Djumbe
Member
- Apr 8, 2011
- 39
- 62
Majigambo na vitisho vingi vya naibu katibu mkuu wa CCM na mbunge wa Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba yalidhihirika kuwa ni kelele za chura baada ya wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye mikutano ya CHADEMA iliyofanyika wiki iliyopita katika vijiji mbalimbali jimboni hapo, Wananchi walidhihirisha kumchoka Mbunge huyo mwenye vituko vya kisiasa visivyowasaidia waliomchagua kwa kulalamikia utendaji wake mbovu jimboni huku wakiorodhesha kero ndogo ndogo alizoshindwa kuzitekeleza ukiacha zile kubwa ambazo wananchi wanafikiri ni Miujiza tuu ndio inyoweza kuwaokoa kama wataendelea kuwa chini ya utawala wa CCM.
Mwigulu kwa kutaka kuivuruga mikutano hiyo alianza kwa kuwatishia wananchi wasihudhurie mikutano na akaanzisha Ligi ya mpira wa miguu kila tulipokwenda, lakini vijana waliendelea kuja kwenye mikutano yetu na wale ambao walichukua kadi za CHADEMA aliwatoa kwenye Ligi hiyo kama alivyofanya katika kijiji cha Ndulungu.
Nia yake ya kutufanyia fujo ilishindakana kutokana na mikutano yetu yote kupewa ulinzi wa askari Polisi wasiopungua 10, na hivyo wananchi walipata ujasiri wa kuhudhuria na kueleza wazi kero zao.
Katika kijiji cha Tyegelo ambapo kuna umaskini mkubwa sana wa kipato,wananchi walilalamikia kwa uchungu hatua ya Mbunge huyo kutumia Million 13 kuilipa timu ya Simba kucheza mechi Kiomboi siku ya ziara ya Dr Slaa ili kuvuruga mkutano huo ,wakati Dispensary yao iliyoanza kujengwa miaka 3 iliyopita imeshindikana kukamilika kwa kukosekana Sh million 5 tu,huku yeye akiwalazimisha wananchi hao kuchangishana kumalizia ujenzi huo.
Wakati yeye anajitapa kwenye mitandao ya kijamii kwamba amejenga miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara, vijiji vingi jimboni hapo havifikiki kwa gari kikiwepo kijiji cha Makunda (kwao na Mwigulu) pamoja na kijiji alikozaliwa Dr Kitila Mkumbo cha Mgela, huku fedha za mfuko wa maendeleo ya Jimbo anazopewa kila baada ya miezi 3 hazijulikani
zinakotokomea na hivyo kusababisha baadhi ya wasaidizi wake wa karibu kama Emmanuel Edger Ntundu kujitoa kwenye chama hicho na kuhamia CHADEMA kukwepa ufisadi huo.
Pamoja na kuwa ziara yetu tulichagua vijiji na Kata ambazo hazikuwahi kufikiwa na CHADEMA kabla, wananchi walikiri wazi kuwa walifanya makosa kumchagua Mbunge huyo na kwamba hawako tayari kurudia makosa hayo tena 2015, na nilichojifunza mimi ni kwamba wanyiramba huwa hawarudii makosa pale wanapojifunza na kujua ukweli na ndio maana tangu uhuru ni mbunge 1 tu (Nalaila Kiula ) ndiye aliyeweza kulishikilia Jimbo hilo kwa awamu zaidi ya 1.
Tutaendelea kwenda Iramba magharibi kuwaelimisha wananchi ili 2015 ikifika wafanye maamuzi wakiwa na ufahamu wa kutosha na hivyo kutochagua AIBU kama walivyofanya 2010,
na ushauri wangu kwa Mwigulu ni kwamba aanze kufungasha virago vyake badala ya kupoteza muda kwa kutengeneza propaganda dhidi ya CHADEMA ambazo kimsingi zinazidi kuiua CCM na kuipaisha CHADEMA na ndio maana hata hali yake ya kisiasa ndani ya CCM sasa ni mbaya maana hawamhitaji tena na hapo alipo amekalia kuti KAVU.
Mimi nimewasilisha, karibuni mnaojua kubisha maana mnakomaa utafikiri nyie ndo mlikuwepo!!!
Mwigulu kwa kutaka kuivuruga mikutano hiyo alianza kwa kuwatishia wananchi wasihudhurie mikutano na akaanzisha Ligi ya mpira wa miguu kila tulipokwenda, lakini vijana waliendelea kuja kwenye mikutano yetu na wale ambao walichukua kadi za CHADEMA aliwatoa kwenye Ligi hiyo kama alivyofanya katika kijiji cha Ndulungu.
Nia yake ya kutufanyia fujo ilishindakana kutokana na mikutano yetu yote kupewa ulinzi wa askari Polisi wasiopungua 10, na hivyo wananchi walipata ujasiri wa kuhudhuria na kueleza wazi kero zao.
Katika kijiji cha Tyegelo ambapo kuna umaskini mkubwa sana wa kipato,wananchi walilalamikia kwa uchungu hatua ya Mbunge huyo kutumia Million 13 kuilipa timu ya Simba kucheza mechi Kiomboi siku ya ziara ya Dr Slaa ili kuvuruga mkutano huo ,wakati Dispensary yao iliyoanza kujengwa miaka 3 iliyopita imeshindikana kukamilika kwa kukosekana Sh million 5 tu,huku yeye akiwalazimisha wananchi hao kuchangishana kumalizia ujenzi huo.
Wakati yeye anajitapa kwenye mitandao ya kijamii kwamba amejenga miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara, vijiji vingi jimboni hapo havifikiki kwa gari kikiwepo kijiji cha Makunda (kwao na Mwigulu) pamoja na kijiji alikozaliwa Dr Kitila Mkumbo cha Mgela, huku fedha za mfuko wa maendeleo ya Jimbo anazopewa kila baada ya miezi 3 hazijulikani
zinakotokomea na hivyo kusababisha baadhi ya wasaidizi wake wa karibu kama Emmanuel Edger Ntundu kujitoa kwenye chama hicho na kuhamia CHADEMA kukwepa ufisadi huo.Pamoja na kuwa ziara yetu tulichagua vijiji na Kata ambazo hazikuwahi kufikiwa na CHADEMA kabla, wananchi walikiri wazi kuwa walifanya makosa kumchagua Mbunge huyo na kwamba hawako tayari kurudia makosa hayo tena 2015, na nilichojifunza mimi ni kwamba wanyiramba huwa hawarudii makosa pale wanapojifunza na kujua ukweli na ndio maana tangu uhuru ni mbunge 1 tu (Nalaila Kiula ) ndiye aliyeweza kulishikilia Jimbo hilo kwa awamu zaidi ya 1.
Tutaendelea kwenda Iramba magharibi kuwaelimisha wananchi ili 2015 ikifika wafanye maamuzi wakiwa na ufahamu wa kutosha na hivyo kutochagua AIBU kama walivyofanya 2010,
na ushauri wangu kwa Mwigulu ni kwamba aanze kufungasha virago vyake badala ya kupoteza muda kwa kutengeneza propaganda dhidi ya CHADEMA ambazo kimsingi zinazidi kuiua CCM na kuipaisha CHADEMA na ndio maana hata hali yake ya kisiasa ndani ya CCM sasa ni mbaya maana hawamhitaji tena na hapo alipo amekalia kuti KAVU.
Mimi nimewasilisha, karibuni mnaojua kubisha maana mnakomaa utafikiri nyie ndo mlikuwepo!!!