Nafikiria kusoma Diploma ya Meno

Nafikiria kusoma Diploma ya Meno

idrissi

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2016
Posts
512
Reaction score
433
Habari ya muda wadau wa elimu.

Mimi ni kijana wa miaka 26 na nina Diploma ya Clinical Medicine ambayo nimehitimu 2020..tangu nipo mtaani kufanya kazi sehemu mbali mbali(vijiwe) nimejikuta sina chochote cha maana ninachofanya kwa sababu malipo madogo na kazi zenyewe za kubabaisha sana.

Nina rafiki yangu yeye ni ana Diploma ya meno na tulimaliza wote mwaka mmoja ajabu mpaka sasa ana mafanikio makubwa sana kwanza anapofanya kazi ana thaminiwa na anapewa hela nzuri si chini ya laki 9 kwa mwezi(yeye hulipwa kwa kichwa).

Kiufupi ana maendeleo makubwa kiasi mpaka ananihurumia mimi Tabibu wakati tulipokua tunasoma nilikua najiona niko juu sasa niko vibaya kiuchumi.

Kijiwe ninachofanya kazi na vijiwe mbali mbali nilivyopita hakuna mshahara unalipwa kutokana na uanchoingiza unajikuta kwa mwezi unapata kiasi cha 200k-280k na unakopwa juu na ajira za serikali nimeomba nimeangukia pua.

Sasa wazo nililopata ni kusoma hiyo C.Dentisry je, kwa ufaulu wangu huu nilio nao wa Physics C,Bios B ,Chemistry C naweza kupata chuo cha serikali nikajiuma tena kwa miaka 3 na huku nikitumia cheti changu cha C.O kujikidhi mahitaji?

NB;Sifikiri Digrii ya Udaktari kwa sababu ya Hela kua kubwa,ushindani mkubwa na GPA yangu nadhani siwezi kukompiti...

Naomba ushauri katika hilo je,nipo sahihi au nimevurugwa nahitaji ushauri wa kitaalamu

Matusi sitaki naomba ushauri
 
Habari ya muda wadau wa elimu.

Mimi ni kijana wa miaka 26 na nina Diploma ya Clinical Medicine ambayo nimehitimu 2020..tangu nipo mtaani kufanya kazi sehemu mbali mbali(vijiwe) nimejikuta sina chochote cha maana ninachofanya kwa sababu malipo madogo na kazi zenyewe za kubabaisha sana.

Nina rafiki yangu yeye ni ana Diploma ya meno na tulimaliza wote mwaka mmoja ajabu mpaka sasa ana mafanikio makubwa sana kwanza anapofanya kazi ana thaminiwa na anapewa hela nzuri si chini ya laki 9 kwa mwezi(yeye hulipwa kwa kichwa).Kiufupi ana maendeleo makubwa kiasi mpaka ananihurumia mimi Tabibu wakati tulipokua tunasoma nilikua najiona niko juu sasa niko vibaya kiuchumi.

Kijiwe ninachofanya kazi na vijiwe mbali mbali nilivyopita hakuna mshahara unalipwa kutokana na uanchoingiza unajikuta kwa mwezi unapata kiasi cha 200k-280k na unakopwa juu na ajira za serikali nimeomba nimeangukia pua.

Sasa wazo nililopata ni kusoma hiyo C.Dentisry je, kwa ufaulu wangu huu nilio nao wa Physics C,Bios B ,Chemistry C naweza kupata chuo cha serikali nikajiuma tena kwa miaka 3 na huku nikitumia cheti changu cha C.O kujikidhi mahitaji?

NB;Sifikiri Digrii ya Udaktari kwa sababu ya Hela kua kubwa,ushindani mkubwa na GPA yangu nadhani siwezi kukompiti...

Naomba ushauri katika hilo je,nipo sahihi au nimevurugwa nahitaji ushauri wa kitaalamu.

Matusi sitaki naomba ushauri
Ukikosa mchongo kwenye hiyo diploma ya meno utaenda kusomea nini tena?
 
Nasimama hapa.

Mtoa mada hujasikia yule dogo wa Mtwara aliyemlima mwl barua ili aache masomo?
Dogo alitambua kipaji chake akafanya maamuzi bila kushurutishwa.

Kila mtu ana njia zake za kutoka, ni kujitambua na kupambania kile unachoamini na sio kupiga chabo kwa wengine, hapo lazima upotee sababu hujui mwenzako anapambana vipi kuwa vile unavyomuona.
 
Write your reply...mafanikio hayatokani kozi bali mindset yako,tumie CA kuvumbua kipato chako nje ya kuajiriwa,ulishawah kujiuliza siku rafki yako huyo centre aliyoajiriwa ikipata vichwa vichache zaidi atandelea kupata 900
 
Fanya procedures za Dental kwa wingi kwa muda Fulani ukishajua upige na part-time kwenye Dental unit huku unakomaa CO yako muda wa ziada unaenda kwenye vijiwe vya Dental

Jifunze na kutengeneza Meno bandia pia mjini mipango mwamba

Ukiwa sawa degree kasome DDS kurudi tena 3 Miaka mitatu nyuma Huenda hiyo dental yenyewe ikakosa soko uzuri wake

Dental ina surgery na Cosmetics

Zamani Dental ilitazamwa kama Dying cadle ujue
 
Watu mnachekesha Sana, badala ya kusomea teknolojia uwe na uwezo wa kufikiri mkubwa unawaza kusomea jino, khaaaaaaa.
Muhimbili Wanatoa Dental laboratory technologist

Ukiwa free ulizia Bei ya dental implants na teeth braces kwa Bei ya hapa Nyumbani tuuu

Kisha uwe huru kuidogosha fani ya Afya ya kinywa na meno
 
Watu mnachekesha Sana, badala ya kusomea teknolojia uwe na uwezo wa kufikiri mkubwa unawaza kusomea jino, khaaaaaaa.
Kozi ya meno inahusisha vitu vingi..magonjwa yote ya kinywa,kung'oa meno,kuziba na kuweka ya bandia uhitaji mkubwa sana kama hujawahi kukaa sekta hii huwezi elewa.kingine mimi afya ndo ndoto yangu kwingine sitaweza
 
Ukikosa mchongo kwenye hiyo diploma ya meno utaenda kusomea nini tena?
Siwezi kukosa mchongo Meno inahitajika sana na kwakua nina lengo la kujiajiri nitatumia C.O na Dental kufanya makubwa kwa wakati mmoja.
 
Write your reply...mafanikio hayatokani kozi bali mindset yako,tumie CA kuvumbua kipato chako nje ya kuajiriwa,ulishawah kujiuliza siku rafki yako huyo centre aliyoajiriwa ikipata vichwa vichache zaidi atandelea kupata 900
Ni kweli ila nitakua na fani mbili zote zitanipush kua na mafanikio.
 
Muhimbili Wanatoa Dental laboratory technologist

Ukiwa free ulizia Bei ya dental implants na teeth braces kwa Bei ya hapa Nyumbani tuuu

Kisha uwe huru kuidogosha fani ya Afya ya kinywa na meno
Ushauri wako nimependa ngoja nije Pm unipe nondo mkuu.
 
Daktari nipe ushauri ndugu yangu nategemea ushauri bora kutoka kwako.
Shule ya msingi nilikuwa mwanafunzi pekee niliyechaguliwa kwenda kusoma shule ya Bweni ya wavulana nje ya mkoa wangu.

Wengi niliowaacha hasa wale ambao hawakufaulu kabisa, sasa wapo imara kimaendeleo wameshajenga misingi ya kiuchumi.

Mimi mwenye shahada moja sikuhoi mbele yao kiuchumi, nipo mdogo kama kidoge cha Piriton.

Niko early 30 ila najiona sina nyuma wala mbele.

NASIMAMA NA DOGO WA MTWARA
 
Back
Top Bottom