nimekuwa mtu wa kutopata usingizi usiku, nilipambana kwa hali zote lakini haikiwa riziki yangu nikasimamishwa hivyo nikarudi nyumbani.
Nimejitahidi kutafuta kazi lakini nimekosa ilifikia point nikaona bora nijiue lakini nikifikiria wanangu na mama yao wananitegemea. Inabidi nipambane kwa ajili yao sina kazi ikabidi nianze kudeal na vibarua nipate 2000 watoto wangu wale. Ni maosha magumu sana haya najua ni mitihani nami sikati tamaa.
Lengo la kuandika historia fupi ya nilikopitia mpaka hapa nilipo sasa ni kutaka msaada wenu wana JF
1. Tangu mwanzo wa hii wiki imekuwa ngumu sana kupata vibarua imepelekea ugumu sana kupata chakula. Nina watoto wawili wadogo mkubwa ana miaka 5 na mdogo ana miaka 3 naumia sana roho ina niuma sana nikiwaona nashindwa kuwapa milo yote mitatu. Jana usiku wamelalia uji na leo asubuhi nimeondoka sijaacha kitu kwani hata senti sina. Ndugu zangu kwa mwenye uwezo wa kunistiri familia yangu leo ipate chakula nitashukuru sana.
NB.:Nakushukuru kwa kusoma thread yangu na mungu akubariki sana na uwe na siku njema.
Amiin
Kwa alie teyari kunipa msaada wa aina yoyote naomba tuwasiliane PM
Mimi ni kijana na nina familia ya mke na watoto wawili. Nimshukuru mungu baada ya kumaliza elimu yangu ya chuo ngazi ya shahada ya kwanza nilipata kazi mkoan Tanga maisha yakaendelea, niliweza kukidhi haja mbalimbali za familia yangu na kuendesha maisha. Baada ya mwaka mmoja wa kazi nilianza kupatwa na hali ya ajabu sana, kwanza kuwa na usingizi mzito sana asubuhi pili kutokuwa na morali ya kazi.
Kwa muda mrefu sana nipipigana na hii hali ambayo ilipelekea kutokuwa na ufanisi mzuri katika utendaji kazi. Nilijaribu kutafuta ushauri kila mtu alisema lake nilojikaza na hatimae miaka miwili ikapita lakini katika hali ngumu sana pesa haikai na niseme tu mimi sina matumizi mabaya ya pesa halafu si mtu wa anasa.
Nikajikuta naingia kwenye madeni ambayo yalipelekea mshahara wangu kupinguwa sana na hata kufikia hatua mshahara hautoshi hali ilikuwa ni mbaya sana. Ni muda mrefu sana nimekuwa mtu wa kutopata usingizi usiku, nilipambana kwa hali zote lakini haikiwa riziki yangu nikasimamishwa hivyo nikarudi nyumbani.
Nimejitahidi kutafuta kazi lakini nimekosa ilifikia point nikaona bora nijiue lakini nikifikiria wanangu na mama yao wananitegemea. Inabidi nipambane kwa ajili yao sina kazi ikabidi nianze kudeal na vibarua nipate 2000 watoto wangu wale. Ni maosha magumu sana haya najua ni mitihani nami sikati tamaa.
Lengo la kuandika historia fupi ya nilikopitia mpaka hapa nilipo sasa ni kutaka msaada wenu wana JF
1. Tangu mwanzo wa hii wiki imekuwa ngumu sana kupata vibarua imepelekea ugumu sana kupata chakula. Nina watoto wawili wadogo mkubwa ana miaka 5 na mdogo ana miaka 3 naumia sana roho ina niuma sana nikiwaona nashindwa kuwapa milo yote mitatu. Jana usiku wamelalia uji na leo asubuhi nimeondoka sijaacha kitu kwani hata senti sina. Ndugu zangu kwa mwenye uwezo wa kunistiri familia yangu leo ipate chakula nitashukuru sana.
NB.:Nakushukuru kwa kusoma thread yangu na mungu akubariki sana na uwe na siku njema.
Amiin
Kwa alie teyari kunipa msaada wa aina yoyote naomba tuwasiliane PM