Nafanya kama sijali ila moyoni naumia!

Nafanya kama sijali ila moyoni naumia!

Hady

Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
19
Reaction score
4
Jamani naombeni msaada, hivi mtu kama huyu nyie mnamchukuliaje? tulikuwa ndo tumeanza tu kuongea kwa njia ya simu mimi na mpenzi wangu ambae nkonae mbali, hata dakika tano hazikuisha akanambia "kata simu kuna mtu anapiga" hapo akatumia zaidi ya lisaa kuongea anadai ni kaka yake,mi nkaamua kumpotezea, kiukweli ameniboa na nimeamua kuzima simu kabisa au nimekosea?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mhhhh! Pole sana. Mpe nafasi kama naye ana hamu ya kuongea nawe akutafute. Ukiona kimya basi ujue kwamba moyoni mwake haupo kabisa.

Jamani naombeni msaada, hivi mtu kama huyu nyie mnamchukuliaje? tulikuwa ndo tumeanza tu kuongea kwa njia ya simu mimi na mpenzi wangu ambae nkonae mbali, hata dakika tano hazikuisha akanambia "kata simu kuna mtu anapiga" hapo akatumia zaidi ya lisaa kuongea anadai ni kaka yake,mi nkaamua kumpotezea, kiukweli ameniboa na nimeamua kuzima simu kabisa au nimekosea?
 
Asante Bak kwa ushauri, ngoja niiwashe nione kama kunachochote.
 
Bado sijaelewa mkuu . Je hili limetokea leo tu au ndio mchezo wake. Nahisi kama ume-over react ...................
 
Hili limetokea leo tu ila tangu amekuwa mbali na mimi nahisi kama amebadilika coz ninaweza piga simu isipatikane au isipokelewe nkimuuliza anadai imekufa betri wakati haikuwa na shida kama hiyo before, yaani kifupi ni kwamba amekuwa muda mwingi hayupo hewani.
 
Simu nimeiwasha now, na ametuma text kuwa "Beb stop that,sleep tit". Ila mwenzenu hata simuelewi.
 
mh! mnanishauri nifanye nini? maana naogopa kuendelea kupata maumivu zaidi.
 
Hili limetokea leo tu ila tangu amekuwa mbali na mimi nahisi kama amebadilika coz ninaweza piga simu isipatikane au isipokelewe nkimuuliza anadai imekufa betri wakati haikuwa na shida kama hiyo before, yaani kifupi ni kwamba amekuwa muda mwingi hayupo hewani.
Mapenzi yana kazi pole sana vumilia dear. Piga moyo konde manake mapenzi ya mbali yanaumiza sana lkn sioni tatizo kwani hakuna jambo kubwa ni huo umbali tu ambao naamini utaisha muda wake ukifika.
 
Hili limetokea leo tu ila tangu amekuwa mbali na mimi nahisi kama amebadilika coz ninaweza piga simu isipatikane au isipokelewe nkimuuliza anadai imekufa betri wakati haikuwa na shida kama hiyo before, yaani kifupi ni kwamba amekuwa muda mwingi hayupo hewani.

Acha kulalamika mnunulie betri ya simu utakua ume-solve tatizo.
 
Mapenzi ya mbali yanasumbua sana, kweli unawezakuta network inasumbua akawa hapatikani sasa ukawaza anazima cm makusudi. hivyo basi jaribu kumpigia cm ongea nae taratibu mwambie jinsi unavyokwazika na hiyo tabia then uone yeye atareply vipi.
 
chezea mapenzi ya mbali unaweza waza hivi au vile ukawa tofauti na mawazo ya mwenzio kuwa mvumilivu one day yataisha
 
TRUST ME, THERE IS ONLY 5% FOR LONG DISTANCE TO WORK, 95% LONG DISTANCE DOESN'T WORK AND BELIEVE ME WHEN I SAY THERE IS 95% THAT SHE FOUND ANOTHER GUY.......... wanawake hawatabiliki, don't trust too much
 
.... Ivi kile chuo cha mapenzi kiko wapi???? vijana wanaangamia kwa kukosa maarifa..

anyway.. unapaswa kufahamu kwamba mapenzi ya kileo yanahitaji uwezo na akili binafsi kuyamudu.. Mabinti wa sasa si wa kale..
 
Jamani naombeni msaada, hivi mtu kama huyu nyie mnamchukuliaje? tulikuwa ndo tumeanza tu kuongea kwa njia ya simu mimi na mpenzi wangu ambae nkonae mbali, hata dakika tano hazikuisha akanambia "kata simu kuna mtu anapiga" hapo akatumia zaidi ya lisaa kuongea anadai ni kaka yake,mi nkaamua kumpotezea, kiukweli ameniboa na nimeamua kuzima simu kabisa au nimekosea?

Kitu kikubwa kinachowaunganisha wapendanao ni mawasiliano. Ukiona kuna magumashi kwenye mawasiliano ujue there must be something wrong somewhere. Watu wanaopendana kwa dhati iwe wako mbali au la, always huwa unatamani kuwasiliana na mpenzi wako. Toka lini kaka akawa wa muhimu zaidi ya MPENZI? Huyo bado hajapenda. Usichukulie jazba anza kulifanyia kazi kuna kitu utagundua.
 
Pole sana mkuu, kama ni mara ya kwanza vumilia uone kama hali hiyo itaendelea, usichukue maamuzi magumu ambayo yatakuathiri na wewe pia.
 
hivi nyie muambiwe mara ngapi ndio mtaelewa kuwa long distance relationship ni uzushi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom