Ndugu zangu,
Katika nchi, uwepo wa uhuru wa kujieleza ni jambo muhimu sana. Maana, nchi haijengwi kwa dhahabu au almasi bali fikra za watu. Na katika nchi, uwepo wa fikra tofauti ni jambo jema kabisa.
Na kwangu mimi, Mzee Mwinyi namwona kuwa ni mmoja wa WaTanzania ambao ametoa mchango mkubwa katika kujenga utamaduni wa kuvumilia fikra tofauti na hata zenye kushutumu. Na mpaka sasa, akiwa amebaki na miaka minne madarakani, Jakaya Kikwete namwona kuwa ni kiongozi anayeonyesha uvumilivu mkubwa wa fikra zenye kushutumu , hivyo basi, kuchangia katika kuimarisha misingi ya uwepo wa fikra huru, hivyo basi, demokrasia. Na kimsingi haya ya ufisadi yaliimarika zaidi enzi za Mkapa. Enzi za Mkapa hayakuwekwa wazi, lakini wakati huu wa Kikwete ameonyesha kuruhusu kuanikwa hadharani.
Ndugu zangu,
Tuliokuwepo tunakumbuka, kuwa pamoja na mema ya Mwalimu, lakini, enzi za Nyerere hakukuwa na uhuru wa fikra. Na si kweli kuwa enzi za Ben Mkapa zilikuwa za Ukweli na Uwazi. Hicho kilikuwa ni kibwagizo tu cha kwenye mikutano na hotuba za Mheshimiwa.
Na namkumbuka Mkapa kwa kauli yake hii; Tanzania hakuna waandishi wa habari. Akamsifu sana mwandishi Riz Khan akisahau kuwa naye ' Mkapa', alikuwa mwandishi wa habari na waziri wa habari katika Tanzania. Na Mkapa aliposema Tanzania hakuna waandishi wa habari labda alikuwa na maana, kuwa mwandishi wa habari aliyebaki alikuwa ni yeye tu!
Kauli ile ya Mkapa kwa wanahabari inanikumbusha miaka ile ya 80. Kwenye moja ya hitimisho la mifungo ya Ramadhan, Sheikh Yahya akatamka; " Ramadhan hii WaTanzania waliofunga ni wawili tu". Baada ya kusikia hayo ya Sheikh Yahya, basi, kilichonijia kichwani ni hiki; yumkini wawili hao waliofunga ni Sheikh mwenyewe na mkewe!
Na ruksa kwa wenye kutaka kunishambulia kwa haya niliyoyaandika.
Maggid,
Njiani kwenda Iringa.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
Katika nchi, uwepo wa uhuru wa kujieleza ni jambo muhimu sana. Maana, nchi haijengwi kwa dhahabu au almasi bali fikra za watu. Na katika nchi, uwepo wa fikra tofauti ni jambo jema kabisa.
Na kwangu mimi, Mzee Mwinyi namwona kuwa ni mmoja wa WaTanzania ambao ametoa mchango mkubwa katika kujenga utamaduni wa kuvumilia fikra tofauti na hata zenye kushutumu. Na mpaka sasa, akiwa amebaki na miaka minne madarakani, Jakaya Kikwete namwona kuwa ni kiongozi anayeonyesha uvumilivu mkubwa wa fikra zenye kushutumu , hivyo basi, kuchangia katika kuimarisha misingi ya uwepo wa fikra huru, hivyo basi, demokrasia. Na kimsingi haya ya ufisadi yaliimarika zaidi enzi za Mkapa. Enzi za Mkapa hayakuwekwa wazi, lakini wakati huu wa Kikwete ameonyesha kuruhusu kuanikwa hadharani.
Ndugu zangu,
Tuliokuwepo tunakumbuka, kuwa pamoja na mema ya Mwalimu, lakini, enzi za Nyerere hakukuwa na uhuru wa fikra. Na si kweli kuwa enzi za Ben Mkapa zilikuwa za Ukweli na Uwazi. Hicho kilikuwa ni kibwagizo tu cha kwenye mikutano na hotuba za Mheshimiwa.
Na namkumbuka Mkapa kwa kauli yake hii; Tanzania hakuna waandishi wa habari. Akamsifu sana mwandishi Riz Khan akisahau kuwa naye ' Mkapa', alikuwa mwandishi wa habari na waziri wa habari katika Tanzania. Na Mkapa aliposema Tanzania hakuna waandishi wa habari labda alikuwa na maana, kuwa mwandishi wa habari aliyebaki alikuwa ni yeye tu!
Kauli ile ya Mkapa kwa wanahabari inanikumbusha miaka ile ya 80. Kwenye moja ya hitimisho la mifungo ya Ramadhan, Sheikh Yahya akatamka; " Ramadhan hii WaTanzania waliofunga ni wawili tu". Baada ya kusikia hayo ya Sheikh Yahya, basi, kilichonijia kichwani ni hiki; yumkini wawili hao waliofunga ni Sheikh mwenyewe na mkewe!
Na ruksa kwa wenye kutaka kunishambulia kwa haya niliyoyaandika.
Maggid,
Njiani kwenda Iringa.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo