Nadhani nimesahau kukasirika

Nadhani nimesahau kukasirika

mtoto mdogo sana

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2020
Posts
476
Reaction score
1,446
Habari wana jamvi.

Bila shaka hamjambo, mimi pia sijambo.

Bila longolongo nyingi, naenda kwenye mada.

Nadhani mimi ni kati ya watu waliowahi kupata maswaibu makubwa kwenye maisha na hii nadhani imepelekea kujenga usugu wa hali ya juu. Na wakati fulani hata mimi nilikuwa sijiamini, yaani najitilia mashaka mwenyewe.

Kuna muda nilikuwa nikifikiri hivi je nafaa kuaminiwa? Au je ni salama mimi kupewq dhamana ya jambo? Ila mwisho wa siku nikaanza kujifunza kuishi na watu mwisho nikaweza.

Anyway nisitoke nje ya mada. Zamani utotoni nilikuwa ni mtoto mtukutu mwenye hasira za kuua, hali iliyonipelekea kutopata hata marafiki wa kucheza nao. Nilikuwa siwezi kabisa kuvumilia kuudhiwa. Nilikuwa napigana mpaka ninayepigana nae ashindwe kurudisha.
Ilikuwa nikishiriki mchezo wa mpira wa miguu, basi akijichanganya mtu akanichezea vibaya 'rafu' basi keaho lazima atatembelea magongo na POP nyingi.

Nadhani kwa sababu sikuwa na uangalizi wowote na nilikuwa sina ninayemuogopa. Ilikuwa hata mwalimu akinizingua, basi namlia 'timing' anakula virungu na kesho yake atatembelea magongo

Ilifika wakati nikawa naogopwa hata na watu wazima. Nishapigwa lockup mara nyingi sana utotoni. Sema sio lockup ile nilikuwa nafungiwa kwenye ofisi ya mtendaji wa kata. Mpaka siku tatu. Kwa kuwa sikuwa na mtu wa kuniletea chakula basi wananichimba mkwara wananiachilia.

Shule nilikuwa na akili kupita kiasi, yaani nilikuwa mpaka naboa, kuna darasa moja nilirushwa (hii sio stori ya leo) basi nilikuwa nashauriwa sana, ila nikikasirika, basi ushauri woote nausahau. Ni vita tu.

Ilikuwa sio inshu kubwa mimi kumpiga mtu tofali, wala nilikuwa sina ile hali ya kusita. Sijui kama mnanielewa ila nilikuwa mnyama hasa.

Nikawa sipati wa kucheza nae mpira wa miguu, sipati watoto wa kwenda nao kucheza michezo ya kitoto n.k.
Basi nachokumbuka nilijikuta mimi ni jasiri kupita maelezo, naenda mapori makubwa narudi na sungura, kware, mayai mbalimbali, na sometime niliwahi kurudi na nungunungu peke yangu.

Akinizingua tu mtu, nakiwasha.. basi nikatengwa mazima na watu wa rika langu. Nilioweza kuongea nao ni wazee sana kwnye vijiwe vya kucheza bao, pamoja na askari polisi. Hao ndio nilikuwa siingii nao vita. Anywai nikatokea kuwa mtoto mdogo mwenye uwezo mkubwa sana wa kucheza bao (mpaka leo)

Basi tu cut the story short, niliqnza kujifunza kucontrol hasira zangu, kwa kipindi kirefu zaidi nikajimudu kuzuia hasira mpaka nikaweza kuendelea na masomo, nikahitimu masomo, mpaka nikawa zezeta kabisa nikawa siwezi kuhoji hata napokashfiwa, ninapptukanwa sijibu chochote. Unaambiwa mpaka leo kuna wakati nadhulumiwa haki ila natabasamu tu na maisha yanaendelea.

Nimeanza kushtuka siku hizi naona sasa watu wananipanda sanankichwani kwa kuwa wanajua sina madhara kabisa, wananidhulumu, wanatukana, wanasingizia, wanafanya chochote ilimradi wanaamini mimi ni 'zombitype'.

