Mzee Farijala wa CCM Amshambulia Dkt. Charles Kitima

Mzee Farijala wa CCM Amshambulia Dkt. Charles Kitima

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2008
Posts
10,565
Reaction score
7,988
Salam Wana JF,

Bila kutarajia asubuhi hii nimejikuta nalazimika kuitazama television ya TBC1 kwakua mazingira niliyokuwepo ndio channel pekee ya nyumbani inayoonekana.

Mtangazaji wa TBC1 amemkaribisha studio mzee Farijala ambaye ni kada wa CCM. Katika mazungumzo yake amejikita katika kumshambulia aliyekuwa Makamu Mkuu wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) cha Mwanza Dkt. Charles Kitima, kwamba pamoja na kuwa amesomeshwa na CCM lakini amekuwa akiikisoa sana na kuilaumu serikali ya CCM.

Mzee huyo anadai kuwa anamfahamu sana Dkt. Kitima kwamba ametoka katika familia duni sana alikuwa akivaa kaniki lakini leo hii amesahau fadhila ya serikali ya CCM.

Pia amezungumzia wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutofanya siasa kwa madai kuwa wako vyuoni kusoma na si kufanya siasa akitolea mifano vyuo vya SAUT TABORA NA SAUT MWANZA.
 
CCM ingekuwa na wazee isingefika hapa ilipofika. Kama wapo basi wameichoka na wameamua kuiacha ife kibudu.
 
Mwita ni kweli namie nimemuona na kumsikiliza hadi nikaona kama Wazee waliobaki CCM ndiyo hao basi CCM hakuna Wazee. Mf. Ameulizwa na mtangazaji kuhusu Tanzania imefikia wapi kwenye malengo ya milenia yanayokamilika 2015, mzee yeye kaenda kwenye mabomu ya Arusha, mtangazaji amejitahidi sana kumweka kwenye mstari waapi! Hivi huyo Mzee Farjalla ndiyo yule fisadi wa EPA?
 
Yule kitima ni janga kuu la taifa, mtokwa povu tu. Njaa inamsumbua
 
Yule kitima anatumika kama kile kifaa ambacho huwa kinatumika mara moja na kutupwa jalalani, ameahidiwa ubunge viti maalum na chadema
 
Haka kazee hakana jipya, bado kako Stone Age! Kajinga kweli
 
Mwita Maranya
Hivi mtu akisema una mapengo atakuwa amekushambulia au ameeleza hali halisi?
cc Ritz, Chilisosi

Mkuu chama nilichoandika hapa ni kwa kifupi sana lakini kiujumla alikuwa anazungumzia personal affairs za Dkt. Kitima wakati wakati kipindi kinaanza wamesema atazungumzia bajeti ya mwaka 2013/14.
Unachosema wewe ni kitu tofauti kabisa na kinachofanyika studio kwakuwa hakuna uchambuzi wowote bali wanafanya mashambulizi dhidi ya SAUT na Dkt. Kitima hadi Marine analazimika kusawazisha mambo kwa kutaa vyuo vingine wakati kada mwenzako anazungumzia chuo kimoja tu na mkuu wake.
 
Last edited by a moderator:
Mzee farijalla lazima angetoa tu lawama kwani awezi kushambulia wana ccm kwa sababu kuna madudu mengi nyuma yake ila wajue kuwa ccm imeshikwa pabaya na hawana pakutokea.
 
Mtaji wa ccm kwa sasa ni wazee kama hao waliojichokea na kudanganywa na pilau,shati la kijani,buku 5.Mzee Farijala ulidanganywa mwaka 2005 mtapewa mahakama ya kadhi na ccm,mpaka leo hakuna kitu,bakwata imekula deal kuna kadhi asiyetambuliwa na katiba wala sheria.
 
Haha! Hao wengine ni kwa ajili ya kuhakiki post kwa ajili ya malipo. Halafu lazima ujue kuwa mbomoa hoja inataka kuwa na kichwa kizuri, hawa wanaonekana hata shule walikuwa watu wa kuibia.

sasa kilaza kama wewe una hoja gani zaidi ya kutumika tu hapa. Kutwa usiku na mchana unajiongezea vi mia mbili mia mbili kwenye post hapa jf. Leo umeanza mapem hadi mda wa chai utakuwa na ef 3
 
Mwita ni kweli namie nimemuona na kumsikiliza hadi nikaona kama Wazee waliobaki CCM ndiyo hao basi CCM hakuna Wazee. Mf. Ameulizwa na mtangazaji kuhusu Tanzania imefikia wapi kwenye malengo ya milenia yanayokamilika 2015, mzee yeye kaenda kwenye mabomu ya Arusha, mtangazaji amejitahidi sana kumweka kwenye mstari waapi! Hivi huyo Mzee Farjalla ndiyo yule fisadi wa EPA?

Sasa na huyo mtangazaji kumuuliza Mzee Mambo ya Malengo ya Millenia; mzee atayajulia wapi wakati kama kweli ni mzee alizaliwa millenia iliyopita. Hiyo MDG ataijulia wapi? Amemuonea tu ndio maana akakimbilia kwenye mabomu kwa kuwa ndicho kitu alichokisiakia hivi karibuni.

Mkuu hapo kwenye: Yule wa EPA si yupo Lupango! Labda huyu ni baba yake au babu yake manake wote Makada.
 
Mkuu chama nilichoandika hapa ni kwa kifupi sana lakini kiujumla alikuwa anazungumzia personal affairs za Dkt. Kitima wakati wakati kipindi kinaanza wamesema atazungumzia bajeti ya mwaka 2013/14.
Unachosema wewe ni kitu tofauti kabisa na kinachofanyika studio kwakuwa hakuna uchambuzi wowote bali wanafanya mashambulizi dhidi ya SAUT na Dkt. Kitima hadi Marine analazimika kusawazisha mambo kwa kutaa vyuo vingine wakati kada mwenzako anazungumzia chuo kimoja tu na mkuu wake.

mkuu Mwita Maranya
Hivi wewe mwenyewe ni mara ngapi umeongoza mashambulizi dhidi ya raisi JMT mpaka leo ushangae anaposhambuliwa mtu mdogo kama Dr. Kitima? personal attacks ni sehemu ya siasa kwa usiliogope wala usilikatae!
 
Last edited by a moderator:
Sasa huyu mzee naye anaongea nini??? Hajui watanzania wengi tu ulikuwa tunavaa hizo kaniki cuz hata nchi ilikuwa haina nguo kipindi hicho hadi mwinyi aliporuhusu MITUMBA.

Dkt Kitima ni mtu makini sana, na kwa msomi yeyote sioni kama itakuwa busara wala jambo la heri kukaa kimya huko akiona mambo ndani ya nchi yake yakienda hovyo kama ilivyo sasa. Kuhusu Kusomeshwa na serikali ya ccm-Ni upuuzi kuona kuwa kila aliesoma enzi za ccm anyamazie upuuzi wa ccm ya sasa. Kwanza ni wajibu wa serikali kusomesha wananchi wake na wala isitegemee fadhila baada ya kuwasomesha ikiwamo kusifiwa hata kwa mambo yasokuwa ya msingi na ambayo yanaharibu misingi ya utaifa.

Go Dr. Kitima, Achana na hawa makada waliopoteza mwelekeo kwa kuendekeza u-ccm.
 
mkuu Mwita Maranya
Hivi wewe mwenyewe ni mara ngapi umeongoza mashambulizi dhidi ya raisi JMT mpaka leo ushangae anaposhambuliwa mtu mdogo kama Dr. Kitima? personal attacks ni sehemu ya siasa kwa usiliogope wala usilikatae!

Sasa chama hapa Dkt. Kitima anahusikaje na bajeti ya serikali?

Mimi namshambulia raisi Kikwete pale anaposhindwa kutimiza majukumu yake kwa wananchi.


Sasa ninyi maccm mnapomshambulia Dkt. Kitima yeye ni nani katika serikali yenu ya ccm?
 
Last edited by a moderator:
Salam Wana JF,

Bila kutarajia asubuhi hii nimejikuta nalazimika kuitazama television ya TBC1 kwakua mazingira niliyokuwepo ndio channel pekee ya nyumbani inayoonekana.

Mtangazaji wa TBC1 amemkaribisha studio mzee Farijala ambaye ni kada wa CCM. Katika mazungumzo yake amejikita katika kumshambulia aliyekuwa Makamu Mkuu wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) cha Mwanza Dkt. Charles Kitima, kwamba pamoja na kuwa amesomeshwa na CCM lakini amekuwa akiikisoa sana na kuilaumu serikali ya CCM.

Mzee huyo anadai kuwa anamfahamu sana Dkt. Kitima kwamba ametoka katika familia duni sana alikuwa akivaa kaniki lakini leo hii amesahau fadhila ya serikali ya CCM.

Pia amezungumzia wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutofanya siasa kwa madai kuwa wako vyuoni kusoma na si kufanya siasa akitolea mifano vyuo vya SAUT TABORA NA SAUT MWANZA.

Huyo mzee ni mbumbumbu tu hajui anachokisema! Ccm ina mashamba? Watu wanasomeshwa kwa kodi za wananchi wote sio za ccm!
 
Sasa chama hapa Dkt. Kitima anahusikaje na bajeti ya serikali?

Mimi namshambulia raisi Kikwete pale anaposhindwa kutimiza majukumu yake kwa wananchi.


Sasa ninyi maccm mnapomshambulia Dkt. Kitima yeye ni nani katika serikali yenu ya ccm?

mkuu Mwita Maranya
Lazima atakuwa anahusika kwa namna moja ama nyingine nina uhakika mtoa mada anajua nini anachoongea; kwani kuna ubaya kwa mwanaccm kukamata kamanda mmoja na kutoa mashambulizi? Mbona wewe unayafanya sana humu jamvini?
 
Last edited by a moderator:
sahihi mkuu, na hivi karibuni msomi wa chuo kikuu udsm amefanya utafiti na kubaini kuwa wanaoishabikia chadema ni wavivu na wanapenda vya bure na vya kupewa..

Msomi wa chuo kikuu?! Kwa taarifa yako huko vikuu ndio kuna wasomi wanao tumika kuliko unavyofikiri! Hivi unajua mbunifu wa kauli mbiu "Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya?", unamjua mbunifu wa kauli mbiu "Maisha bora kwa kila mtanzania?" Ni mtu mahiri aliye chuo kikuu! Ukiulizwa kauli mbiu zake zimefanyaje kazi kupitia mtu aliye muandikia utashangaa! Au hujui kuwa hata aliye sema "We will mafucture teachers" naye ni msomi wa chuo kikuu cha dsm?! Au hujui kuwa hata aliyesema kuwa "Sijui sababu za wananchi wangu kuwa maskini?" Naye ni mshika shahada wa chuo kikuu bora Afrika

Muambie huyo msomi wako wapenda vya bure ni wale wanao hongwa chumvi, kofia, t shirt na khanga ili wachaguliwe.

Tumia akili usitumike tu bila kushirikishaa ubongo wako.
 
Back
Top Bottom