Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Nasra Mohamed, amewataka vijana kuepuka kujiingiza katika wito wa kufanya maandamano yaliyopangwa kufanyika tarehe 9 Desemba 2025, akisema kuwa maandamano hayo hayana msingi na yanachochewa na watu wenye malengo yao binafsi.
Akizungumza leo, Nasra amesema baadhi ya vijana wanaojiandaa kushiriki maandamano hayo ni “vijana wanaolaghaiwa” na watu wanaotumia hisia zao kuleta vurugu na usumbufu katika jamii, jambo ambalo sio sahihi kulieleza kama maandamano halisi yenye hoja na misingi ya kikatiba.
“Maandamano yana misingi yake. Haya tunayoyaona yakipangwa mitandaoni hayana uhalisia wa madai ya msingi. Vijana wasitumiwe kama chombo cha kuvuruga amani ya nchi,” amesema Nasra.
Akizungumza leo, Nasra amesema baadhi ya vijana wanaojiandaa kushiriki maandamano hayo ni “vijana wanaolaghaiwa” na watu wanaotumia hisia zao kuleta vurugu na usumbufu katika jamii, jambo ambalo sio sahihi kulieleza kama maandamano halisi yenye hoja na misingi ya kikatiba.
“Maandamano yana misingi yake. Haya tunayoyaona yakipangwa mitandaoni hayana uhalisia wa madai ya msingi. Vijana wasitumiwe kama chombo cha kuvuruga amani ya nchi,” amesema Nasra.