Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,608
Siku mbili kabla ya Uchaguzi nchini Uganda, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini humo Simon Byabakama amefichua kwamba amepokea vitisho juu ya kutangaza mshindi katika uchaguzi huo. Byabakama alikuwa akizungumza na BBC mara baada ya kumaliza kutoa taarifa na vielelezo vingine juu ya zoezi la kupiga kura. Wapiga kura zaidi ya milioni 20 nchini Uganda wanatarajiwa kwenda kuchagua Rais na wabunge wao siku ya Alhamis tarehe 15 Januari.