Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,114
Sijawa Bakari (30) mkazi wa kijiji cha Nangumbu, Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi, ameuawa kikatili kwa kukatwa Koromeo na watu wanaosadikika kuwa ni raia wenye hasira kali baada ya kumtuhumu kuwa ni mwizi wa mazao ya wakulima mashambani.
---
Sijawa Bakari (30) mkazi wa kijiji cha Nangumbu, Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi, ameuawa kikatili kwa kukatwa Koromeo na watu wanaosadikika kuwa ni raia wenye hasira kali baada ya kumtuhumu kuwa ni mwizi wa mazao ya wakulima mashambani
Inaelezwa kwamba, kijana Sijawa alikuwa na Tabia ya wizi ambapo ni siku chache zimepita tangu atoke jela baada ya kutumikia kifungo kwa wizi wa korosho mashambani, Sijawa amerudi kutoka jela Mwaka huu mwezi wa 5.
Kutokana na zao la ufuta kuongezeka bei hadi shilingi elfu 4 kwa kilo, wezi wanaohujumu mazao ya wakulima shambani wamekithiri jambo ambalo linasababisha kuwepo kwa matukio mengi ya wizi na mauwaji katika msimu huu.
Wananchi wanasimulia kwamba, walifahamu mienendo ya kijana huyo na kuamua kumfuata hadi nyumbani kwake ambapo walimkuta na shehena ya ufuta, licha ya yeye kutokuwa na shamba lolote.
Wananchi wanasema kwamba, kijana huyo alikuwa akivamia mashambani na kuiba masuke ya ufuta na baadaye kwenda nayo nyumbani ambapo alikamatwa akiwa anakafua ufuta huo (kutoa ufuta kwenye masuke yake).
---
Inaelezwa kwamba, kijana Sijawa alikuwa na Tabia ya wizi ambapo ni siku chache zimepita tangu atoke jela baada ya kutumikia kifungo kwa wizi wa korosho mashambani, Sijawa amerudi kutoka jela Mwaka huu mwezi wa 5.
Kutokana na zao la ufuta kuongezeka bei hadi shilingi elfu 4 kwa kilo, wezi wanaohujumu mazao ya wakulima shambani wamekithiri jambo ambalo linasababisha kuwepo kwa matukio mengi ya wizi na mauwaji katika msimu huu.
Wananchi wanasimulia kwamba, walifahamu mienendo ya kijana huyo na kuamua kumfuata hadi nyumbani kwake ambapo walimkuta na shehena ya ufuta, licha ya yeye kutokuwa na shamba lolote.
Wananchi wanasema kwamba, kijana huyo alikuwa akivamia mashambani na kuiba masuke ya ufuta na baadaye kwenda nayo nyumbani ambapo alikamatwa akiwa anakafua ufuta huo (kutoa ufuta kwenye masuke yake).