Ngosha hizo kama ni gunia 50 na kila gunia linasimamia kilo 100 basi hizo ni Tani 5. Mkuu sikushauri ulete huku bora uuzie huko huko mpaka ufike huku na hizo Tani 5 utakuwa umeingia gharama kubwa mno. Biashara ya mahindi ni ngumu mno japo watu wanaichukulia kirahisi tu unaweza leta mzigo wako huo ukakuta bei zimeshuka huku hapo ndio utajuta kuingia kwenye biashara hii. Umefanya Vizuri kuuliza kwa ngosha siku ukiwa na matani kama 30 nakuendelea nichek tufanye kazi. Ila ata hapo Mbeya huwa nafika kuchukua mzigo. Ngosha karibu sana