Mwili kuchoka na usingizi usioisha

Natumai muwazima wana jf,nimekuwa na tatizo ambalo sielewi linasababishwa na nn,nasikia uchovu sana kiasi cha kuhisi kama naumwa na tena muda mwingi nakuwa najisikia kulala,naomba msaada madaktari.

Kuna mambo mengi saana yanayoweza kusababisha uchovu. Cha msingi, mtafute tabibu afanye upembuzi yakinifu. Baadhi tu ya matatizo yanayoweza kukusababishia ujisikie uchovu ni mfano anemia(upungufu wa damu), hypothyroidism(upungufu wa madini ya thyroid), Obstructive sleep apnea(kutopumua vizuri unapokuwa usingizini), infections (malaria, minyoo nk), depression, chronic fatigue syndrome, hiv, malignancy, na kadhalika.
Ni vigumu saana kwa kupata majibu bila ya kumhoji mgonjwa na kufanya vipimo ili kufahamu hasa ni nini kinachoeeza kuwa kinasababisha uchovu.
Nakushauri umtafute tabibu akusaidie kufanya upembuzi huo yakinifu.
 
Natumai muwazima wana jf,nimekuwa na tatizo ambalo sielewi linasababishwa na nn,nasikia uchovu sana kiasi cha kuhisi kama naumwa na tena muda mwingi nakuwa najisikia kulala,naomba msaada madaktari.
Tumia Dawa hii itaweza kukusaidia inshallah.

Udhaifu kwa Ujumla

Utachukua unga wa habat soda kiasi cha kikombe kimoja, Unga wa uwatu kikombe kimoja na ambari (ambergris) ilioyeyushwa kiasi cha kijiko kidogo, vyote atavichanganya katika chombo chenye asali iwe kama jamu; halafu awe akila kama jamu kila siku na wakati wowote apendao lakini kwa mkate wa ngano asili
 
Habari zenu umu ndani wengi tuna changia mada nakupoteza mda lakini hatujui sababu maalum za hilo tatizo ndugu yangu jieleke hospitali kapime vipimo aina zote amna jibu zaidi yailo
 
Angalia uzito wako, kama una unene wa kupita kiasi (obese) inawezekana unapolala muscles kwenye koo lako zinaziba air ways na kufanya mwili usipate oxygen ya kutosha.
Kama unamatatizo kwenye mapafu (mengine yanasababishwa na uvutaji sigari wa muda mrefu) mapafu yanapunguza uwezo wa kutoa carbon dioxide iliyoko mwilini. Carbon dioxide ikibaki mwilini inakufanya ujisikie kuchoka muda wote, mara nyingi huwezi kuangalia TV kwa lisaa zima bila kusinzia. Kama unaendesha gari unaweza kusinzia barabarani hivyo kusababisha ajali pia kuhatarisha maisha yako.
 
Utatoaje ushauri wa tiba kabla haujafahamu uchovu unasababishwa na nini? Au ndiyo haya matibabu ya kubahatisha? Nashindwa kuelewa.
Mkuu mi mwenyewe nimesoma prescription zao nikaogopa kidogo. Ni kama washajua tatizo na wameenda moja kwa moja kwenye tiba wakati symptoms sio ugonjwa in most cases. Hatari sana. Anyway....
 
Kuna hatari ya mgonjwa kuzidiwa kama hataenda hospital kujua kiini cha tatizo manake madaktari wengi washatoa tiba zao kabla ya kujua what's the problem
 
mawazo ni tatizo sugu!
kua na amani ndio tiba mbadala!
jitahidi kuchangamka.

maana hata mimi huwa nakumbwa na hio hali mara kwa mara..
hata kula sijisikii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom