Nafasi za kazi 16/07/2014

Nafasi za kazi 16/07/2014

Kanisa la Eagt mtoni kwa kushirikiana na shirika la Compassion International Tanzania linatangaza nafasi za kazi katika kituo cha kuwahudumia watoto wenye mazingira magumu.

Mkataba wa ajira: miaka mitatu mitatu

Mahali pa kazi.: Dar es salaam

Deadline: 25/07/2014

1.Project Director .nafasi 1

Sifa za mwombaji:
- Awe mkristo aliyeokoka na mwenye maisha ya ushuhuda katika mwenendo wake wa kila siku.
-Akubali kuhamia na kusali kanisa la Eagt Mtoni
-shahada ya kwanza kutoka chuo kinachotambulika na serikali katika maeneo ya uongozi /utawala,usimamizi wa miradi,usimamizi wa biashara, maendeleo ya jamii,maendeleo ya watoto,theolojia,na ualimu.
-Uwezo wa kutumika katika jamii maskini iliyo katika mazingira hatarishi,
-Awe na elimu na uwezo wa kutumia compyuta
-Umri 25-40
-Awe na moyo wa kupenda watoto na kutumika mazingira ya kanisani

2.SOCIAl WORKER:nafasi 1

Sifa za mwombaji

- Aliyeokoka mwenyenye maisha ya ushuhuda katika mwenendo wa kila siku.
-Akubali kusali na kuhamia Eagt mtoni
-Elimu , kuanzia stashahada ya maendeleo ya jamii, watoto, ualimu,kozi yoyote inayoendana na hizo kutoka katika chuo kinachotambulika na serikali.
-mwenye moyo wa kufanya kazi kanisani na kuwatumikia watoto
-uwezo wa kutumia compyuta
-umri 25-40

NAMNA YA KUTUMA MAOMBI

Maombi yote yaambatanishwe na barua ya mchungaji wako ikiwa na mawasiliano yake ya simu yenye kueleza uhai wako kiroho kama mshirika .
-Barua ya kuomba kazi na nakala za vyeti kwa anuani ifuatayo

Mchungaji Kiongozi
Mtoni Eagt Church
P.o.box 46249
Temeke
Dar es salaam

Email: tz-678@icptz.org au chisoropm@hotmail.com

kwa mafafanuzi zaidi piga simu :0756 390 857,0657 552 902
tunashukuru
 
sasa kama ndo ivyo si bora hizi kazi mngezitangaza kanisani kwenu? yann kutaka mtu aamie kwenye kanisa lako??
 
duh kusali mtoni hpo ndiyo pamekaa vibaya binafsi sintoweza

Usiogope ndugu. Mtoni (kwa muktadha wa hilo tangazo) ni eneo, sio sehemu ya maji. Ni kama vile ilivyo Forodhani, Mtendeni, Mkunazini, Mianzini nk. Ni jina la eneo tu. Omba hiyo kazi
 
Njia rahis ilikua kutangaza Kazi hiyo makanisani kwenu maana kwa hapa inaonyesha jinsi gani udin upo kwenye maeneo ya Kazi na kwa hapo ni rahisi kumpata MTU mwenye vigezo hivyo lakini atakua feki. Vigezo vyote mnavyohitaji ni sawa lakin hapo kwenye dini!
 
nimeona nitoe ufafanuzi kidogo, kwanza hili ni kanisa na linafanya kazi na shirika la kikristo hivyo kila shirika lina mission na dira. sasa hivi tukiajiri mtu asie mkristo atawezaje kusimamia maono na utume wa huduma. kama tungekua na ubaguzi basi tungeishia kutangaza kanisani tu lakini tangazo limetangazwa kuanzia kanisani na pia tumeona tuwatangazie na watanzania popote wenye vigezo wajaribu bahati yao. kama una vigezo bila shaka hauwezi kulalamika. kumbuka hii ni kazi ambayo ndani yake ni huduma ya kumtumikia Mungu kwa njia ya watoto maskini na kwa muktadha wa kazi na majukumu inakubidi uwe ni mtu wa kudumu wa mahali hapo . sasa nakushauri kuliko kuwapotosha watu kama haujakidhi vigezo ni heri kuwaachia wenzako watafakari na kuomba kazi. kila kazi ina sifa na vigezo vinavyohitajika . kwahiyo hakuna kosa lolote lililofanyika kwa kutangaza nafasi hii humu. na si lazima kila jambo likufurahishe ndio lionekane jema kwa kila mtu. nawatakia kazi njema
 
nimeona nitoe ufafanuzi
kidogo, kwanza hili ni kanisa na linafanya kazi na shirika la kikristo
hivyo kila shirika lina mission na dira. sasa hivi tukiajiri mtu asie
mkristo atawezaje kusimamia maono na utume wa huduma. kama tungekua na
ubaguzi basi tungeishia kutangaza kanisani tu lakini tangazo
limetangazwa kuanzia kanisani na pia tumeona tuwatangazie na watanzania
popote wenye vigezo wajaribu bahati yao. kama una vigezo bila shaka
hauwezi kulalamika. kumbuka hii ni kazi ambayo ndani yake ni huduma ya
kumtumikia Mungu kwa njia ya watoto maskini na kwa muktadha wa kazi na
majukumu inakubidi uwe ni mtu wa kudumu wa mahali hapo . sasa nakushauri
kuliko kuwapotosha watu kama haujakidhi vigezo ni heri kuwaachia
wenzako watafakari na kuomba kazi. kila kazi ina sifa na vigezo
vinavyohitajika . kwahiyo hakuna kosa lolote lililofanyika kwa
kutangaza nafasi hii humu. na si lazima kila jambo likufurahishe ndio
lionekane jema kwa kila mtu. nawatakia kazi njema

na sisi ambao ni wakatoliki na walutherani si ni wakristo???........tunaweza pata hiyo kazi??....maana sio kila mkristo ameokoka........japo mnataka wakristo....na nikituma application zangu na nna vigezo ila sina barua kutoka kwa mchungaji inakuwaje???
 
zingatia vigezo .kukosekana kwa kigezo kimoja ni sababu ya kutokuchaguliwa. iwapo upo serious jitathmin mwenyewe ukiona una sifa zote fanyia kazi tangazo.
 
zingatia vigezo .kukosekana kwa kigezo kimoja ni sababu ya kutokuchaguliwa. iwapo upo serious jitathmin mwenyewe ukiona una sifa zote fanyia kazi tangazo.

Vip nikiambatanisha barua ya padri coz me ni mromani!
 
MKANKULE. Hembu fafanua hilo la kuhama kanisa maana tatizo liko hapo naweza nikawa mkristo niliyeokoka na vigezo vyote Lakini nikasali kanisani kwangu? Kote Mungu ni mmoja .
 
zingatia tangazo na maelezo yaliyotangulia .labda kama unahitaji mafafanuz piga simu kwa mawasiliano niliyoweka hapo kwenye tangazo.
 
walokole bwana !! sasa madhehebu yote yakifanya hvyo itakuwaje.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom