Mzimu wa kutendwa!

Mzimu wa kutendwa!

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Siku hizi vijana ambao hawajaoa wamekuwa wakisema kuwa mwenza wanaemhitaji wanataka awe hivi au vile ili kujiridhisha

Dhana hii inatokana na dhana nyingine ambayo vijana tumejijengea kuwa ukiwa na mtu wa aina fulani utaifurahia ndoa wakati hata ndoa yenyewe hatuijui,matarajio haya ndio ambayo yanasababisha vijana wengi kuja kuiona ndoa kama uongo ambao umekuwa ukihubiriwa sana na watu ambao umri umekwenda kwani hakuna raha na furaha ambayo imekuwa ikisemwa

Wakati vijana tukiilaani ndoa tunakuwa tumejisahau sana kuwa tulijenga maamuzi yetu kwenye dhana ambazo wala hatukuwa na ushahidi wowote kama zina ukweli wowote

Maisha ni mchezo ambao mara nyingi unaweza kumfanya mtu ajikute mahali ambapo anaweza kuwalaumu sana waliomleta duniani au kuwasifia

Vijana hawa ambao wamekuwa wakitarajia matamu mengi wenye ndoa au uhusiano na mtu mwenye sifa ambazo alidhani zinamsaidia kuyafanya mahusiano hayo kuwa matamu,mambo yanageuka na kuwa kinyume,anatendwa...

Hapo maisha hubadilika na kuwa mengine,kijana huyu anaishi kwenye hofu nyingi sana za kutendwa hadi anauharibu ujasiri wake kwenye mahusiano na kuanza kuwa mwoga wa kutendwa

Kitendo hiki kinamfanya kijana huyu kuanza kuchagua sana watu wa kuwa nae kwenye mahusiano huku akiwa hajiamini kwa kuandamwa na mzimu wa kutendwa na mtu wake wa mwanzo

Kufikia hatua hii kijana huyu hawezi tena kujisimamia,anaanza kuwa mtu wa kulaumu tu

Ni kweli kuwa sasa kutafuta mke wa kuoa au mume ni kazi ngumu pengine sawa kabisa na kutafuta hela,lakini kwa ambae tayari ametendwa na anaishi kwa kufuata maumivu ya kutendwa ni ngumu zaidi mara dufu

Inafikia mahali mtu hajiamini tena na anaweka sana masharti kiasi kwamba mtu ambae anakuwa nae kwenye mahusiano anaona kama yupo jela ndogo

Mwenza wake akitoka bila kuaga ni ugomvi,anawaza kaenda kufanya kama ya yule aliyemtenda,akichelewa kazini hivyo hivyo,akipokea simu na kutoka nje nako ni hivyo hivyo

Watu hawa wanakuwa wanayafanya maisha na mahusiano yao mapya kuwa magumu wenyewe kwasababu wanakuwa hawaamini tena wenzao na kuona kila mmoja ni mkosaji

Jifunze kujifunza na kuwaamini wenzako

Ukipita barabara hii na ukaporwa simu haina maana kuwa kila siku ukipita barabara hiyo au nyingine utaporwa pia!
 
^^
Haaaa inategemea na kiwango cha kutendwa!!
Kuna watu wanajua kutenda mpaka wanakufikisha kwenye point of no return
^^
 
^^
Haaaa inategemea na kiwango cha kutendwa!!
Kuna watu wanajua kutenda mpaka wanakufikisha kwenye point of no return
^^

Mkuu,

Kiwango tunakiweka sisi wenyewe wala sio mtu mwingine

Unaweza kujiuliza tu ni kuwa unaweza kuwa umetendwa kwa kiwango ambacho wewe unakiona kuwa ni kikubwa na ikaona kuwa umetendwa jambo baya sana kwa kiwango kikubwa sana hadi ukatamani ufe

Upande wa pili kuna mtu ambae ametendwa kama wewe lakini ameliona kuwa ni jambo la kawaida sana wala hata halifikirii kabisa

Katika watu hao wawili unadhani ni kitu gani kimewafanya watu hao walione jambo lilelile kwa viwango tofauti?
 
