Nafasi za kazi 16/07/2014

Nafasi za kazi 16/07/2014

nimeona nitoe ufafanuzi kidogo, kwanza hili ni kanisa na linafanya kazi na shirika la kikristo hivyo kila shirika lina mission na dira. sasa hivi tukiajiri mtu asie mkristo atawezaje kusimamia maono na utume wa huduma. kama tungekua na ubaguzi basi tungeishia kutangaza kanisani tu lakini tangazo limetangazwa kuanzia kanisani na pia tumeona tuwatangazie na watanzania popote wenye vigezo wajaribu bahati yao. kama una vigezo bila shaka hauwezi kulalamika. kumbuka hii ni kazi ambayo ndani yake ni huduma ya kumtumikia Mungu kwa njia ya watoto maskini na kwa muktadha wa kazi na majukumu inakubidi uwe ni mtu wa kudumu wa mahali hapo . sasa nakushauri kuliko kuwapotosha watu kama haujakidhi vigezo ni heri kuwaachia wenzako watafakari na kuomba kazi. kila kazi ina sifa na vigezo vinavyohitajika . kwahiyo hakuna kosa lolote lililofanyika kwa kutangaza nafasi hii humu. na si lazima kila jambo likufurahishe ndio lionekane jema kwa kila mtu. nawatakia kazi njema

usitake kupotosha watu hapa lengo ni kuwabadilisha dini vijana wote mtakaowachukua kuwalea ambao si dini yenu sasa mkimuweka mtu ambaye si wa dini yenu atafichua mnayoyafanya
 
vigezo vyote ninavyo naa mpaka vya ziada maana mimi kanisani kwangu nina nafasi ya uongozi, sasa kuhama mpaka kanisa jamani, huduma hiyo ni ya kiroho na roho wetu yupo kila mahali, kikubwa ni kumsikiliza na kufanya yale yaliyo mema. hakika sitaweza kutoka K.K.K.T wakati Mungu ni mmoja.
 
eti unatoa ufafanuzi kuwa tangazo c lakibaguzi...una hata aibu....nashukuru wametokea wakristo wamekuchalenji kidogo tu unaweweseka.....SOCIAL WORKER na kuokoka au ushuhuda wapi na wapi????kusimamia watoto c lazima uwe mkristo....huu ni ubaguzi tena wa wazi acha mara moja.....angekuwa anatakiwa padri au askofu au sister watu wasingelalamika coz tunajua ni mambo ya ukristo..lakini SOCIAL WORKER.....teh teh teh....umechemka hiyo ni taaluma ya kijamii hivyo haisomwi na wakristo pekee....umechemka MKANKULE uspende kuweka matangazo ya kibaguzi.......katika mambo/kazi za kitaaluma...napiittaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
usitake kupotosha watu hapa lengo ni kuwabadilisha dini vijana wote mtakaowachukua kuwalea ambao si dini yenu sasa mkimuweka mtu ambaye si wa dini yenu atafichua mnayoyafanya

sasa akibadilishwa dini kutoka upagani inakuuma nini
 
We nawe!
Sasa unadhani angetangaziwa shehe angefanya hii kazi kanisani?
Kuna vitu vingine bibie tuviache tu kama vilivyo!
Imagine kahtaan ama FaizaFoxy anapewa hii kazi, lazima kutakuwa na mkanganyiko tuu!


Kuna vitu vingine inabidi tuviache tu kama vilivyoo! Enh!
hahahahaaaaa..mfumo kristo kama kawa
 
Last edited by a moderator:
Bado naamini kabisa kwamba kati ya wale watu elfu 10 walioitwa uhamiaji, unemployed walikuwa ni kama elfu 5 tu!
Wengineo walikuwa mamluki!

Kwa mfano!....hapa!
vigezo vyote ninavyo naa mpaka vya ziada maana mimi kanisani kwangu nina nafasi ya uongozi, sasa kuhama mpaka kanisa jamani, huduma hiyo ni ya kiroho na roho wetu yupo kila mahali, kikubwa ni kumsikiliza na kufanya yale yaliyo mema. hakika sitaweza kutoka K.K.K.T wakati Mungu ni mmoja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom