Mwenye maarifa na utapeli huu

Mwenye maarifa na utapeli huu

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,427
Reaction score
10,749
Habari,
Kuna Bwana mmoja anaitwa Sauli, ni mtu wangu wa karibu. Tumeshughurikia pensheni yake as kastaafu shirika la Posta na kalipwa Milioni 70. Sasa game iko hivi, kuna tapeli mmoja dreva (inasemekana kashamliza mfanya biashara mmoja Tsh 80M na mwingine takribani 50M), kashamuweka king huyu mzee wetu. Huyu dreva anachofanya anasema anawatafutia watu fursa za biashara na anawaunganisha na shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNDP kwa kutafuta watu wenye mitaji watakaofanya biashara za misitu. Huyu dreva anakupa mipango kabambe na anakuunganisha na mapadre, maaskofu, mashehe au wachungaji (hawa huwa ni fake) ambao husema nao wanafanya biashara hizi. Sasa siku ya siku utashangaa hao wachungaji fake wanakuja kwako au mnakutana hotelini huku wamevaa mavazi ya kichungaji mainly Roman Color shirts au nguo za kiustaadhi na wanakupa mipango mizuri ya biashara. Wanahakikisha unakuwa interested na watakuomba uchangie mf gharama ya wao kukaa hoteli, mafuta ya gari n.k (kumbe ndo watapeliwa hivyo).

Sasa mtaendelea kuwa na mawasilino huku wakitumia vifungu vya Biblia/Kurani uwachangie karibu kila huduma. Siku nyingine huchagua msitu wa mbali na kwako na kumuagiza huyo dreva muende ukauone then ushughurikie leseni ya umiliki. Sasa hapo penye leseni utaandaliwa watu wa ardhi/misitu fake na utalipia leseni fake let say ya 25M, utalipia usafiri, gharama za upimaji n.k kumbe msitu wenyewe hauuzwi ni mali ya serikari.

Siku nyingine itapangwa trip ya kupeleka hivyo viambatanisho vya Misitu unayomiliki huko Dar, Arusha, Mwanza, Kampala, Nairobi etc kwenye ofisi ya wawakilishi wa UNDP. Kumbuka kila gharama unalipia wewe, huko sasa ndo unaenda kutapeliwa mpaka ndala, unakuja kustuka pensheni yooote uliyoisotea kwa miaka dahari inaliwa na wasio na uchungu nayo.........

Ndugu yangu,
Utapeli ni taaluma, wizi ni ubunifu makini na hawa watu ni wajanja na hubuni mbinu nyingi sana kuibia watu. Wanaofanya haya wakati mwingine ni watu tunaowafahamu, kwa kujua ama kutojua. Wastaafu wengi wamelizwa kwa njia hizi au nyingine. Muonye ndugu yako, muelekeze ajikite ktk biashara halali, asitafute pesa za haraka haraka. Pesa hutafutwa kwa jasho na si kwa njia za mkato. Pensheni imefarakanisha wastaafu wengi na familia zao kwa kuingia ktk biashara za magumashi zisizo na faida na zilizojaa utapeli. Pole kwa waliolizwa. Mzee huyu tunatafuta namna ya kumuokoa ila ndo hivyo keshalizwa, hivi sasa hata pesa za kununulia wanzuki au mbege huku kwetu Katesh hana, anatia huruma na familia yake imesambaratika.

Waweza ongezea utapeli mwingine unaowakumba wastaafu, ili tujiepuke nao.

Wasalaam....
 
Kuna vitu ambavyo mtu anapaswa kupitia wakati anaingia kwenye maisha, sio wakati amechoka tayari na wakati wa kutundika daluga umewadia, nampa pole sana, hao hawez waona kwa namna yeyote ile
 
Habari,
Kuna Bwana mmoja anaitwa Sauli, ni mtu wangu wa karibu. Tumeshughurikia pensheni yake as kastaafu shirika la Posta na kalipwa Milioni 70. Sasa game iko hivi, kuna tapeli mmoja dreva (inasemekana kashamliza mfanya biashara mmoja Tsh 80M na mwingine takribani 50M), kashamuweka king huyu mzee wetu. Huyu dreva anachofanya anasema anawatafutia watu fursa za biashara na anawaunganisha na shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNDP kwa kutafuta watu wenye mitaji watakaofanya biashara za misitu. Huyu dreva anakupa mipango kabambe na anakuunganisha na mapadre, maaskofu, mashehe au wachungaji (hawa huwa ni fake) ambao husema nao wanafanya biashara hizi. Sasa siku ya siku utashangaa hao wachungaji fake wanakuja kwako au mnakutana hotelini huku wamevaa mavazi ya kichungaji mainly Roman Color shirts au nguo za kiustaadhi na wanakupa mipango mizuri ya biashara. Wanahakikisha unakuwa interested na watakuomba uchangie mf gharama ya wao kukaa hoteli, mafuta ya gari n.k (kumbe ndo watapeliwa hivyo).

Sasa mtaendelea kuwa na mawasilino huku wakitumia vifungu vya Biblia/Kurani uwachangie karibu kila huduma. Siku nyingine huchagua msitu wa mbali na kwako na kumuagiza huyo dreva muende ukauone then ushughurikie leseni ya umiliki. Sasa hapo penye leseni utaandaliwa watu wa ardhi/misitu fake na utalipia leseni fake let say ya 25M, utalipia usafiri, gharama za upimaji n.k kumbe msitu wenyewe hauuzwi ni mali ya serikari.