Sahihi kabisa mkuu haya mambo kwa sasa yamekuwa ya kuhisiana vibaya tu..wewe utamwamini yeye hakuamini basi tabu tupu..watu walishang'atwa na nyoka bwana.,
 
Sahihi kabisa mkuu haya mambo kwa sasa yamekuwa ya kuhisiana vibaya tu..wewe utamwamini yeye hakuamini basi tabu tupu..watu walishang'atwa na nyoka bwana.,

Unapong'atwa na nyoka ni ujumbe kuwa kuna ka uzembe ulikafanya mahali hivyo inatakiwa kuwa makini na sio kuwa mwoga

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuwa makini na kuwa mwoga!
 
Ujumbe murua sana,la kuongezea ni kwamba wengi wanapooa au kuolewa wanadhani wanakuwa wamemaliza matatizo yao

yote,au anafikiri kwa kumchagua mtu sahihi itakuwa ni amani tu huyo mtu hawezi kosea hata siku moja,matokeo yake

mambo yakiwa ni kinyume inakuja lawama,ndugu tu tuliozaliwa nao tumbo moja tunagombana sembuse mtu mliyekuja

juana ukubwani?? kinachotakiwa ni kutatua tatizo na hizo changamoto ziwe ni ngazi za kupandia kwenye hitimisho

zuri la furaha.
 
dunia sasa imani imekwisha

hii nyimbo aliimba marijani rajabu
ila sina uhakika
 
Unapong'atwa na nyoka ni ujumbe kuwa kuna ka uzembe ulikafanya mahali hivyo inatakiwa kuwa makini na sio kuwa mwoga

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuwa makini na kuwa mwoga!

Watu wengine wana jema mkuu umpe nini asikutende dawa hapo kama unavyosema kuwa makini na woga tupa kule...then kaicheze ngoma.,
 
Utaleta vipi furaha na amani kwa mwenzako wakati wewe mwenyewe umeingia kwenye mahusiano na emotional baggage, Hiyo sio healthy relationship na muda utaexpose tu hizo cracks.
 
And the more you get exposed with dsyfunctional relationships the lesser your trust
 
And the more you get exposed with dsyfunctional relationships the lesser your trust

Raha ya mapenzi ni ku trust blindly.....ukiweza hiyo uta enjoy....machale machale yanaua mno mapenzi...sasa ndo naielewa ile thread ya Kaunga ya kuishi kimachale machale
 
Last edited by a moderator:
And the more you get exposed with dsyfunctional relationships the lesser your trust

Naamnini kila mtu yupo responsible for his/her own actions, ukiona you jumping from one dysfunctional relationship to the other, jua wewe mwenyewe ndivyo ulivyo{dysfunctional}. We attract what we are not what we want, uta trust vipi wakati we mwenyewe you cant be trusted
 
Naamnini kila mtu yupo responsible for his/her own actions, ukiona you jumping from one dysfunctional relationship to the other, jua wewe mwenyewe ndivyo ulivyo{dysfunctional}. We attract what we are not what we want, uta trust vipi wakati we mwenyewe you cant be trusted

kuna ukweli hapa,japo it doesnt always apply..
 
Mkuu,

Kiwango tunakiweka sisi wenyewe wala sio mtu mwingine

Unaweza kujiuliza tu ni kuwa unaweza kuwa umetendwa kwa kiwango ambacho wewe unakiona kuwa ni kikubwa na ikaona kuwa umetendwa jambo baya sana kwa kiwango kikubwa sana hadi ukatamani ufe

Upande wa pili kuna mtu ambae ametendwa kama wewe lakini ameliona kuwa ni jambo la kawaida sana wala hata halifikirii kabisa

Katika watu hao wawili unadhani ni kitu gani kimewafanya watu hao walione jambo lilelile kwa viwango tofauti?

^^
, MkuuUmehawi kutendwa?
^^
 
nakumbuka growing up nilikuwa naiingia kwenye relationships with all emotional doors closed kwa kuhofia kutendwa, tatizo lake ni kwamba unadate mademu kibao lakini hakuna anayekujua on a personal level kwa ajili ya mask uliyovaa.

moral of the story nilikuwa kwenye mahusiano,but deep inside I was empty, I changed my ways na I am lovin the new me.
 
Back
Top Bottom