Nahamia Botswana, naomba mawili matatu kuhusu huko

Nahamia Botswana, naomba mawili matatu kuhusu huko

Complicator

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2013
Posts
2,207
Reaction score
3,604
Nimebahatika kupata kazi katika chuo kimoja cha elimu cha Botswana, baada ya kukosa ajira Tanzania.

Sasa nauliza wadau mnaojua machache kuhusu nchi hii mnijuze.
 
Ingia google utafahamu mengi
ukifika huko utuambie fursa zilizopo tukufuate mkuu
nakutakia safari njema.
 
Botswana ni nchi nzr...inayoendelea kusini mwa africa..idadi ya watu ni kama..mkoa wa arusha...kuna jua na baridi kali...kuna mambo mengi..inafanana na namibia...pako poa...safar njema...
kama hujaoa ukioa mwanamke wa kule na kuzaa nae sahau kuhusu watoto,kama ikifikia wakat wa kurud tz.utarud mwenyewe tuu watoto ni wa mwanamke.pili kama ww ni mgonga mvinyo jiandae kunoa meno kwani kule kila bar lazima iwe na burcher.ukichukua kimada lazima ukipige nyama ya ukwelii kwanza ndiyo vinywaji vianze.
 
Nimebahatika kupata kazi katika chuo kimoja cha elimu cha Botswana, baada ya kukosa ajira Tanzania.

Sasa nauliza wadau mnaojua machache kuhusu nchi hii mnijuze.

Ukiweza kufunga zipu mbele ya watoto chocolate color, shepu za uhakika, chuchu konzi, utatoka mkuu Othewise tunasubiri utuletee mbegu kama utabahatika kurudi mzima.
 
Karibu ughaibuni. Elimu ni ile inayokuwezesha kutawala mazingira yako. Ikuwezeshe kuishi popote katika sayari hii na kustawi. Sasa naweza kusema shuleni ulielimika. Wengi wenu mkifika Dar mnajiona mko "on top of the world". Mnajiona mmepata "trophy" maishani. Wewe ni mfano wa kuigwa kwa wadogo zetu. Hapo Botswana leseni ya udereva inaisha muda wake baada ya miaka 5, siyo mitatu kama Bongo. Gaborone kuna parking lots za kutosha. Hautolipia tena ku-park kwenye ardhi ya Mungu. Gaborone ina wakaazi kama lakh 3 hivi na magari machache lakini barabara zao ni pana ajabu. Hakuna foleni. Unaweza kukaa sehemu yoyote ya mji na kuamka saa 12:30 asubuhi, ukaoga, ukala kifungua kinywa na bado ukawahi kazini. Malls kubwa ziko kila mahali. Siyo Dar yenye wakaazi mil 5 lakini ina ka-Mlimani City tu. Cost of living iko chini ukilinganisha na Afrika Kusini.
 
Kuwa makini sana na ngono uzembe, maana watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kati ya umri wa miaka 15- 49 ni asilimia 24.8. Akili kichwani kwako ndugu, maana wanawake wa kitswana sio wachoyo wa viungo vyao ...haswa kwa wageni (foreigners).
Kila la heri mkuu.

PS: Kaka yangu alikuwa Daktari huko Botswana miaka ya 1989....kwa bahati mbaya alipata maambukizi ya UKIMWI huko. Alifariki mwaka 1997. Alituachia majonzi makubwa sana katika familia yetu. Mke wake alifariki mwaka 2012 na kuwaacha watoto bila wazazi. Kwa kweli nilipachukia sana Botswana. Ila Mungu ni mwema.
 
nina karafiki ka kike kabotswana... ila naona giza giza tu hapa.... yani sielewi elewi... hadi mwili umekosa nguvu...
 
Back
Top Bottom