Mwenyekiti Halmashauri ya Uyui auwawa

Haya ndio mauaji ya siku hizi hapa Tabora, ni mambo ya kisiasa na wanapopingana juu ya miradi hewa ndipo DHAHMA kama hizi hujiri kwao na huwa ni risasi tu. No dialogue, can't negotiate
 
WanaJF,
Usiku wa kuamkia leo mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Uyui mkoani Tabora (Mh. Mashaka) ameuawa kikatili kwa risasi akiwa nyumbani kwake eneo la Ipuli nje kidogo ya mji. Ameuwawa akiwa na familia yake ambapo inasemekana ni wezi, iko hivi...
  • Nyumba yake imepigwa jiwe kubwa mlangoni maarufu kama 'fatuma' na kuweza kuingia ndani.
  • Amemiminiwa risasi 7 mkono wa kulia.
  • Risasi 8 upande wa mkono wa kushoto.
  • Amekatwa panga utosini na fuvu kuchanika.
  • Alikuwa na familia yake nyumbani.
  • Mazishi yatafanyika siku ya jumapili katika kijiji cha Utyatya-Sikonge.
  • Alikuwa ni diwani wa kata ya Iyenze.
  • Ameuwawa kati ya saa saba usiku na saa nane usiku.
  • Ameuwawa akiwa ndie mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Uyui.
  • Taarifa za kiintelijensia bado hazijatolewa na chombo kinachohusika.
  • Wauaji nao bado hawajapatikana.
Hili ni tukio baya kabisa likiwa ni la pili ndani ya miaka 5 kuhusisha madiwani/wenyeviti wa Uyui Districts na huwa hakuna taarifa kubaini wauaji zaidi ya kuzungushwa.
Mwaka 2008 tarehe 19 saa tatu usiku aliuawa diwani ambaye alikuwa ni babu yangu aitwae Salum Said Mgeleka wa kata ya Ibiri ambapo hadi tuongeavyo hakuna taarifa zozote za kiintelijensia zilizobaini wauaji zaidi ya porojo. Mzee Mgeleka aliuawa kwa kupigwa risasi tatu pajani na kutelekezwa jirani ya mtaro ambapo bleeding ilisababisha kifo chake. Huyu pia alikuwa jirani kabisa na nyumbani kwake. Inaogofya.

MY TAKE: Tabora inatisha sana kwa mauaji ya aina hii, serikali zote kuu zipo lakini sijui tatizo ni nini. Kuna harufu mbaya sana. Wale wanaowania nafasi fulani za Tabora wawe chonjo na aina hii ya mauaji.

Source: Madiwani 2 wa Uyui, kunijuza kwa kunipigia simu.


KAMA NI MAJABAZI WAMEIBA NINI? cha kujiuliza zaidi kwanini wamiminie risasi zote hizo mwenyewe pamoja na mapanga? je hakuna mwanafamilia yeyote aliyejeruhiwa hapo? ikiwa majibu ya maswali hayo ni SIYO basi ujue marehemu kuna kitu alifanya hivyo ilikuwa ni kulipiza kisasi.
 
Hivi hii nchi inaelekea wapi. Polisi imegeuka Green gard ya CCM. Kama issue haina interest na wakubwa hakuna kinachotendeka. Hivi kwa nini IGP hasiondolewe
 
Aisee!RIP Diwani na poleni sana wanafamilia...Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu muweze kustahimili msiba huu mzito.
 
WanaJF,
Usiku wa kuamkia leo mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Uyui mkoani Tabora (Mh. Mashaka) ameuawa kikatili kwa risasi akiwa nyumbani kwake eneo la Ipuli nje kidogo ya mji. Ameuwawa akiwa na familia yake ambapo inasemekana ni wezi, iko hivi...
  • Nyumba yake imepigwa jiwe kubwa mlangoni maarufu kama 'fatuma' na kuweza kuingia ndani.
  • Amemiminiwa risasi 7 mkono wa kulia.
  • Risasi 8 upande wa mkono wa kushoto.
  • Amekatwa panga utosini na fuvu kuchanika.
  • Alikuwa na familia yake nyumbani.
  • Mazishi yatafanyika siku ya jumapili katika kijiji cha Utyatya-Sikonge.
  • Alikuwa ni diwani wa kata ya Iyenze.
  • Ameuwawa kati ya saa saba usiku na saa nane usiku.
  • Ameuwawa akiwa ndie mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Uyui.
  • Taarifa za kiintelijensia bado hazijatolewa na chombo kinachohusika.
  • Wauaji nao bado hawajapatikana.
Hili ni tukio baya kabisa likiwa ni la pili ndani ya miaka 5 kuhusisha madiwani/wenyeviti wa Uyui Districts na huwa hakuna taarifa kubaini wauaji zaidi ya kuzungushwa.
Mwaka 2008 tarehe 19 saa tatu usiku aliuawa diwani ambaye alikuwa ni babu yangu aitwae Salum Said Mgeleka wa kata ya Ibiri ambapo hadi tuongeavyo hakuna taarifa zozote za kiintelijensia zilizobaini wauaji zaidi ya porojo. Mzee Mgeleka aliuawa kwa kupigwa risasi tatu pajani na kutelekezwa jirani ya mtaro ambapo bleeding ilisababisha kifo chake. Huyu pia alikuwa jirani kabisa na nyumbani kwake. Inaogofya.