Kimsingi, hata nikisingiziwa jambo huwa siwezi kujitetea kabisa. Najikuta tu nanyamaza namsikiliza mtu na madai yake na hatimaye hukumu yake. Najikuta jibu la haraka nilonalo ni OKAY, au wakati mwingine kufuata maelekezo bila kuhoji zaidi.

Hali hii ya kuzuia hasira kwa muda mrefu, imenipelekea kupata mdonda ya tumbo kwa kuwa pamoja na kutolitoa fukuto la hasira

Anyway, nitaimalizia stori baadae. Ngoja kwanza nile
 
Habari wana jamvi.

Bila shaka hamjambo, mimi pia sijambo.

Bila longolongo nyingi, naenda kwenye mada.

Nadhani mimi ni kati ya watu waliowahi kupata maswaibu makubwa kwenye maisha na hii nadhani imepelekea kujenga usugu wa hali ya juu. Na wakati fulani hata mimi nilikuwa sijiamini, yaani najitilia mashaka mwenyewe.

Kuna muda nilikuwa nikifikiri hivi je nafaa kuaminiwa? Au je ni salama mimi kupewq dhamana ya jambo? Ila mwisho wa siku nikaanza kujifunza kuishi na watu mwisho nikaweza.

Anyway nisitoke nje ya mada. Zamani utotoni nilikuwa ni mtoto mtukutu mwenye hasira za kuua, hali iliyonipelekea kutopata hata marafiki wa kucheza nao. Nilikuwa siwezi kabisa kuvumilia kuudhiwa. Nilikuwa napigana mpaka ninayepigana nae ashindwe kurudisha.
Ilikuwa nikishiriki mchezo wa mpira wa miguu, basi akijichanganya mtu akanichezea vibaya 'rafu' basi keaho lazima atatembelea magongo na POP nyingi.

Nadhani kwa sababu sikuwa na uangalizi wowote na nilikuwa sina ninayemuogopa. Ilikuwa hata mwalimu akinizingua, basi namlia 'timing' anakula virungu na kesho yake atatembelea magongo

Ilifika wakati nikawa naogopwa hata na watu wazima. Nishapigwa lockup mara nyingi sana utotoni. Sema sio lockup ile nilikuwa nafungiwa kwenye ofisi ya mtendaji wa kata. Mpaka siku tatu. Kwa kuwa sikuwa na mtu wa kuniletea chakula basi wananichimba mkwara wananiachilia.

Shule nilikuwa na akili kupita kiasi, yaani nilikuwa mpaka naboa, kuna darasa moja nilirushwa (hii sio stori ya leo) basi nilikuwa nashauriwa sana, ila nikikasirika, basi ushauri woote nausahau. Ni vita tu.

Ilikuwa sio inshu kubwa mimi kumpiga mtu tofali, wala nilikuwa sina ile hali ya kusita. Sijui kama mnanielewa ila nilikuwa mnyama hasa.

Nikawa sipati wa kucheza nae mpira wa miguu, sipati watoto wa kwenda nao kucheza michezo ya kitoto n.k.
Basi nachokumbuka nilijikuta mimi ni jasiri kupita maelezo, naenda mapori makubwa narudi na sungura, kware, mayai mbalimbali, na sometime niliwahi kurudi na nungunungu peke yangu.

Akinizingua tu mtu, nakiwasha.. basi nikatengwa mazima na watu wa rika langu. Nilioweza kuongea nao ni wazee sana kwnye vijiwe vya kucheza bao, pamoja na askari polisi. Hao ndio nilikuwa siingii nao vita. Anywai nikatokea kuwa mtoto mdogo mwenye uwezo mkubwa sana wa kucheza bao (mpaka leo)

Basi tu cut the story short, niliqnza kujifunza kucontrol hasira zangu, kwa kipindi kirefu zaidi nikajimudu kuzuia hasira mpaka nikaweza kuendelea na masomo, nikahitimu masomo, mpaka nikawa zezeta kabisa nikawa siwezi kuhoji hata napokashfiwa, ninapptukanwa sijibu chochote. Unaambiwa mpaka leo kuna wakati nadhulumiwa haki ila natabasamu tu na maisha yanaendelea.

Nimeanza kushtuka siku hizi naona sasa watu wananipanda sanankichwani kwa kuwa wanajua sina madhara kabisa, wananidhulumu, wanatukana, wanasingizia, wanafanya chochote ilimradi wanaamini mimi ni 'zombitype'.

Kimsingi, hata nikisingiziwa jambo huwa siwezi kujitetea kabisa. Najikuta tu nanyamaza namsikiliza mtu na madai yake na hatimaye hukumu yake. Najikuta jibu la haraka nilonalo ni OKAY, au wakati mwingine kufuata maelekezo bila kuhoji zaidi.

Hali hii ya kuzuia hasira kwa muda mrefu, imenipelekea kupata mdonda ya tumbo kwa kuwa pamoja na kutolitoa fukuto la hasira

Anyway, nitaimalizia stori baadae. Ngoja kwanza nile
Kama umefanikisha kusahau kukasirika, basi usiyaweke mawazoni mwako mpaka yanaathiri afya.
 
Ngoja nimalizie stori

Shule ya msingi niliyosoma alikuja mwalim mpya, huyu alijaribu kuongea na mimi akitumia njia tofauti. Nadhani aligundua kipengele cha upweke wangu neio akakaza hapo. Aisee alikuwa akinipa muongozo ambao umenikenga mpaka leo. Yule jamaa mpaka leo namkumbuka sana.

Nikaanza kujiweka mbali na vitu vinavyonikasirisha, mwanzo ilikuwa ngumu. Alinielekeza kunyamaza kimya na kuhesabu kimya kimya mpaka 20 kabla ya kumjibu mtu yeyote. Nikaanza kuwa 'neo zezeta' wakati mwingine nikipata ghadhabu wakati nikihesabu kimoyomoyo najikuta napiga mguu chini kwa nguvu, au na-crush nilichokishika, wakati mwingine napiga ngumi ukuta yaani ilimradi tu hasira zipungue bila kumdhuru mtu.

Miaka hiyo kulikuwa na zile kalam za wino za kuandikia zinaitwa BIC, basi hizo zimeshanichanachana sana mikono zile glass zake nikizivunjia mkononi au mfukoni. Sema Mungu mkubwa makovu madogo kwenye viganja vya mikono huwa yanafutika na kupokea kabisa.

Kucontrol hasira kulianza kuniweka karibu na baadhi ya watu ambao wamepelekea mpaka leo nimemaliza chuo kikuu, namshukuru Mungu kwani sijui kama primary yenyewe ningeimaliza.

Nachoshukuru kingine ni kuwa, pamoja na kiburi na hasira zile ila nilikuwa siibi cha mtu. Watu walikuwa wananitegea nikiiba wanipige waniue (nilikuwa naboa) lakini haikutokea, hiyo ikawa ndio pona yangu.

Kati ya mwezi August na September mwaka jana nilienda kijijini nilipokulia, niliwaona watu baadhi wanaotembea kwa kuchechemea kwa ajili ya kilema nilichowatia, niliona mtu mwenye kovu kubwa kichani, nikakumbuka it was all my doing, kuna mtu mwingine nilikutana nae mkono wa kulia umepinda nikamkumbuka, nilimvuja mkono sehem mbili, wazazi wake hawakumpeleka hosp, wakamtibu kienyeji. Sipendi kuielezea hii.

Napapenda kijijini kule na watu hunichukulia kama mfano unaoishi, uthibitieho wa muujiza ila ile guilty inaninyonga mno.

Sasa hivi nina theory naiita 'tinting' yaani kumpuuza mtu anayenitafuta ugomvi. Sasa hii inanifanya nazidi kudharaulika. Nashindwa kujitetea, nahesabu kila neno nalozungumza nikianzisha mazungumzo na watu. Siku za karibuni nimeanzisha ucheshi na utani kwa watu wachache niliobahatika kuwazoea, ila naona I am not good at it. Najiona kama naigiza maisha. Wakati mwingine najishtukia mwenyewe.

Pamoja na kuwa nina uwezo mkubwa wa kusoma saikolojia ya mtu, lakini nashindwa yani kuendana na energy ya kila mtu. Mtu akiniona negative, nafunga 'tinted' sasa inanipa shida. Kwa sababu ya kutozoea kuishi kijamii sana, kauli zangu huwa zimekaa kimaamizi sana. Watu hawapendi hiyo, wanaamini katika majadiliano. Sasa mpaka nakosa niganyaje.

Kipengere muhimu sasa, hata kwenye mahusiano hali hii inaniathiri. Ni afadhali ningekuwa nakasirika nafoka yanaisha. Ila siwezi. Yaani nikiudhiwa, nafunga vioo 'kufunga ubalozi' nabaki natafakari suala kimoyomoyo mpaka nafikia maamuzi bila kujadiliana. Huwa nawaepuka wapenz naokuwa nao, nakata mawasiliano kuepuka ugomvi, nakaa kimya, na wakati mwingine hata kuziacha kabisa namba zangu za simu.

Nilishawahi kumkimbia mpenzi wangu geto nilikopanga baada ya kunizingua, nilikaa kitaa muda mrefu bila kumrudia, akanitafuta sana tusuluhishe, akaharibu akanitafuta kupitia mtu pekee anayenifahamu, na akatumia approach mbaya akazidi kuharibu. Na hadithi yetu iliishia happ.

Suala linaloniharibu zaidi ni lawama. Aisee lawama huwa zinanitafuna mno. Na zimenikosanisha na watu wengi mno. Nimefunga ubalozi na watu lukuki kisa nimelaumiwa. Kipengere ni kuwa mimi siwez kujitetea kukanusha madai. Siwezi kumshawishi mtu aamini kinyume na alivyodhania.

Mimi huishi nikijua, siibi, siui, sio mnafiki niko 'fea' na 'ofkoz' sina shida na mtu. Ila ikitokea ukanichukulia tofauti na nilivo basi nakukata lisehem chako kwenye maisha yangu.

Najitahidi nirudishe hasira kidogo ili nipate reaction ya kawaida niishi na watu vizuri nashindwa.

Ndugu zangu, natamani sana kukasirika tena. Nina madonda ya tumbo sugu kwa ajili ya kunyamaza mambo yangu kwa muda mrefu, nakaa na maudhi siku zote bila kumlaum mtu wala kujadiliana nae. Nateseka mno.

Sijui kama mnanielewa, ila napitia wakati mgumu sana.

Anyway. Niwatakoe majukumu mema.
 
Ngoja nimalizie stori

Shule ya msingi niliyosoma alikuja mwalim mpya, huyu alijaribu kuongea na mimi akitumia njia tofauti. Nadhani aligundua kipengele cha upweke wangu neio akakaza hapo. Aisee alikuwa akinipa muongozo ambao umenikenga mpaka leo. Yule jamaa mpaka leo namkumbuka sana.

Nikaanza kujiweka mbali na vitu vinavyonikasirisha, mwanzo ilikuwa ngumu. Alinielekeza kunyamaza kimya na kuhesabu kimya kimya mpaka 20 kabla ya kumjibu mtu yeyote. Nikaanza kuwa 'neo zezeta' wakati mwingine nikipata ghadhabu wakati nikihesabu kimoyomoyo najikuta napiga mguu chini kwa nguvu, au na-crush nilichokishika, wakati mwingine napiga ngumi ukuta yaani ilimradi tu hasira zipungue bila kumdhuru mtu.

Miaka hiyo kulikuwa na zile kalam za wino za kuandikia zinaitwa BIC, basi hizo zimeshanichanachana sana mikono zile glass zake nikizivunjia mkononi au mfukoni. Sema Mungu mkubwa makovu madogo kwenye viganja vya mikono huwa yanafutika na kupokea kabisa.

Kucontrol hasira kulianza kuniweka karibu na baadhi ya watu ambao wamepelekea mpaka leo nimemaliza chuo kikuu, namshukuru Mungu kwani sijui kama primary yenyewe ningeimaliza.

Nachoshukuru kingine ni kuwa, pamoja na kiburi na hasira zile ila nilikuwa siibi cha mtu. Watu walikuwa wananitegea nikiiba wanipige waniue (nilikuwa naboa) lakini haikutokea, hiyo ikawa ndio pona yangu.

Kati ya mwezi August na September mwaka jana nilienda kijijini nilipokulia, niliwaona watu baadhi wanaotembea kwa kuchechemea kwa ajili ya kilema nilichowatia, niliona mtu mwenye kovu kubwa kichani, nikakumbuka it was all my doing, kuna mtu mwingine nilikutana nae mkono wa kulia umepinda nikamkumbuka, nilimvuja mkono sehem mbili, wazazi wake hawakumpeleka hosp, wakamtibu kienyeji. Sipendi kuielezea hii.

Napapenda kijijini kule na watu hunichukulia kama mfano unaoishi, uthibitieho wa muujiza ila ile guilty inaninyonga mno.

Sasa hivi nina theory naiita 'tinting' yaani kumpuuza mtu anayenitafuta ugomvi. Sasa hii inanifanya nazidi kudharaulika. Nashindwa kujitetea, nahesabu kila neno nalozungumza nikianzisha mazungumzo na watu. Siku za karibuni nimeanzisha ucheshi na utani kwa watu wachache niliobahatika kuwazoea, ila naona I am not good at it. Najiona kama naigiza maisha. Wakati mwingine najishtukia mwenyewe.

Pamoja na kuwa nina uwezo mkubwa wa kusoma saikolojia ya mtu, lakini nashindwa yani kuendana na energy ya kila mtu. Mtu akiniona negative, nafunga 'tinted' sasa inanipa shida. Kwa sababu ya kutozoea kuishi kijamii sana, kauli zangu huwa zimekaa kimaamizi sana. Watu hawapendi hiyo, wanaamini katika majadiliano. Sasa mpaka nakosa niganyaje.

Kipengere muhimu sasa, hata kwenye mahusiano hali hii inaniathiri. Ni afadhali ningekuwa nakasirika nafoka yanaisha. Ila siwezi. Yaani nikiudhiwa, nafunga vioo 'kufunga ubalozi' nabaki natafakari suala kimoyomoyo mpaka nafikia maamuzi bila kujadiliana. Huwa nawaepuka wapenz naokuwa nao, nakata mawasiliano kuepuka ugomvi, nakaa kimya, na wakati mwingine hata kuziacha kabisa namba zangu za simu.

Nilishawahi kumkimbia mpenzi wangu geto nilikopanga baada ya kunizingua, nilikaa kitaa muda mrefu bila kumrudia, akanitafuta sana tusuluhishe, akaharibu akanitafuta kupitia mtu pekee anayenifahamu, na akatumia approach mbaya akazidi kuharibu. Na hadithi yetu iliishia happ.

Suala linaloniharibu zaidi ni lawama. Aisee lawama huwa zinanitafuna mno. Na zimenikosanisha na watu wengi mno. Nimefunga ubalozi na watu lukuki kisa nimelaumiwa. Kipengere ni kuwa mimi siwez kujitetea kukanusha madai. Siwezi kumshawishi mtu aamini kinyume na alivyodhania.

Mimi huishi nikijua, siibi, siui, sio mnafiki niko 'fea' na 'ofkoz' sina shida na mtu. Ila ikitokea ukanichukulia tofauti na nilivo basi nakukata lisehem chako kwenye maisha yangu.

Najitahidi nirudishe hasira kidogo ili nipate reaction ya kawaida niishi na watu vizuri nashindwa.

Ndugu zangu, natamani sana kukasirika tena. Nina madonda ya tumbo sugu kwa ajili ya kunyamaza mambo yangu kwa muda mrefu, nakaa na maudhi siku zote bila kumlaum mtu wala kujadiliana nae. Nateseka mno.

Sijui kama mnanielewa, ila napitia wakati mgumu sana.

Anyway. Niwatakoe majukumu mema.
Pole sana!
 
Ukiwa mkorofi udogoni mara nyingi ukiwa mkubwa unapoa. And vise verse.

Mie pia nilikuwa mtundu sana, mkali na mjeuri ila sasa nimekuwa zuzu wa zuzuni hasa, nna huruma na sigombani na mtu hata anikere vp
Kweli mambo hubadilika. Mm ndio proof ya ule msemo shetani akizeeka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom