Nahitaji msaada wenu kwenye hili

Nahitaji msaada wenu kwenye hili

Broussard

Member
Joined
Jan 30, 2021
Posts
28
Reaction score
29
Habari za muda huu wakuu, mimi ni member mzoefu ila nimeamua kuja na Id nyingine ili niweze kuwa huru zaidi kwenye hili lililonifanya niandike huu uzi. Kuna jambo linanitatiza sana nahitaji ushauri juu ya maamuzi niliyoyafikia kama ni sahihi au sio sahihi.

Ni hivi wakuu, nipo kwenye mahusiano na dada mmoja huu mwaka wa pili tupo pamoja lakini mwenzangu huwa apendi kabisa kipengele cha kufanya mapenzi(tupo mikoa tofauti ila huwa tunakutana kila baada ya miez miwili) yeye ni mwanafunzi wa chuo (afya/udaktari). Nilijaribu kuchunguza kwanini hapendi kuna mda hana ham kabisa imagine mnaweza toka ukalipa lodge lakin mwisho wa siku mnaishia kulala tu mpaka kunakucha bila ya kufanya chochote.

Nilivumilia hali hii kwa mda kwakuwa ni mwanamke nnaempenda, akiwa on mood anatoa ushirikiano vizuri tu lakin baadae utamuona analia anasema nimemuumiza nambembeleza anatulia. Baada ya mda kidogo nilikuja kugundua tatzo lakini hadi sasa hajawahi kunieleza(nadhani sio rahisi kwake kuliweka hili wazi na linamtesa sana kwa sababu kuna mda unaona kabisa anafosi ili nisihisi kitu lakini afanikiwi). Nilikuja kugundua kuwa amekeketwa na anawahi kuwa mkavu ndio maana analalama kuwa anaumia.

Huu ukweli uliniumiza sana kwa kuwa nampenda sana sikujali nikasema ahsante Mungu kwa huyu ulienipa sina budi kuendelea nae kwa kuwa sio yeye alipenda awe hivyo. Siku zikazidi kusonga mbele nikawa naona ni kawaida, kuna siku tulikutana tukawa pamoja kwa siku kama 5 hivi, hali haikuwa shwari kabisa nikamuuliza kama kuna tatzo lolote nieleze hupaswi kunificha mimi ndio mwanaume wako nakumbuka alilia sana lakin hakunieleza chochote.

Sasa kubwa ni hili wakuu tuna takribani miezi kama 7 hivi hatujafanya na tunakutana mara nyingi tu ila jibu lake ni kuwa hataki kwa sasa na ukimuuliza sana anasema yeye hajui sababu ni nini. Binafsi naona kama anakosea sana kwa sababu namgharamia na kumthamini nikiamini ni mwanamke wa ndoto zangu bila ya kujali hali yake lakini kwa mwenendo huu tena bila kuweka wazi sababu hasa ni nini nimefika mahali nimemkatia tamaa na kuamua bora tu nimuache huenda sio fungu langu. Nagharamika kusafiri kila mara and all bills for nothing inanihuzunisha mno.

Kwa upande wa tabia na mienendo mingine ni wife material kabisa na ndio maana nnampenda(nilimbikiri mimi) . Mawasiliano kwetu hayajawai kuyumbishwa na chochote(strong) sijawahi kuona dalili za yeye kunicheat nadhani inachangiwa pia na hali yake ya kutokupenda sex(sio mtu wa kujichanganya kabisa).
Nawaza sana baadae nikija kumuoa itakuwaje, yataendelea haya haya nayoyaona sasa au atabadilika. Kuvumilia hali yake naweza kwa mda fulani lakin changamoto ni ikiwa ni kwa mda mrefu maana mpaka sasa ni mda umepita na ukiuliza mwisho wa haya ni lini jibu ni sijui na sababu sijaambiwa.

Wakuu haya maamuzi niliyoyafikia ya kumuacha ni sahihi au sio sahihi? Nahitaji ushauri zaidi kwenye hili nifanyaje wakuu?

NB: ukeketaji unawaumiza sana wahusika kimwili na kisaikolojia, tukemee kutokomeza hali hii kwenye jamii zetu. Humfanya ke asijiamini, kupoteza ham ya tendo. Hii inampelekea kuwa na zile kauli za “love is not about sex” kwa sababu anajua kabisa huko yeye ni maumivu tu.
 
kama tatizo umelingua na umekaa kimya hapo sasa ni wewe ndio mwenye makosa inatakiwa uchukue muda taratibu na kwa akili nyingi huku ukianzia mbali sana na ukionesha kuwa unapenda au hautakuwa na unyanyapaa kwa mtu akiwa amekeketwa hivyo uoneshe kuwa hautakuwa na tatizo then ndio taratibu umwambie unahisi kama amekeketwa ila na bado unampenda sana cha msingi akili kwa kinywa chake halafu uone kama bado ataendelea kuumia maana mda mwingine huenda pale anapokuwa uchi mbele yako hajiamini na ndoi sababu inayopelekea kutopata hisia ila akiwa wazi basi ile hali ya kutojiamini kwako itaisha na halafu atakufurahia
 
kama tatizo umelingua na umekaa kimya hapo sasa ni wewe ndio mwenye makosa inatakiwa uchukue muda taratibu na kwa akili nyingi huku ukianzia mbali sana na ukionesha kuwa unapenda au hautakuwa na unyanyapaa kwa mtu akiwa amekeketwa hivyo uoneshe kuwa hautakuwa na tatizo then ndio taratibu umwambie unahisi kama amekeketwa ila na bado unampenda sana cha msingi akili kwa kinywa chake halafu uone kama bado ataendelea kuumia maana mda mwingine huenda pale anapokuwa uchi mbele yako hajiamini na ndoi sababu inayopelekea kutopata hisia ila akiwa wazi basi ile hali ya kutojiamini kwako itaisha na halafu atakufurahia

Kwa hiyo nijipe muda kwenye hili? Ukweli ni kwamba nampenda na namuonesha hilo kwa kila namna hata hili la kuweza kuvumilia for 7 months na tunakutana mara kwa mara linathibitisha upendo wangu kwake na mpaka sasa sijapunguza chochote kama kumjali na kumpenda.

Sipendi kabisa hiyo hali imuumize sema ndio hivo unamuona hajiamini kabisa.
 
  • Thanks
Reactions: lup
Jaribu kufuatilia hata kwa wataalamu wa Mambo ya wanawake. Tatizo Hilo sio kwa sababu amekeketwa. Wapo wanawake waliokeketwa lakini hamu ya kushiriki tendo wanayo. Fanya utafiti kwa lengo la kubaini namna gani unaweza kumsaidia na mwishoe muishi kwa amani.

Trust me brother, unapokuwa na mwanamke asiyewaka tamaa ya ngono, akili yako inakuwa na utulivu mwingi pale unapopambana kuzisaka pesa, maana huwazi kuhusu kuibiwa tunda lako.

Tafiti, msaidie, tambua namna utaishi naye (Kama utaweza) finally OA.
 
Habari za muda huu wakuu, mimi ni member mzoefu ila nimeamua kuja na Id nyingine ili niweze kuwa huru zaidi kwenye hili lililonifanya niandike huu uzi. Kuna jambo linanitatiza sana nahitaji ushauri juu ya maamuzi niliyoyafikia kama ni sahihi au sio sahihi.

Ni hivi wakuu, nipo kwenye mahusiano na dada mmoja huu mwaka wa pili tupo pamoja lakini mwenzangu huwa apendi kabisa kipengele cha kufanya mapenzi(tupo mikoa tofauti ila huwa tunakutana kila baada ya miez miwili) yeye ni mwanafunzi wa chuo (afya/udaktari). Nilijaribu kuchunguza kwanini hapendi kuna mda hana ham kabisa imagine mnaweza toka ukalipa lodge lakin mwisho wa siku mnaishia kulala tu mpaka kunakucha bila ya kufanya chochote.

Nilivumilia hali hii kwa mda kwakuwa ni mwanamke nnaempenda, akiwa on mood anatoa ushirikiano vizuri tu lakin baadae utamuona analia anasema nimemuumiza nambembeleza anatulia. Baada ya mda kidogo nilikuja kugundua tatzo lakini hadi sasa hajawahi kunieleza(nadhani sio rahisi kwake kuliweka hili wazi na linamtesa sana kwa sababu kuna mda unaona kabisa anafosi ili nisihisi kitu lakini afanikiwi). Nilikuja kugundua kuwa amekeketwa na anawahi kuwa mkavu ndio maana analalama kuwa anaumia.

Huu ukweli uliniumiza sana kwa kuwa nampenda sana sikujali nikasema ahsante Mungu kwa huyu ulienipa sina budi kuendelea nae kwa kuwa sio yeye alipenda awe hivyo. Siku zikazidi kusonga mbele nikawa naona ni kawaida, kuna siku tulikutana tukawa pamoja kwa siku kama 5 hivi, hali haikuwa shwari kabisa nikamuuliza kama kuna tatzo lolote nieleze hupaswi kunificha mimi ndio mwanaume wako nakumbuka alilia sana lakin hakunieleza chochote.

Sasa kubwa ni hili wakuu tuna takribani miezi kama 7 hivi hatujafanya na tunakutana mara nyingi tu ila jibu lake ni kuwa hataki kwa sasa na ukimuuliza sana anasema yeye hajui sababu ni nini. Binafsi naona kama anakosea sana kwa sababu namgharamia na kumthamini nikiamini ni mwanamke wa ndoto zangu bila ya kujali hali yake lakini kwa mwenendo huu tena bila kuweka wazi sababu hasa ni nini nimefika mahali nimemkatia tamaa na kuamua bora tu nimuache huenda sio fungu langu. Nagharamika kusafiri kila mara and all bills for nothing inanihuzunisha mno.

Kwa upande wa tabia na mienendo mingine ni wife material kabisa na ndio maana nnampenda(nilimbikiri mimi) . Mawasiliano kwetu hayajawai kuyumbishwa na chochote(strong) sijawahi kuona dalili za yeye kunicheat nadhani inachangiwa pia na hali yake ya kutokupenda sex(sio mtu wa kujichanganya kabisa).
Nawaza sana baadae nikija kumuoa itakuwaje, yataendelea haya haya nayoyaona sasa au atabadilika. Kuvumilia hali yake naweza kwa mda fulani lakin changamoto ni ikiwa ni kwa mda mrefu maana mpaka sasa ni mda umepita na ukiuliza mwisho wa haya ni lini jibu ni sijui na sababu sijaambiwa.

Wakuu haya maamuzi niliyoyafikia ya kumuacha ni sahihi au sio sahihi? Nahitaji ushauri zaidi kwenye hili nifanyaje wakuu?

NB: ukeketaji unawaumiza sana wahusika kimwili na kisaikolojia, tukemee kutokomeza hali hii kwenye jamii zetu. Humfanya ke asijiamini, kupoteza ham ya tendo. Hii inampelekea kuwa na zile kauli za “love is not about sex” kwa sababu anajua kabisa huko yeye ni maumivu tu.
Pole kwa maswahibu. Nadhani ulitakiwa kusimama kwa nafasi ya mpenzi wako. ingekua yamekukuta ww binafsi ungechukua hatua gani. Kwanza ni dhahiri ulishalitambua kiini cha kutopenda kwake kufanya tendo la kujaamiana. (Amekeketwa na Anakua mkavu ndani ya uke wake). Kwa hiyo ww mwanaume unaejidai rijali unasubiri mpenzi wako akuandikie barua ndo uchukue hatua? Unatakiwa umshauri kwenda kwa wataalam kwa ajli ya kutatua changamoto zake. Hilo tatizo lake linadhibitiwa iwe kwa madaktari au kwa nataalamu wa tiba za asili na sunna.
 
Jaribu kufuatilia hata kwa wataalamu wa Mambo ya wanawake. Tatizo Hilo sio kwa sababu amekeketwa. Wapo wanawake waliokeketwa lakini hamu ya kushiriki tendo wanayo. Fanya utafiti kwa lengo la kubaini namna gani unaweza kumsaidia na mwishoe muishi kwa amani.

Trust me brother, unapokuwa na mwanamke asiyewaka tamaa ya ngono, akili yako inakuwa na utulivu mwingi pale unapopambana kuzisaka pesa, maana huwazi kuhusu kuibiwa tunda lako.

Tafiti, msaidie, tambua namna utaishi naye (Kama utaweza) finally OA.
Umeeleza ukweli mkuu binafsi utulivu upo ila changamoto ni namna ya kumsaidia ili tuende sawa.
Huyo ni mzuri kwa sababu bodaboda hawataweza kufua dafu.(Napita)
imebidi nicheke tu
 
Pole kwa maswahibu. Nadhani ulitakiwa kusimama kwa nafasi ya mpenzi wako. ingekua yamekukuta ww binafsi ungechukua hatua gani. Kwanza ni dhahiri ulishalitambua kiini cha kutopenda kwake kufanya tendo la kujaamiana. (Amekeketwa na Anakua mkavu ndani ya uke wake). Kwa hiyo ww mwanaume unaejidai rijali unasubiri mpenzi wako akuandikie barua ndo uchukue hatua? Unatakiwa umshauri kwenda kwa wataalam kwa ajli ya kutatua changamoto zake. Hilo tatizo lake linadhibitiwa iwe kwa madaktari au kwa nataalamu wa tiba za asili na sunna.
Ahsante kwa ushauri mkuu ndio maana nimelileta hili jukwaani ili nipate ushauri zaidi.
 
Aisee watu wanashida sana

Mimi niseme tuu hata kwenye hilo kuna njia ya kutokea n swala la muda
 
Kwa hiyo nijipe muda kwenye hili? Ukweli ni kwamba nampenda na namuonesha hilo kwa kila namna hata hili la kuweza kuvumilia for 7 months na tunakutana mara kwa mara linathibitisha upendo wangu kwake na mpaka sasa sijapunguza chochote kama kumjali na kumpenda.

Sipendi kabisa hiyo hali imuumize sema ndio hivo unamuona hajiamini kabisa.
fanya niliyokuambia utanishukuru baadaye na yeye ataongeza upendo zaidi
 
Pole brother pray hard litapita muombe mungu akupe njia katika hili maana kajua unaliweza ndio maana kakupitisha
 
Aiseee vyema kama uliligundua tatizo, na kumbuka unapoligundua tatizo inatakiwa kugundua na njia.
Hivyo cha msingi usimwache/muoe ila sio saivi
jaribu kutulia na kuendana naye na mambo yatakwenda shwari
Na hata hivyo unaweza kumweleza juu ya hilo tatizo lake naye atafunguka zaidi kukuelezea
 
Kukeketwa hakuondoi hamu hapo lazma ana shida ya ziada au kisaikolojia.
Ma be keshawahi nyanyaswa kijinsia kwa kubakwa na akapata maumivu.
Cha kufanya nenda hospitali achinguzwe atapewa booster antenna isome tena
 
Back
Top Bottom