Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 980
- 3,646
Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, ameeleza kuwa mchakato wa uandikishaji wapigakura wapya visiwani Zanzibar unakabiliwa na changamoto kubwa, hasa kutokana na matumizi ya nguvu na ushawishi wa vyombo vya dola. Kwa mujibu wake, hali hiyo inaashiria kwamba watawala hawana dhamira ya dhati ya kuhakikisha haki, licha ya maneno yao ya mara kwa mara yanayohamasisha amani.
Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa chama uliofanyika katika Ukumbi wa Jimbo la Konde, wilaya ya Micheweni, Othman – ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar – alisema mwenendo wa sasa unaonyesha wazi kuwa mazingira ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 yanatengenezwa kwa njia isiyo ya haki, kwa lengo la kuwakandamiza wananchi kupitia matumizi ya vyombo vya dola.
Licha ya hali hiyo, alisema wanachama na viongozi wa ACT-Wazalendo wameendelea kuonyesha mshikamano na kujitolea kwa ajili ya kusimamia haki. Aliwasisitiza waendelee kushikamana na kutokata tamaa.
Aliwataka wanachama kudumisha nidhamu na mshikamano, hasa wakati huu wa maandalizi ya uchaguzi, akisisitiza kuwa ushindi unapatikana kupitia umoja na utii kwa kanuni na taratibu za chama. Aidha, alitoa onyo kwa wanachama na viongozi kutokubali kurubuniwa na maneno matamu kutoka kwa baadhi ya viongozi wa serikali, akibainisha kuwa:
Othman alisisitiza kuwa huu si wakati wa kuwa watazamaji, bali ni muda wa kuchukua hatua katika kudai haki, hasa kwa wale waliokosa fursa ya kuandikishwa kuwa wapigakura.
Katika mazungumzo hayo, alifichua kuwa viongozi wa upinzani walijaribu njia ya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujenga mazingira ya amani ya kweli. Hata hivyo, alisema juhudi hizo hazikupokelewa kwa nia njema.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Zanzibar, Omar Ali Shehe, alisema kuwa hujuma zinazofanywa na baadhi ya vyombo vya dola zimesababisha zaidi ya watu 770 kushindwa kujiandikisha. Hata hivyo, alibainisha kuwa chama kina mikakati madhubuti kuhakikisha ushindi mkubwa katika uchaguzi ujao licha ya vikwazo hivyo.
Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa chama uliofanyika katika Ukumbi wa Jimbo la Konde, wilaya ya Micheweni, Othman – ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar – alisema mwenendo wa sasa unaonyesha wazi kuwa mazingira ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 yanatengenezwa kwa njia isiyo ya haki, kwa lengo la kuwakandamiza wananchi kupitia matumizi ya vyombo vya dola.
Licha ya hali hiyo, alisema wanachama na viongozi wa ACT-Wazalendo wameendelea kuonyesha mshikamano na kujitolea kwa ajili ya kusimamia haki. Aliwasisitiza waendelee kushikamana na kutokata tamaa.
“Tuna kila sababu ya kujivunia umoja wetu. Hakuna jambo gumu kama kudai haki, lakini tupo karibu kufikia malengo ya kuona Zanzibar yenye mamlaka kamili,” alisema.
Aliwataka wanachama kudumisha nidhamu na mshikamano, hasa wakati huu wa maandalizi ya uchaguzi, akisisitiza kuwa ushindi unapatikana kupitia umoja na utii kwa kanuni na taratibu za chama. Aidha, alitoa onyo kwa wanachama na viongozi kutokubali kurubuniwa na maneno matamu kutoka kwa baadhi ya viongozi wa serikali, akibainisha kuwa:
“Wanaonekana wapole lakini ‘wanaua watu huku wakiwa na tasbihi mkononi.’”
Othman alisisitiza kuwa huu si wakati wa kuwa watazamaji, bali ni muda wa kuchukua hatua katika kudai haki, hasa kwa wale waliokosa fursa ya kuandikishwa kuwa wapigakura.
Katika mazungumzo hayo, alifichua kuwa viongozi wa upinzani walijaribu njia ya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujenga mazingira ya amani ya kweli. Hata hivyo, alisema juhudi hizo hazikupokelewa kwa nia njema.
“Wasidhani hata Polisi wanapenda machafuko. Hata wao wamechoka. Wazanzibari nao wamechoshwa na dhuluma hizi,” alisema kwa kusisitiza, akifananisha hali ya sasa na historia ya ubaguzi wa rangi Afrika Kusini, akionya kuwa mwisho wa ukandamizaji huwa hauna heri.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Zanzibar, Omar Ali Shehe, alisema kuwa hujuma zinazofanywa na baadhi ya vyombo vya dola zimesababisha zaidi ya watu 770 kushindwa kujiandikisha. Hata hivyo, alibainisha kuwa chama kina mikakati madhubuti kuhakikisha ushindi mkubwa katika uchaguzi ujao licha ya vikwazo hivyo.