Mzee Akilimali acharuka, aapa Manji hatorudi Yanga

craq

JF-Expert Member
Mar 22, 2017
859
1,864
-Mjumbe wa Baraza la wazee wa klabu ya Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali amemshangaa Mwenyekiti wa baraza la wadhamini wa klabu ya Yanga, George Mkuchika kwa kukiuka katiba ya klabu ya Yanga kuhusu maagizo ya BMT kupitia shirikisho la soka Tanzania (TFF) la kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi 6 za uongozi ndani ya klabu ya Yanga.

-Mzee Akilimali amesema wajumbe wanne waliobaki walikubaliana na TFF kuhusu kufanya uchaguzi na wakasaini makubaliano ya kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi sita ndani ya klabu ya Yanga sasa amelishangaa Baraza la wadhamini kuingilia majukumu ya kamati tendaji ya klabu. Akilimali ameenda mbali zaidi na kusema kwa mujibu wa katiba ya Yanga kazi ya Baraza la wadhamini ni kulinda mali za klabu tu na si kupitisha maamuzi ya kikao au kuitisha mkutano wa klabu.

-Mzee Akilimali ameuliza why Bwana Yusuph Manji amekuwa wa kusemewa kila siku kama Manji anataka kurudi Yanga kwa nini asijitokeze hadharani atangaze yeye mwenyewe kuliko kuja kusemewa na watu na ameomba TAKUKURU kuichunguza barua iliyosomwa jana na Mkuchika inayodaiwa kuandikwa na Yusuph Manji. Akilimali amesema kuna watu wanatumiwa ndani ya klabu ya Yanga na hawafuati katiba ya Yanga. amesema yeye kamwe hatakubali katiba ya Yanga ivunjwe na watu wachache kwa maslahi yao wenyewe.

FB_IMG_1542011212759.jpg
 
Huyu mtu ni mvurugaji wa mambo tu?Yanga inahitaji pesa,viingilil havitoshi kabisa kulipa mishahara sasa pesa tunapata wapi?Hatusemi manji atoe zake za mfukoni bali manji kama mwenyekiti ni mfanya biashara aliyefanikiwa kwa hiyo ana mbinu na uwezo wa kututoa hapa tulipo
 
huyu mzee nadhani ndiyo amebaki huko vyurani ninayemkubali,huwa hakopeshi mtu,utamnyenyekea mtu hadi lini? Hivi manji ndiyo angetekwa kama alivyotekwa mo si wanayanga tungejikojolea
 
Huyu mtu ni mvurugaji wa mambo tu?Yanga inahitaji pesa,viingilil havitoshi kabisa kulipa mishahara sasa pesa tunapata wapi?Hatusemi manji atoe zake za mfukoni bali manji kama mwenyekiti ni mfanya biashara aliyefanikiwa kwa hiyo ana mbinu na uwezo wa kututoa hapa tulipo
Kwa maana hiyo ndo akanyage katiba ya Yanga kwa kushirikiana na baraza la wadhamini? Sheria na taratibu zinatakiwa zifuatwe sio kisa eti tajiri na mfanyabiashara.

Inawezekana mzee Akilimali akawa na matatizo mengi sana,lakini pale anapotetea ukweli wa kitu tuweke unazi wetu pembeni.

Tunamhukumu huyu mzee kulingana na hali yake ya kimaisha tu,lakini ana maono. Ulijiuliza siku zote bwana Yusuph alikuwa wapi mpaka asikie uchaguzi umeitishwa ndio aandike barua ya kurudi uongozini?
 
Mimi nimeelewa swali moja, kwa nini Manji yeye binafsi yuko kimya?

Uchaguzi umetangazwa, kama anahitaji uongozi kwa nini asichukue fomu akagombea?

Anyway, mimi kama mpinzani napenda mwendelee kulumbana hivyo hivyo.
Umeambiwa Manji ni mgonjwa asijihusishe na chochote mpaka disemba15 hata biashara zake hashuguliki nazo,bi hindu atawashikia akili mpaka lini nyie mbumbumbu?
 
Umeambiwa Manji ni mgonjwa asijihusishe na chochote mpaka disemba15 hata biashara zake hashuguliki nazo,bi hindu atawashikia akili mpaka lini nyie mbumbumbu?

Tumeshikwaje akili?

Mkuu wewe uko upande gani, Manji Mwenyekiti au uchaguzi wa Mwenyekiti ufanyike?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom