Nabi na Kaizer Chiefs ngoma bado ngumu

bullar

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
9,161
20,055
Dili la Kocha Nabi Laekekea Kushindwa South Africa, Msimamo Wake Wamponza maskini...Dili la Kocha Nabi Laekekea Kushindwa South Africa, Msimamo Wake Wamponza

Mazungumzo kati ya Kaizer Chiefs na wakala wa Nasreddine Nabi yameripotiwa kufifia huku pande hizo mbili zikijipapatua kutafuta muafaka.

Kocha huyo raia wa Tunisia anasemekana kufanya kazi benchi lake la ufundi aliokuwa akifanya nao kazi katika Klabu ya Yanga ambayo inajumuisha kocha msaidizi, kocha wa makipa, na kocha wa mazoezi ya viungo.

Hata hivyo, uongozi wa Kaizer Chiefs unadaiwa kugoma kufanya mabadiliko makubwa katika benchi lao la ufundi la sasa ambalo linaongozwa na Arthur Zwane.

Taarifa kutoka nchini humo zinaeleza kuwa, mashabiki wengi wa Kaizer wamemtaka Nabi kutokubali masharti ya Glamour Boys, badala yake asimamie msimamo wake kwani iwapo timu inamhitaji kweli basi watakubaliana na matakwa yake.

Kaizer Chiefs walikuwa na mkutano wikendi iliyopita na wenye lengo la kutatua suluhu kuhusu vikwazo vya kocha Nabi.

Taarifa kutoka chombo kimoja cha habari nchini Afrika Kusini, TimesLIVE kimearifiwa kuwa dili hilo bado si la uhakika, na kwamba Amakhosi wamekuwa wakiwasiliana na makocha wengine wa kigeni ambao wanaweza kuchukua nafasi hiyo.

Klabu hiyo ina hamu ya kufanya miadi katika wiki mbili zijazo, kabla ya kuanza kwa msimu wa kujiandaa wa 2023-24.

Uhakika zaidi ni kwamba Arthur Zwane, ambaye ameiongoza Chiefs msimu uliopita na kumaliza katika nafasi ya tano kwenye Ligi Kuu ya DStv 2022-23, ni msimu wa nane sasa Kaizer hawajapata taji lolote na anaonekana kutokuwa na uwezekano mkubwa wa kuendelea na kazi hiyo.

Inaonekana Zwane anaweza kubakishwa katika kikosi cha kwanza cha makocha kama msaidizi, ingawa hilo linaweza kutegemea matakwa ya kocha mkuu mpya anayekuja.

Nabi aliiongoza Young Africans ya Tanzania, inayojulikana kama Yanga, kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho la Caf 2022-23 ambapo walipoteza kwa mabao ya ugenini dhidi ya USM Alger baada ya jumla ya mabao 2-2.

Raia huyo wa Tunisia, aliyejiunga na Yanga Aprili 2021, pia aliiwezesha klabu hiyo kutwaa taji lake la pili mfululizo la Ligi Kuu Tanzania Bara chini yake msimu wa 2022-23.

Pia alishinda Kombe la Shirikisho la Azam Sports (Kombe la FA la Tanzania) mfululizo 2021-22 na 2022-23, na kufanya kwa ligi na vikombe mara mbili katika misimu yake yote miwili katika klabu hiyo.

Yanga wiki iliyopita ilimtangaza Nabi kuondoka, ikisema katika taarifa yake: “Uongozi wa Young Africans Sports Club unapenda kuutaarifu umma umefikia makubaliano ya kuachana na Nasreddine Nabi baada ya kocha huyo kuomba kutoongeza mkataba mpya. ”

Vilabu vingine vilivyonolewa na Nabi tangu aanze taaluma yake mwaka 2013 ni Al-Ahly ya Libya, Al-Hilal ya Sudan, Ismaily ya Misri na Al-Merrikh ya Sudan.

Chiefs hawajavunja ukimya wao kuhusu mustakabali wa Zwane au mtu atakayechukua nafasi yake tangu mwisho wa msimu wa 2022-23 mwezi Mei.
-----------------------
 
Nabi naye bora angebaki tu msimu huu, halafu mwakani angetembea zake. Kuondoka kwake kuna kila dalili ya woga.

Ameona bora alinde heshima yake, huku akiusahau huu msemo wa "coaches are hired to be fired".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom