Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,615
- 40,162
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu kimepata pigo kufuatia kifo cha Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoani humo, Mariam Manyangu, aliyefariki dunia leo Jumamosi Machi 21, 2026.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa CCM Mkoa wa Simiyu, Lumen Ngunda, marehemu amefariki dunia akiwa jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa chama kimepokea kwa masikitiko makubwa kifo hicho, kikimtaja Manyangu kuwa kiongozi aliyetoa mchango mkubwa katika kuimarisha umoja wa wanawake ndani ya chama na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii mkoani humo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa CCM Mkoa wa Simiyu, Lumen Ngunda, marehemu amefariki dunia akiwa jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa chama kimepokea kwa masikitiko makubwa kifo hicho, kikimtaja Manyangu kuwa kiongozi aliyetoa mchango mkubwa katika kuimarisha umoja wa wanawake ndani ya chama na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii mkoani humo.