Ndugu marafiki naombeni ushauri wenu nina uhusiano na msichana kwa muda wa miaka 2 hivi karibuni amenisumbua sana kwani muda mwingi nampigia simu na hapokei pia baada ya kumpigia tena anakuwa hanipi sababu za msingi kutopokea zaidi ya kusema nilikuwa mbali na simu na hata nikimwuliza kwanini hukunitafuta baada ya kukuta missed calls zangu anadai hajaziona leo aliacha simu nyumbani kwao na kwenda sabasaba kumwuliza anadai aliiacha kuhofia kuibiwa,ki ukweli nahisi kuibiwa na kupoteza muda wangu.Pia ni mbishi hata kuniomba msamaha huwa hataki kifupi nimemvumilia sana na habadiliki.