Hakuna cha timu wala nini, tatizo hasa ni hawa wasanii wa kibongo kuishabikia CCM kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana 2015. Kuanzia Diamond, Kiba, Raymond, Vanessa mpaka Ya moto band walikuwa busy kwenye majukwaa ya kampeni za CCM wakipiga push up na kumdhihaki Lowassa, wakidhania watanzania wote ni wajinga tu.
Wengi wetu tuliapa kamwe hatutawapigia kura tena hawa wasanii katika kuwania hizo Tuzo.
Na huu ni mwanzo tu, makubwa yanakuja zaidi. Kama wanabisha wamuulize yuko wapi Nakaaya na Maro. Mpaka leo wanajuta kuipigia kampeni CCM 2010, maana tuliwazika rasmi.