chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,696
- 22,729
Siku ya Jumatano mwili utasafirishwa kupelekwa Moshi Machame, ibada ya mazishi ni siku ya Alhamis wilayani humo kanisa la Kisereni (KKKT)- Mwanasheria wa familia, Michael Ngalo.
=====
Mwili wa marehemu wa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi utawasili jumatatu mchana Mei 6, 2019 jijini Dar es salaam kutoka Dubai na kupelekwa kuhifadhiwa katika hospitali ya jeshi ya Lugalo .
Mwanasheria wa familia, Michael Ngalo amesema mwili wa mfanyabiashara huyo maarufu nchini Tanzania utarejea jumatatu na kuagwa siku ya Jumanne katika viwanja vya Karimjee.
Siku ya Jumatano Mei 8, 2019 mwili utasafirishwa kwenda Machame mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko yatakayofanyika siku ya Alhamisi Mei 9, 2019.
"Baada ya mwili kuwasili Machame ibada ya mazishi itafanyika katika Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania la Kisereni,"
UPDATE
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi umewasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar
Msafara wa kuelekea hospitali ya Lugalo kuhifadhiwa utaanza majira ya saa 9:45 alasiri na utapita Tazara-Buguruni-Ilala-Kigogo-Magomeni-Kinondoni-Morocco-Bagamoyo Road-Sayansi-Mwenge na kisha Lugalo
=====
Mwili wa marehemu wa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi utawasili jumatatu mchana Mei 6, 2019 jijini Dar es salaam kutoka Dubai na kupelekwa kuhifadhiwa katika hospitali ya jeshi ya Lugalo .
Mwanasheria wa familia, Michael Ngalo amesema mwili wa mfanyabiashara huyo maarufu nchini Tanzania utarejea jumatatu na kuagwa siku ya Jumanne katika viwanja vya Karimjee.
Siku ya Jumatano Mei 8, 2019 mwili utasafirishwa kwenda Machame mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko yatakayofanyika siku ya Alhamisi Mei 9, 2019.
"Baada ya mwili kuwasili Machame ibada ya mazishi itafanyika katika Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania la Kisereni,"
UPDATE
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi umewasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar
Msafara wa kuelekea hospitali ya Lugalo kuhifadhiwa utaanza majira ya saa 9:45 alasiri na utapita Tazara-Buguruni-Ilala-Kigogo-Magomeni-Kinondoni-Morocco-Bagamoyo Road-Sayansi-Mwenge na kisha Lugalo