Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Mfalme ameandaa sherehe kubwa ya arusi. Amewaalika watu wote bila upendeleo. Lakini ajabu, wote walioalikwa wamekataa mwaliko!
Huyu anasema: "Samahani, naenda kuzika." Yule anasema: "Lazima niende shambani, nimeanza kupanda mbegu." Mwingine amejibu: "Naomba unielewe, nimeoa hivi majuzi!" Wote wana visingizio!
Wahubiri ni wengi mitaani, masokoni, kwenye redio na TV, na kwenye mitandao. Wanapaza sauti kwamba Yesu yuaja kuwachukua watakaokubali mwaliko wake. Atawachukua waende kula vinono kwenye sherehe hiyo ya arusi!
Nacheka kwa uchungu kwa sababu sauti za wahubiri hao zinajibiwa kwa kejeli:
"Ah, hao wahubiri wamechanganyikiwa kabisa! Wafungwe kamba wapelekwe Mirembe!" "Wamekosa kazi ndiyo maana wanatisha watu na moto wa milele!" "Wanapiga makelele tu, dunia haiishi!"
Magari ya abiria yanasafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine huku yakipiga nyimbo za mwaliko wa arusi. Nacheka kwa uchungu kwa sababu abiria waliomo ndani ya magari hayo hawazitaki nyimbo hizo. Wanamshauri konda aweke movie za mapenzi. Na wengine wameweka headphones masikioni wanasikiliza bongofleva kwenye simu zao, huku wakirushiana picha za aibu TikTok na kugombania mademu Facebook!
Nacheka – si kwa dhihaka, bali kwa uchungu, nikiwaangalia watu wengi wanavyoenda motoni. Wanapita njia pana huku wameinua glasi za pombe wakimnyanyapaa Bwana wa uzima. Nawasikia wakishangilia, lakini punde sauti zao zitageuka kuwa za kilio na kusaga meno.
Nacheka kwa uchungu kwa sababu siku ya hukumu inakuja. Waliozoea kukata rufaa, siku hiyo hakuna nafasi ya kukata rufaa.
Watu watakumbuka zile video walizo-skip YouTube kwa sababu zilikuwa za mahubiri badala ya comedy. Watakumbuka nyuzi alizoandika Setfree waka-comment "ana tatizo la afya ya akili."
Ndugu yangu, usifanye mzaha na wokovu. Furaha yako ya leo isije kuwa kilio cha milele. Tubu leo kwa kuwa ufalme wa Mungu umekaribia. Tubu leo uwe miongoni mwao watakaoshiriki karamu(sherehe) kubwa, isiyo na mfano, aliyoiandaa Bwana Yesu. Ukikubali kuokoka leo, nitacheka kicheko cha furaha. Mungu akubariki.
Huyu anasema: "Samahani, naenda kuzika." Yule anasema: "Lazima niende shambani, nimeanza kupanda mbegu." Mwingine amejibu: "Naomba unielewe, nimeoa hivi majuzi!" Wote wana visingizio!
Wahubiri ni wengi mitaani, masokoni, kwenye redio na TV, na kwenye mitandao. Wanapaza sauti kwamba Yesu yuaja kuwachukua watakaokubali mwaliko wake. Atawachukua waende kula vinono kwenye sherehe hiyo ya arusi!
Nacheka kwa uchungu kwa sababu sauti za wahubiri hao zinajibiwa kwa kejeli:
"Ah, hao wahubiri wamechanganyikiwa kabisa! Wafungwe kamba wapelekwe Mirembe!" "Wamekosa kazi ndiyo maana wanatisha watu na moto wa milele!" "Wanapiga makelele tu, dunia haiishi!"
Magari ya abiria yanasafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine huku yakipiga nyimbo za mwaliko wa arusi. Nacheka kwa uchungu kwa sababu abiria waliomo ndani ya magari hayo hawazitaki nyimbo hizo. Wanamshauri konda aweke movie za mapenzi. Na wengine wameweka headphones masikioni wanasikiliza bongofleva kwenye simu zao, huku wakirushiana picha za aibu TikTok na kugombania mademu Facebook!
Nacheka – si kwa dhihaka, bali kwa uchungu, nikiwaangalia watu wengi wanavyoenda motoni. Wanapita njia pana huku wameinua glasi za pombe wakimnyanyapaa Bwana wa uzima. Nawasikia wakishangilia, lakini punde sauti zao zitageuka kuwa za kilio na kusaga meno.
Nacheka kwa uchungu kwa sababu siku ya hukumu inakuja. Waliozoea kukata rufaa, siku hiyo hakuna nafasi ya kukata rufaa.
Watu watakumbuka zile video walizo-skip YouTube kwa sababu zilikuwa za mahubiri badala ya comedy. Watakumbuka nyuzi alizoandika Setfree waka-comment "ana tatizo la afya ya akili."
Ndugu yangu, usifanye mzaha na wokovu. Furaha yako ya leo isije kuwa kilio cha milele. Tubu leo kwa kuwa ufalme wa Mungu umekaribia. Tubu leo uwe miongoni mwao watakaoshiriki karamu(sherehe) kubwa, isiyo na mfano, aliyoiandaa Bwana Yesu. Ukikubali kuokoka leo, nitacheka kicheko cha furaha. Mungu akubariki.