tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,854
- 1,139
Mtu na mkewe wanagombana chumbani, ghafla ugomvi unakuwa mkubwa mke anaamua kukusanya vitu vyake kwa lengo la kuondoka. Mume anashangaa anamuulizaa: Unakusanya vitu unaenda wapi? Mke kwa nyodo anajibu: Nakwenda kwa mama yangu. Mume naye akaanza kukusanya nguo zake na kuweka kwenye mabegi yake, mke kwa jeuri akamuuliza mume wake: Unapaki unakwenda wapi? Mume akajibu kwa tabasamu: na mimi nakwenda kwa mama yangu. Mke akauliza tena "Hawa watoto wako watabaki na nani:Mume kwa kujiamini akajibu Nao waende kwa mama yao kama sisi tunavyokwenda
kwa mama zetu.
kwa mama zetu.