Mwenyekiti Tume ya Uchaguzi atungiwe sheria maalum

emalau

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
2,775
3,100
Nimekuwa nikitafakari juu ya utendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi toka tuingie mfumo wa vyama vingi kwa kweli hauridhishi na unatia shaka impartiality yake. Kwa utaratibu tulio nao sasa rais ndo anateua mwenyekiti na anaweza kumfukuza kazi muda wowote. Jambo hili siyo tu linamfanya mkuu wa tume kuwa na uwoga wa kukosa kazi bali pia unamfanya asiwe mtu wa kuamaminika pamoja na timu yake na vyama shindani.

Nilikuwa napendekeza rais abaki na haki ya kumteua lakini lazima kwanza ajadiliwe na bunge ahojiwe bunge likimpitisha ndo apewe kazi. Akishapewa kazi baada ya kumwapisha rais asiwe na nguvu ya kumwondoa isipokuwa bunge pekee au kamati maalum ya majaji wa mahakama ya rufaa baada ya kujiridhisha kwamba amekiuka maadili ya utendaji kazi wake.

Nawasilisha wana JF
 
Ulianza vizuri sana ila ukajikanyaga kwenye uteuzi. Nashauri kuwa, aandike barua ya kuomba hiyo nafasi, ndipo akutanishwe na wagombea nafasi hiyo wengine. Sifa nyingine ni kuwa, asiwe na uhusiano wowote na chama chenye wabunge wengi bungeni ndipo apelekwe huko kupitishwa.
Hata nafasi ya Jaji Mkuu. Asiteuliwe bali aombe nafasi hiyo na ijadiliwe na bunge. Pia asiwe na fungamano lolote na siasa
 
Ulianza vizuri sana ila ukajikanyaga kwenye uteuzi. Nashauri kuwa, aandike barua ya kuomba hiyo nafasi, ndipo akutanishwe na wagombea nafasi hiyo wengine. Sifa nyingine ni kuwa, asiwe na uhusiano wowote na chama chenye wabunge wengi bungeni ndipo apelekwe huko kupitishwa.
Hata nafasi ya Jaji Mkuu. Asiteuliwe bali aombe nafasi hiyo na ijadiliwe na bunge. Pia asiwe na fungamano lolote na siasa

Naunga mkono pendekezo lako, mawazo kama haya ndo yatatuwezesha kujenga taasisi imara kwa manufaa yetu na vizazi vyetu vijavyo.
 
Awe kama CAG nashangaa CAG wamemlinda

Na kama umefuatilia hivi karibuni CAG akiongea unamwona anaongea akiwa ameweka taaluma mbele na bila woga wowote wa kutumbuliwa na hilo ndo tunataka kwa mwenyekiti wa tume
 
Wazo swafi, ila kwa hiari tu watu hawa kamwe hawawezi hata kujaribu kufikiri kubadili sheria hii, yaani mtu ukanunue kitanzi cha kumnyongea !!!weeee!!!
 
Naunga mkono pendekezo lako, mawazo kama haya ndo yatatuwezesha kujenga taasisi imara kwa manufaa yetu na vizazi vyetu vijavyo.
hii inaweza kuitoa hii nchi kutoka dunia ya tatu kuwa dunia ya pili, wakikubali nitaarifu mkuu.
 
Atapitishwa vio na bunge wakat kwa sehemu Bunge linaongoza kwa wabunge wa chama tawala..

kwa wazo hilo, tutakuwa tunaendelea ku circle mlemle
 
Nimekuwa nikitafakari juu ya utendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi toka tuingie mfumo wa vyama vingi kwa kweli hauridhishi na unatia shaka impartiality yake. Kwa utaratibu tulio nao sasa rais ndo anateua mwenyekiti na anaweza kumfukuza kazi muda wowote. Jambo hili siyo tu linamfanya mkuu wa tume kuwa na uwoga wa kukosa kazi bali pia unamfanya asiwe mtu wa kuamaminika pamoja na timu yake na vyama shindani.

Nilikuwa napendekeza rais abaki na haki ya kumteua lakini lazima kwanza ajadiliwe na bunge ahojiwe bunge likimpitisha ndo apewe kazi. Akishapewa kazi baada ya kumwapisha rais asiwe na nguvu ya kumwondoa isipokuwa bunge pekee au kamati maalum ya majaji wa mahakama ya rufaa baada ya kujiridhisha kwamba amekiuka maadili ya utendaji kazi wake.

Nawasilisha wana JF
Mzee sikiya huwezi kuchaguliwa kuiongoza tume ya uchaguzi kama sio kada wa ccm tena mwenye rikodi nzuri kwenye chama kwahivyo hilo pendekezo lako halitekelezeki
 
Na kama umefuatilia hivi karibuni CAG akiongea unamwona anaongea akiwa ameweka taaluma mbele na bila woga wowote wa kutumbuliwa na hilo ndo tunataka kwa mwenyekiti wa tume
Its time na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kulindwa
 
Mzee sikiya huwezi kuchaguliwa kuiongoza tume ya uchaguzi kama sio kada wa ccm tena mwenye rikodi nzuri kwenye chama kwahivyo hilo pendekezo lako halitekelezeki

Wachangiaji wengine hapo juu wametoa pendekezo zuri zaidi kwamba hiyo kazi iombwe na wafanyiwe usaili
 
Back
Top Bottom