Nahisi maumivu makali tumboni na mgongoni

puker

JF-Expert Member
Nov 22, 2018
940
1,847
Habari za muda huu wanajamvi.

Niingie moja kwa moja kwenye lengo mahususi la uzi huu. Kama kichwa cha habari kinavyoeleza.

Leo ni siku ya tatu kuna maumivu yamezuka ghafla mithili ya mtu aliyeungua na mafuta ya moto au mvuke katika sehemu ya tumbo langu upande wa kushoto.

Maumivu hayo yalianzia mgongoni kwa mbali nikahisi ni kawaida labda ni uchovu na pilika za mjini. Nikapuuza.

Lakini kadri masaa yanavyozidi kusogea yanaongezea mpaka kufika maeneo ya tumboni upande huo huo wa kushoto.

Cha ajabu hakuna vipele, wekundu wala dalili yoyote inayoonesha kama ngozi au mwili una hitilafu. Nina mpango wa kwenda kucheki hospital kesho Mungu akinijalia uhai. Lakini pia nimeeleza hata labda kuna hatua za kuchukua ili tatizo lisiendelee kuwa kubwa.

Pia nikitathmini siku za karibuni hakuna Jambo au tukio lolote linaloweza kusababisha maumivu haya.

Naombeni msaada tafadhali. Yani hata nguo naona inaniumiza.
 
Kwanza pole sana mkuu kwa maswahibu hayo....kwa namna unavoeleza ni ngumu kupata clear medical history ambayo inaweza kumsaidia daktar moja kwa moja kupata ufumbuzi wa tatizo lako unaweza pia kueleza hayo maumivu yana ambatana na dalili zingine zipi ukiachia mbali maumivu ya tumbo ambayo yapo zaidi upande wa kushoto huku yakianzia mgongoni.....hivo nakushauri kamuone daktar ana kw ana atakusaidia kwa kupata clear medical hx...unawez kutumia dawa za kutuliza maumivu mkuu....pole sana
 
Kwanza pole sana mkuu kwa maswahibu hayo....kwa namna unavoeleza ni ngumu kupata clear medical history ambayo inaweza kumsaidia daktar moja kwa moja kupata ufumbuzi wa tatizo lako unaweza pia kueleza hayo maumivu yana ambatana na dalili zingine zipi ukiachia mbali maumivu ya tumbo ambayo yapo zaidi upande wa kushoto huku yakianzia mgongoni.....hivo nakushauri kamuone daktar ana kw ana atakusaidia kwa kupata clear medical hx...unawez kutumia dawa za kutuliza maumivu mkuu....pole sana
Nashukuru kaka..ubarikiwe
 
Poleh sana, ni vizuri ukaenda hospitali ili ufanye vipimo upate uhakika wa kinachokusumbua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom