Kimbojo
JF-Expert Member
- Apr 12, 2009
- 387
- 54
Leo asubuhi Mzee Farijala ameifagilia Star TV kwa kuamini kwamba STAR TV wako upande wao (CCM) ndo maana anaalikwa mara kwa mara kwenye vipindi vyao na kuichana ITV hadharani kuwa inatumika na wapinzani kwa.
Hii imedhihirisha kwamba huyu mzee huwa anahudhuria vipindi ili kukitetea chama chake na sio maslahi ya Taifa. kuna kipindi alialikwa wakati wa mgomo wa madaktari akawatukana madaktari kwa kuwaita ni wala rushwa wakubwa( wanapokea rushwa kwa wagonjwa) na leo kichana ITV kupitia STAR TV. Hoja yangu hapa ni kwamba si dhani kama huyu mzee ana sifa za kualikwa kujadili mambo yahusuyo nchi kwa ujumla wake, STAR TV wapime uzito wa mada na waangalie watu wa wakushiriki katika mada husika. Huyu Mzee anafaa kualikwa kwenye vikao vya fitna na majungu ndani ya chama chake. La sivyo mkiendelea kumualika mtakidharaulisha kituo chenu/chetu na pengine mtaendelea kuomba radhi kwa wengine ambao wataendelea kudhalilishwa kupita kweu STAR TV kama Yahaya ulivyoomba radhi kwa ITV .
Hii imedhihirisha kwamba huyu mzee huwa anahudhuria vipindi ili kukitetea chama chake na sio maslahi ya Taifa. kuna kipindi alialikwa wakati wa mgomo wa madaktari akawatukana madaktari kwa kuwaita ni wala rushwa wakubwa( wanapokea rushwa kwa wagonjwa) na leo kichana ITV kupitia STAR TV. Hoja yangu hapa ni kwamba si dhani kama huyu mzee ana sifa za kualikwa kujadili mambo yahusuyo nchi kwa ujumla wake, STAR TV wapime uzito wa mada na waangalie watu wa wakushiriki katika mada husika. Huyu Mzee anafaa kualikwa kwenye vikao vya fitna na majungu ndani ya chama chake. La sivyo mkiendelea kumualika mtakidharaulisha kituo chenu/chetu na pengine mtaendelea kuomba radhi kwa wengine ambao wataendelea kudhalilishwa kupita kweu STAR TV kama Yahaya ulivyoomba radhi kwa ITV .