Na kadhalika na kadhalika

Na kadhalika na kadhalika

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,846
Reaction score
2,401
Mengi tumeyasikia ktk hotuba ya mh Rais. Wengine wakidhani ni mwanzo wa nchi ya maziwa na asali. Kimtazamo ni mwanzo wa nchi isiyo na mipango. Hivi tutatoa wapi billion zaidi ya 200 za kufidia upungufu wa ada na michango ya mbalimbali? Mbona kuna ujenzi wa barabara nyingi umesimama haujazungumziwa au kwa kuwa ni madeni? Amewataja wamachinga nk mbona hakuna mkakati wowote kisera wa kuwawezesha hawa na mama ntilie? Nchi haijengwi na mtu mmoja bali uwepo wa taasisi imara na endelevu. Kuiga la Kagame ni sawa na kuiga kwa Gaddafi ambapo uendelevu wake unategemea uhai wa mtu.
 
Mbwembwe tu hakuna jipya! mimi nasema ni nguvu ya soda.
 
Mengi tumeyasikia ktk hotuba ya mh Rais. Wengine wakidhani ni mwanzo wa nchi ya maziwa na asali. Kimtazamo ni mwanzo wa nchi isiyo na mipango. Hivi tutatoa wapi billion zaidi ya 200 za kufidia upungufu wa ada na michango ya mbalimbali? Mbona kuna ujenzi wa barabara nyingi umesimama haujazungumziwa au kwa kuwa ni madeni? Amewataja wamachinga nk mbona hakuna mkakati wowote kisera wa kuwawezesha hawa na mama ntilie? Nchi haijengwi na mtu mmoja bali uwepo wa taasisi imara na endelevu. Kuiga la Kagame ni sawa na kuiga kwa Gaddafi ambapo uendelevu wake unategemea uhai wa mtu.

bilion 200 ndo unaona nyingi kwa tanzania
kwa taarifa yako bandari pekeee inatosha kulingiza hiyo hela kwa mwezi ikisimamiwa vizuri
 
bilion 200 ndo unaona nyingi kwa tanzania
kwa taarifa yako bandari pekeee inatosha kulingiza hiyo hela kwa mwezi ikisimamiwa vizuri
Bandari ikiingiza zikaenda kwenye shule, vipi miradi iliyopangiwa pesa hizo? Na kadhalika na kadhalika
 
Usichukue mambo ya utawala wa Kikwete ukaweka kwenye utawala wa Magufuli. Utakosea sana. Hizi ni namba mbili tofauti
 
Ngoja sindano ikuingie. Acha kulalama. Kumbe ulikuwa mnufaika wa uozo pia?
 
Bandari ikiingiza zikaenda kwenye shule, vipi miradi iliyopangiwa pesa hizo? Na kadhalika na kadhalika

Magufuli alituhakikishia kuwa nchi hii ina fedha nyingi. Ila zilikuwa zinatafunwa na wachache
 
Rais magufuri anayo dhamira nzuri ila
1.nchi iko kwenye mkwamo mkubwa wa kiuchumi

2.deni kubwa la taifa lisilolipika kwa muda mfupi[takribani trillioni 40]

3.rushwa imetamalaki sana

kwa mazingira kama haya ni vigumu kufikia ahadi zake zote zinazofikia takribani trillion 70
watanzania wenzangu tusitegemee makubwa sana kwa kipindi cha miaka 5

ni kipindi kigumu cha kufunga mikanda

tufanye kazi jamani,tusitegemee ahueni yoyote
 
Tumtakie longlive Rais wetu mwenye dhamila ya ukombozi wa taifa letu. Doct. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI.
 
Rais magufuri anayo dhamira nzuri ila
1.nchi iko kwenye mkwamo mkubwa wa kiuchumi

2.deni kubwa la taifa lisilolipika kwa muda mfupi[takribani trillioni 40]

3.rushwa imetamalaki sana

kwa mazingira kama haya ni vigumu kufikia ahadi zake zote zinazofikia takribani trillion 70
watanzania wenzangu tusitegemee makubwa sana kwa kipindi cha miaka 5

ni kipindi kigumu cha kufunga mikanda

tufanye kazi jamani,tusitegemee ahueni yoyote
Kula like yangu mkuu!
 
Rais magufuri anayo dhamira nzuri ila
1.nchi iko kwenye mkwamo mkubwa wa kiuchumi

2.deni kubwa la taifa lisilolipika kwa muda mfupi[takribani trillioni 40]

3.rushwa imetamalaki sana

kwa mazingira kama haya ni vigumu kufikia ahadi zake zote zinazofikia takribani trillion 70
watanzania wenzangu tusitegemee makubwa sana kwa kipindi cha miaka 5

ni kipindi kigumu cha kufunga mikanda

tufanye kazi jamani,tusitegemee ahueni yoyote


Afadhali tukiongea kwa Takwimu. Bado kuna mgogoro kule Zanzibar unaviashiria vya kunyimwa misaada. Bado kuna bajeti za kukurupuka. Safari ni ndefu ila haiwezi kufanikiwa kwa kumtegemea Magufuli peke yake. Ajenge Taasisi imara.
 
Magufuli alituhakikishia kuwa nchi hii ina fedha nyingi. Ila zilikuwa zinatafunwa na wachache
Hajahakikisha bado. Amekiri kwamba makusanyo kwa zaidi ya miaka mitatu yamekuwa hayafikii malengo. Kumulika wafanyabiashara wakubwa ni jambo jema, lakini ameahidi nafuu ya kodi kwa hiyo ni zero sum game. Halafu toka ameanza kutoa hotuba amekuwa mahiri saana wa kutaja kilometa za barabara, sasa hivi tunataka awe mahiri wa kutaja miradi au mipango yake na fedha zitakapopatikana. Yeye si Waziri wa Barabara tena bali ni Rais.
 
Naomba audio ya hotuba ya Mh rais kwa mwenye nayo tafadhali.
 
Mkulu hii nchi ina vyanzo vingi vyakuingiza pesa tatzo tulikosa msimamizi. Bill 200 itapatkana bila shida.

Ukumbuke kuna yule mdudu mbaya wa manunuzi (PPA 2011) anatafutiwa dawa.
 
Wabongo akili zetu hatuzishughulishi ilishawahi kutolewa takwimu inayosema zaidi ya asilimia 40 ya bajeti inaenda mikononi mwa mafisadi ni asilimia 60 tu ndio inafanya kilichokusudiwa hivi unajua 40% ya Trilioni 22 ni ngapi ??????
 
Back
Top Bottom