Mzee Sitta Kuunguruma Leo Ofisini Kwake

Mzee Sitta Kuunguruma Leo Ofisini Kwake

Kapela Msonda

Member
Joined
May 29, 2009
Posts
39
Reaction score
11
Waziri wa Uchukuzi, Mzee Samwel Sitta leo saa tano na nusu asubuhi ataongea na waandishi wa habari ofisini kwake kumaliza mzizi wa fitna ndani ya wizara yake, msemaji wake James Rock Mwakibinga amesema. Ujumbe kamili wa msemaji huyo wa Mzee wa Kasi na Viwango unasomeka:
"Ndgu.Mwandishi, kwa nafasi yako wewe ya kipekee unaombwa kufika Wizara ya Uchukuzi leo siku ya Jumapili trh 29/3 kuanzia saa 5 na 30 asbh ,Waziri wa Uchukuzi Mh.Samuel Sitta atazungumza na waandishi wa habari. Ukipata ujumbe huu naomba unijulishe. Ni Mimi James Rock Mwakibinga"
 
Nitakuwa bariadi lakini kwakuwa jf ipo nitafuatilia hapahapa jf mtujuze nyie watu wa dar.
 
Nitakuwa bariadi lakini kwakuwa jf ipo nitafuatilia hapahapa jf mtujuze nyie watu wa dar.

Ccm bana yaani huyu mzee kaona watu tumempotezea sasa anaona atoke vipi wiki jayo mwakyembe nae atatoka na yake hii nchi ya kisanii sana.
 
Sitta yule aliyefoji kura katiba maalumu? au sitta yupi jamani?? kama ni yule wa katiba maalum ni uchafu ktk taifa hata attention haipaswi kumpa, eti zakia kaingia kama mtanganyika ila kura akapiga kama mzenji, aaa 6 huyuuuuu
 
hilo lizeee mm nililichukia toka lipitishe katiba ya majangili
 
Watanzania ukiwafanyia ubaya wanakulipa hapohapo. Asahau Uraisi.
 
Kwa nini ataunguruma! au atakuwa anaumwa! Anyway, mwambien kosa kubwa aliloifanyia nchi hii ni uhujumu katiba mpya.
 
hilo lizeee mm nililichukia toka lipitishe katiba ya majangili

Hiyo ndo inaitwa ntoke vipi alitegemea kura itawezekana katiba mpya impe chati angalau ya kiongo na kweli sasa anaona imebuma kura hamna bora atoke kivingine
 
Back
Top Bottom