Nahisi nilimegewa


Duh....hiyo hadithi ni kubuni tu.
 
 
Nakumbuka thread moja humu. Jamaa aliandika kwamba kuoa mwanamke aliezaa ni kukubaliana na kuishi na mwanaume mwenza.

Atume nauli hadi Marekani. Alale nae nyumba moja wiki mbili. Unadhani lengo ni kumwona mtoto tu! Jiongeze bhana, umemegewa.

Ni vigumu sana kugharimia hiyo safari kuonesha tu mtoto. Alikumbuka mambo yao na hawakuachana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha

Ama kweli haya mambo hayana mjanja ... yaani licha ya kuwa guru katika kuwatafuna wadada lakini ukadiriki kuchezewa akili kizembe namna hiyo ...dahh !!!

Yaani hapo inaonyesha wazi kuwa huyo jamaa aliyemzalisha manzi wako wawakati huo alikuwa anamtafuna asubuhi na mchana atakavyo " ... Ulifanya makosa sana kumruhusu huyo mwanamke aende kumfuata mzazi mwenzio " .. kama kweli huyo mzazi mwenzie alikuwa na shida ya dhati ya kumuona mtoto wake alipaswa kuja yeye kumuona huko mlipokuwa mnaishi _ ...

Yakupasa sasa utambue kwamba kitendo cha yule mwanamke kumfuata mzazi mwenzake kili kuwa kina maanisha kwamba " walikuwa wanatafuta sehemu tulivu ambayo itawawezesha kupasha kiporo bila bugdha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyani Ngabu, kumbuka unapooa mwanamke au kuolewa na mwanaume aliyezaa mtoto/watoto, mambo hayo ni lazima yatokee. Hivyo inabidi uwe na moyo wa chuma, labda mmoja wapo awe ametangulia mbele za haki ndo hayawezi kutokea. Ukubali usikubali kumegewa ni lazima tena kiulaini.
 
Hayo ndio majaribu ayapatayo mtu anayeoa single mother kwasababu huwezi kuzuia mawasiliano Kati ya Baba na mtoto watu watakuona kichaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana...

Labda nikuulize kitu, ingekua ni wewe mama mtoto wako mliyeachana anakuletea mtoto umuone na unakaa nae kwa week mbili, ungemmega au ungemucha?

Ukiwa na jibu, basi lolote linawezekana...


Cc: mahondaw
 

Ndugu yangu huyo mwanamke bado alikuwa anampenda baba mtoto tena sana. wewe uliingia tu by the way sabau aliona jamaa anazingua.

wewe fikiria, mwanaume kampa mimba na kumtelekeza tangu ikiwa na miezi mitano, leo hii anamkuja kumdemand demu ampelekee mtoto tena siyo Kimara walikopeana hiyo mimba bali Canada!!!! kwa nn asimgomee kwa kumwambia kama kweli unataka kumuona mtoto njoo umuone huku mi siwezi kuja huko na kwa sasa nina mchumba wangu hawezi niruhusu.
Yaani wanawake bwana sometimes wana bore sana..... ila acha tu tuwavumilie maana ni mama zetu na dada zetu.

Jamani niwieni radha binafsi nawapenda sana wanawake ila hii ni hasiran tu
 
Pole sana mtoa mada lakini huu ushauri wa Chupaku ndio ushauri mzuri ufuate. Usimuache kwa mambo ya kufikirika tu amini usiamini inawezekana hawakushiriki tendo au walishiriki lakini hangaikia moyo sio mwili. Kama moyo wake uko kwako hilo ndilo la muhimu zaidi.
 
Binafsi mimi kama mm nisingempeleka mtoto kabisaa, mimba ina miezi hadi unajifungua mtu hajui chochote, mtoto anakaribia kumaliza mwaka unamdai, halafu nakuletea tu, sijafanya hiyo kazi, halafu hapo ndio huwa tunafeli sana wanawake tayari una mwanamme mwingine na una furaha nae kwann uhangaike eti kisa tu umezaa nae,mtoto ni wake hilo halibadiliki lkn unapaswa kumweshimu ulo nae kwa wakati huo, angefunga safar aje amuone mtoto wake -period
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…