Mzindakaya, Kimiti na Keenja watangaza kutogombea tena

Kama kumshambulia rais ndio sifa kuu ya utendaji kwa Tanzani; serikali ije JF na itapata washambuliaji wengi ambao wataweza kuliokoa taifa letu.

Watu wamepewa nafasi na wameshindwa, hao ndio tunaimba wanafaa kwasababu tu wamemshambulia rais? Give me a break! I will be the last one to buy into such argument.
 

- Tatizo ni kwamba vijana nao wamepewa nafasi wameshindwa, na mimi mkuu kama wewe nitakuwa mtu mwisho kumpa mtu kura eti kwa sababu ni kijana tu hayo ni mawazo ni mufilisi sana in the wake ya vijana kama Serukamba, nilifikiri tutaona aibu hata kusema maneno ya vijana tena!

Respect.


FMEs!
 
na ukifika uchaguzi mkapige kura kweli sio blahblah tu.
 

sijui ni nani aliyemention vijana akiashiria calibre ya akina Rostam, Masha Ngeleja. Ndulu na akina Serukamba..........walioshindwa/Wezi........

......hao vijana ukiangalia waliingiaje mpaka kufikia hapo walipo.....utaona/utajua........ni kwanini tumepata matokeo mabovu kutoka kwao..............

Sidhani kama kuna mwana JF ambaye atakimbilia kutaja majina ya hao vijana waliopitia kwenye System mbovu/iliyooza.......na bado wakachemsha eti ndio vijana wa kujivunia........
.........nobdoy hata Mkuu wangu Kasheshe siku hizi kabadilika........anamkoma Nyani kwa kwenda mbele..........

..........alikuwepo Zitto hapa JF........tulipomuona kachemka...wanaJF tulimshukia......hapendwi mtu....hapa....

Back to mada

........Wazee Kimiti na Mzindakaya wanaelekea kustaafu.......their action is plausible.......sasa watu wanapowashauri vijana waingie sidhani kama wana maana ya akina "Nungwi" or dizaini ya Rostam/Masha/Ngeleja/Serukamba waingie pale............

Tunataka watu wanaoelewa i.e wenye uwezo na uzalendo waingie kwenye kinyang'anyiro cha kuchukua hizo nafasi.......ili KUTUMIKIA wananchi wa hayo majimbo...........

Now the question comes back........how do we eliminate the Kinjes/Hizas type and Mzindakayas type.............CCM machinery failed us miserably.........give us your ideas Mkuu.........how?
 

well said Mkuu,...........
 

- Siwezi kurudia rudia mkuu, mimi sina tatizo na wazee wala vijana, ninachotaka viongozi wenye uwezo ambao so far kwenye vijana na wazee tulionao hatunao, sasa what to do labda wewe ndio ungesema otherwise inachosha sana kurudia ruida yale yale!

Respect.


FMEs!
 

Nami sipendi kurudia rudia....isipokuwa kwenye hili siwezi kuachia watu mediocre wakitetewa............

tumependekeza njia mojawapo ya kupata viongozi ni kuwapa back nguvu yao wananchi........na sio uporaji wa demokrasia wa sasa hivi......watu waachiwe wachague....na wakitaka kuwawajibisha....the bucks stops to wananchi.......unlike sasa hivi tukisema the backs stops kwa wananchi tunawaonea..........

One way ni Independent Candidates should be allowed........
 
 

- Mediocre wanaotetewa ni nani hapa? Viongozi waliotufikisha hapa tulipo in the last five years ni vijana, sasa kama ni mediocre ni taifa zima kuanzia viongozi mpaka wananchi hakuna wa kumlaumu mwingine!

Butiku na Matheo............tena sio mediocre tu ni JOKERS + WANAFIKI


........

Vijana wachache waliopewa nafasi ni mediocre.......na wametuangusha big time..........siwalaumu sana kwani wali/mepitishwana na system mbovu.....iliyopora nguvu ya wananchi..........

.......the point is .........Kwanini unilazimishe nichague CCM/Chadema/CUF/TLP/NCCR ili nipate k/viongozi (mediocres) kutumikia wananchi?.........huu ndio ninaouita UPORAJI WA DEMOKRASIA..................halafu baadaye ulaumu wananchi....eti viongozi ni reflection yetu wenyewe!!........HAPANA.......kwa misingi hii nasema BIG NO..........ndio maana rafiki yangu anaweza kusema wananchi tunakula/rewarded kwa kile tulichokichagua.............na wengine wanatuita eti BENDERA FUATA UPEPO.........yaani haki yangu unipore hala unaniita bendera fuata upepo.........please!


Hapana.........katika mazingira ya demokrasia iliyopo (Iliyoporwa) ni kuwaonea wananchi kusema "viongozi ni reflection yetu".....kwa ku-take advantage over them...........

...wachache wanaolifahamu hili jambo (i.e. uporaji wa demokrasia) wanapigwa sana vita kwani..........mijizi inaona itapoteza ulaji wakileta haki ya kuchagua na kuchaguliwa............

.....wananchi hawalazimishwi kujihusisha na chaguzi.......if that is the case.......well that may be your opinion.........however......some of us are not DEAD FISH........ndio maana tuko hapa JF

.........nakubaliana na wewe Independent Candidates inahitaji mada yake........lakini pale inapoweza kuwa-refered.......kama moja ya solution dhidi ya matatizo ya system ya demokrasia yetu sidhani kama kuna ubaya wowote.......
 
Wewe umelewa mikusu nini ? 1995-2000 steve galinoma, 2000-05 george fransis mlawa, 2005-10 steve galinoma. 1995 walimng'oa mwalimu mmoja wa primary ambaye alimshinda mlawa kwenye election ya 1990. MZAWA WA LYANDEMBELA WACHA KUPOTOSHA, HE IS AGED BUT VERY CONSTRUCTIVE MAN. NASIKIA KANDORO ANALIWINDA JIMBO HILO += VIJANA WENGINE, SASA KANDORO NAYE NI KIJANA MAANA WALIOSOMA NAYE PALE MASUMBO NI RETIRED OFFICERS!!!! NAKUBALIANA NA MWANAKIJIJI NA MKUU WA MEDANI ZA KIVITA FMES, TUANGALIE ZAIDI BRAIN NA UNYOOFU WA WAHUSIKA NA SI KWA SABABU PETER KISUMO KASEMA WAZEE WAONDOKE WAENDE WAPI? AU TUNAWANYIMA RASMI HAKI YA KUISHI NDANI YA NCHI YAO PIA ? TUSILETE UKABURU MPYA HAPA, MNAWAOGOPA WAZEE KWA LIPI? FANYENI NAO KAZI TUJIFUNZE KWAO NA WAO WAJIFUNZE KWETU NA NDIO MAANA YA UHAI, YOU KEEP ON LEARNING TILL YOU PART THIS WORLD.
 
Ni muda muafaka sasa tukafikiria pia kuwa na Mabunge ya aina mbili kama Marekani ili wazee safi kabisa kama Kimiti, Makweta,... wakawa Maseneta. Kila Mkoa ukachagua Seneta mmoja na kila halmashauri ikachagua Mbunge mmoja tu kuliko utitiri wa majimbo tulionayo na hivyo kuwa na Wabunge wengi mzigo kwa uchumi mdogo wa Taifa letu. Bunge letu la sasa ni kubwa mno bila sababu yoyote ya maana mbali na watu kuwekeza kwenye siasa!
 
Wewe umelewa mikusu nini ? 1995-2000 steve galinoma, 2000-05 george fransis mlawa, 2005-10 steve galinoma. 1995 walimng'oa mwalimu mmoja wa primary ambaye alimshinda mlawa kwenye election ya 1990. MZAWA WA LYANDEMBELA WACHA KUPOTOSHA, HE IS AGED BUT VERY CONSTRUCTIVE MAN. NASIKIA KANDORO ANALIWINDA JIMBO HILO += VIJANA WENGINE, SASA KANDORO NAYE NI KIJANA MAANA WALIOSOMA NAYE PALE MASUMBO NI RETIRED OFFICERS!!!! NAKUBALIANA NA MWANAKIJIJI NA MKUU WA MEDANI ZA KIVITA FMES, TUANGALIE ZAIDI BRAIN NA UNYOOFU WA WAHUSIKA NA SI KWA SABABU PETER KISUMO KASEMA WAZEE WAONDOKE WAENDE WAPI? AU TUNAWANYIMA RASMI HAKI YA KUISHI NDANI YA NCHI YAO PIA ? TUSILETE UKABURU MPYA HAPA, MNAWAOGOPA WAZEE KWA LIPI? FANYENI NAO KAZI TUJIFUNZE KWAO NA WAO WAJIFUNZE KWETU NA NDIO MAANA YA UHAI, YOU KEEP ON LEARNING TILL YOU PART THIS WORLD
 
FDR, kunani mkuu?
Mbona unapost mara mbili mbili kitu kile kile?
 
Kumbe mzee Kisumo bado anaishi?
 
Kwa muono wangu mitizamo kama hii inaashiria kuwa wengi tumegubikwa na hulka za ubaguzi wa kirika na jinsi gani tunapenda kutumia kauli mbiu ya UJANA kama nyenzo ya kuhalalisha uroho wetu wa UHESHIMIWA.


omarilyas

Mimi napenda sana kuangalia hoja yako kwa mtazamo mwingine kuwa, waheshimiwa wana kipya kweli hata tukiwapa nafasi nyingine?
 
Nimesoma hoja zote hapa. Nadhani kuna tatizo la kujiamini la vijana wengi. Ila sikutegemea kuwa tatizo hilo linawakumba pia baadhi ya wanaJF.

Hoja ya Ujana na Uzee katika siasa ni hoja dhaifu sana. Kwa mtazamo wangu ni sawa kabisa na hoja za ukabila, udini na nyingine za namna hiyo katika siasa. Ni hoja za kijinga.

Taifa haliwezi kuendelea kwa kuwa na wanansiasa wanaopatikana kwa umri wao au sura zao. Nchi itaendelea kwa uwezo wa viongozi wake wa rika zote, wenye sura mbalimbali. Kinachohitajika zaidi ni nidhamu, uaminifu, uwezo (kimwili, kiakili, na uzoefu) na nia ya kuleta maendeleo yanayohitajika.

Katika post mbalimbali, imeonekana waliodhaniwa ni vijana na wangeweza kufanya kazi nzuri, wameshindwa kufikia hata malengo madogo tu. Kuna wazee pia ambao hawajaweza kufanikiwa kutimiza yanayotegemewa na wengi. Ila mimi nadhani, vijana na wazee, hata wakibadlishwa kwa kiasi gani, hawawezi kuleta mabadiliko makubwa hadi hapo uongozi wa juu kabisa wa nchi utakapokuwa na nia ya kubadilisha system ya uongozi na utawala wa nchi. System yetu (na hasa Katiba) inahitaji marekebisho makubwa. Viongozi wengi hawana mamlaka, uwezo wala nyenzo za kutimiza majukumu yao kwa asilimia kubwa.

Wabunge na wanasiasa wengine, wanayo nafasi sawa na wengine wote kugombea tena Ubunge, endapo wanataka/wanaona vyema kufanya hivyo. Si sahihi kudhani kuwa, umri au muda wa mtu kuwa Mbunge ni sababu ya kumtaka aachie nafasi hiyo. Maana nafasi hiyo anapewa na wanaomchagua, na wao ndio wenye mamlaka ya kumchagua mwingine watakapoona kuwa wanahitaji kufanya hivyo. Kwanini tushabikie Mbunge wa watu aachie madaraka ili eti kijana achukue nafasi hiyo? Mantiki yake hasa ni nini? Tena bila kutoa sababu za maana.

Tuwaachie wananchi wachague wabunge wao. Kama wanamtaka Mbunge waliekuwa nae tangu Uhuru, ni haki yao kumchagua. Kama wanamtaka Mbunge mwenye umri wa miaka 18 au miaka 81, pia ni haki yao kumchagua. Wao wanajua wanamtakia nini, kwakuwa atakuwa mwakilishi wao.
 

SAFI SANA WildCard.
 
Hivi na huyu Mkenya - mkikuyu Mungai bado unasubiri nini kutangaza kujitoa kugombea!!! Unangoja hadi uaibishwe na vijana??? Tangu tunazaliwa wewe mbunge wa Mufindi hadi leo!!!!!!! USHAURI WA BURE MKIKUYU MUNGAI pumzika usichukue kabisa form za ubunge. Endelea kutafuna pesa za miradi yako uliyojiuzia kwa kuwadhulumu wana Mufindi/ Mafinga hasa mashamba ya chai na viwanda vyake pamoja na kiwanda cha karatasi mgololo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…