carmel
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 2,836
- 262
Bwana Yesu asifiwe,
Kwa kweli, Babu wa Loliondo na ndoto zake na dawa yake hakuna utukufu wowote anaopata Mungu aliye hai ambaye alijifunua kupitia neno lake Yesu Kristo. Kwa hiyo, watumishi wa Mungu kama Kakobe, Mwingira na wengine kupinga ni sahihi tu wala hawana kosa. Tatizo ni kwamba watu wamezama katika udunia na kusahau kabisa maisha ya utakatifu ndiyo maana wanatafuta ufumbuzi laini kwa matatizo magumu kitu ambacho hakiwezekani.
Cha kufanya ni kama mtu unaumwa dawa ni kuokoka na kuishi maisha ya utakatifu; kama ukipona sawa na kama usipopona si unakufa na kwenda mbinguni. tusidanganyane hata ukinywa kikombe na kupona mwili je kesho ukifa utakwenda wapi? Na hata kama huumwi ugonjwa wowote kama mimi dawa ni kuishi maisha ya utakatifu wa kweli ndani ya Yesu tu.
Pia naomba tuwe wastaarabu tuache kuwatukana watumishi wa Mungu kwani tutavuna laana. Wao wanafanya kazi yao kwa kuangalia kila jambo kama linapingana na maandiko matakatifu ya biblia lazima walipinge tu kwani linatoka kwa yule mwovu.
Mwingira, Kakobe na wengine wanaopinga mambo ya Babu wa Loliondo mbarikiwe sana.
Nawasilisha.
Kuna kitu sijaelewa, watu humu mnapinga nini? kwamba dawa ya babu inatibu v/s haitibu?, au whether babu ni mtumishi wa Mungu v/s mtumishi wa shetani? watu wanachohitaji ni kupona, mbona hamuwapingi madaktari wanaotengeneza dawa kila siku? na zenyewe si zinatoka kwenye mitishamba? as long as mtu anamjua anayemuabudu mi sioni shida iko wapi, maana akipona siku zote sifa na utukufu atarudisha kwa Mungu alie hai, so long as hata Ambikile mwenyewe kakiri kwa jina la Yesu kuwa anatibu kwa jina hilo, na anamtumikia Mungu alie hai, hiyo inatosha kwa muumini wa kawaida hana hatia, msim underestimate Mungu kwa uelewa wenu wa kibinadamu. Pingeni na dawa za hospitali kwanza kwa spidi hii hii.