MY TAKE: Tabora inatisha sana kwa mauaji ya aina hii, serikali zote kuu zipo lakini sijui tatizo ni nini. Kuna harufu mbaya sana. Wale wanaowania nafasi fulani za Tabora wawe chonjo na aina hii ya mauaji.

Source: Madiwani 2 wa Uyui, kunijuza kwa kunipigia simu.

Poleni sana mkuu Yousuph .M.
 
Ningependa kujua Kama Aden Rage alichukuliwa hatua gani kupanda jukwaani Igunga na silaha
 
Poleni wana IGUNGA-ndivyo serikal ya magamba ilivyo kila mmoja analipo kisasa.maana serikal haijielew iko wapi na inafanyanini.
 
nakumbuka kuna diwani wa tabora,kanyenye alivyolambwa risasi kwake,siku moja kabla ya kutoa ushahidi mahakamani dhidi ya mkurungenzi (mama khalfan na genge lake wakina munde tambwe)walivyokuwa wakitafuna pesa za halmashauri.isije ikawa ndio yaliomkuta huyo diwani.tabora huwa ni shamba la bibi.ni sehemu pa kuchumia mihela.


Huyu mama sijui dada sasa hivi si wamempa na ubunge wa viti maalumu?Yaani ndani ya magamba kuna umafia wa kutisha aisee!!
 
Mimi siku hizi huwa siwalaumu viongozi lahasha ila nawalaumu wananchi. Kwanini tusiwatupe nje hawa magamba? Tabora hakuna upinzani kwa nini? Tunalalamika halafu uchaguzi ukifika mtu anaridhika na pipi! Maamuzi ya kuondoa upuuzi wote huu na uushenzi huo wa kuuana yako mikononi mwa mwanachi. Sio kweli kwamba hawajulikani wauaji ila mijitu mingine inaficha tu uharamia kama huu. Serikali yetu imisha kuwa ya kishenzi sana, tunahitaji uongozi wenye dira na dhamira ya kumlinda mwanachi. Je tutafika kweli? Labda miaka 100 ijayo maana kwa akili hizi tulizonazo sasa hivi haitawezekana. Unamuua mwenzio kisa uongozi? Hao wanajulikana sana wanajf
 
Mimi siku hizi huwa siwalaumu viongozi lahasha ila nawalaumu wananchi. Kwanini tusiwatupe nje hawa magamba? Tabora hakuna upinzani kwa nini? Tunalalamika halafu uchaguzi ukifika mtu anaridhika na pipi! Maamuzi ya kuondoa upuuzi wote huu na uushenzi huo wa kuuana yako mikononi mwa mwanachi. Sio kweli kwamba hawajulikani wauaji ila mijitu mingine inaficha tu uharamia kama huu. Serikali yetu imisha kuwa ya kishenzi sana, tunahitaji uongozi wenye dira na dhamira ya kumlinda mwanachi. Je tutafika kweli? Labda miaka 100 ijayo maana kwa akili hizi tulizonazo sasa hivi haitawezekana. Unamuua mwenzio kisa uongozi? Hao wanajulikana sana wanajf


Mkuu kwanza naoma ku-declare interest mapema kabisa,mimi ni mnyamwezi wa Tabora na nimezaliwa na nimekulia Tabora hivyo katika watu wanaoifahamu mboka japo kwa uchache na mimi ni mmoja wapo!Si kweli kwamba Tabora hakuna upinzani isipokuwa wapinzani hawapo serious na mkoa wa Tabora,wanatabora tupo tayari kwa mabadiliko lakini mara zote watu wanaogombea kwa upinzani either wanakuwa hawapo serious or hawana mvuto kisiasa labda kutokana na elimu yao au other potentialities kwa jamii!Kudhihirisha hilo mbunge wa kwanza wa jimbo la Urambo Mashariki(Kwa Sitta) tangu mfumo wa vyama vingi uanze alikuwa anaitwa Dr Jacob Msina kupitia chama cha NCCR-Mageuzi.Tatizo kubwa wanyamwezi wengi ambao ni potential hawapo tayari kurudi nyumbani kuusaidia mkoa wao!!Mfano kinyang'anyiro cha ubunge 2010 Rage almost alikuwa peke yake,CUF waliweka mtu asiyepotential hata kidogo,CHADEMA ingeweza kulichukua jimbo maana mgombea wao alikuwa ni msomi (Alishawahi kuwa jaji kipindi cha Mwalimu)na ni mwanasheria aliyebobea lakini sijui alilazimishwa kugombea maana kampeni alifanya mara moja tu na nasikia hata kipindi cha kupiga kura alikuwa nje ya nchi!!
 
Back
Top Bottom