Siku nyingine itapangwa trip ya kupeleka hivyo viambatanisho vya Misitu unayomiliki huko Dar, Arusha, Mwanza, Kampala, Nairobi etc kwenye ofisi ya wawakilishi wa UNDP. Kumbuka kila gharama unalipia wewe, huko sasa ndo unaenda kutapeliwa mpaka ndala, unakuja kustuka pensheni yooote uliyoisotea kwa miaka dahari inaliwa na wasio na uchungu nayo.........

Ndugu yangu,
Utapeli ni taaluma, wizi ni ubunifu makini na hawa watu ni wajanja na hubuni mbinu nyingi sana kuibia watu. Wanaofanya haya wakati mwingine ni watu tunaowafahamu, kwa kujua ama kutojua. Wastaafu wengi wamelizwa kwa njia hizi au nyingine. Muonye ndugu yako, muelekeze ajikite ktk biashara halali, asitafute pesa za haraka haraka. Pesa hutafutwa kwa jasho na si kwa njia za mkato. Pensheni imefarakanisha wastaafu wengi na familia zao kwa kuingia ktk biashara za magumashi zisizo na faida na zilizojaa utapeli. Pole kwa waliolizwa. Mzee huyu tunatafuta namna ya kumuokoa ila ndo hivyo keshalizwa, hivi sasa hata pesa za kununulia wanzuki au mbege huku kwetu Katesh hana, anatia huruma na familia yake imesambaratika.

Waweza ongezea utapeli mwingine unaowakumba wastaafu, ili tujiepuke nao.

Wasalaam....


Napata shida sana kutaka kumhurumia huyo mzee lakini nashindwa...mimi binafsi nina huruma sana lakini kuna watu wana tamaa hulaghaiwa kwa haraka mno na huwa hawataki ushauri... Tatizo mojawapo ni taasisi chache mno nchini mwetu hutoa ushauri kwa watu wanaokaribia kustaafu...ndio maana mtu akistaafu utaona anannunua daladala tano, kuweka duka, au grocery ya vinywaji na kadhalika na baada ya miaka miwili vyote vinatoweka...
 
Asante mkuu kwa taarifa
Ila utapeli huu na waaina hiyo,mara nyingi huwakumba wale Wastaafu ambao walichezea maisha wakati wa ujana wao.

Ila kama ni mstaafu ambae alikuwa ni mfanyabiashara au amewekeza kile kidogo alichokuwa kaipata na kuwa mfanyabiashara wa aina yoyote basi haingii kwenye mtego huu maanaa nakuwa tayuari na mipango ya kuboresha miradi yake au kuongeza miradi.

Hii hali inawakumba wale wastaafu ambao walicheza na maisha ya ujana,na kutegemea sana kiinua mgongo kije kimpe utajiri na kumtoa kimaisha ambapo wengi sana wanafeli na wengi hufa kwa maradhi.Ukitaka kujua hili we kaa na mstaafu ambae ana miradi halafu kaa na mstaafu ambae anategemea apate kiinua mgongo ndio aanzishe miradi na utaona utofauti.Wale waliobweteka wengi wanakuwa kama wamechanganyikiwa vile kabla ya kupata hiyo pesa.

Maana wanataka kuwekeza pesa kwa kutegemea mafanikio na faida kubwa kwa muda mfupi mno huku umri ukiwa umempita.
Ila hili ni somo kwa vijana wa sasa ambaeo ni wastaafu watarajiwa.
 
njia rahisi ya kuepuka utapeli ni kutotaka mafanikio kwa njia za mkato
 
Asante mkuu kwa taarifa
Ila utapeli huu na waaina hiyo,mara nyingi huwakumba wale Wastaafu ambao walichezea maisha wakati wa ujana wao.

Ila kama ni mstaafu ambae alikuwa ni mfanyabiashara au amewekeza kile kidogo alichokuwa kaipata na kuwa mfanyabiashara wa aina yoyote basi haingii kwenye mtego huu maanaa nakuwa tayuari na mipango ya kuboresha miradi yake au kuongeza miradi.

Hii hali inawakumba wale wastaafu ambao walicheza na maisha ya ujana,na kutegemea sana kiinua mgongo kije kimpe utajiri na kumtoa kimaisha ambapo wengi sana wanafeli na wengi hufa kwa maradhi.Ukitaka kujua hili we kaa na mstaafu ambae ana miradi halafu kaa na mstaafu ambae anategemea apate kiinua mgongo ndio aanzishe miradi na utaona utofauti.Wale waliobweteka wengi wanakuwa kama wamechanganyikiwa vile kabla ya kupata hiyo pesa.

Maana wanataka kuwekeza pesa kwa kutegemea mafanikio na faida kubwa kwa muda mfupi mno huku umri ukiwa umempita.
Ila hili ni somo kwa vijana wa sasa ambaeo ni wastaafu watarajiwa.

U naied it rafiki. Tujitahidi kuwashauri
 
Yaani wanahakikisha umebaki mweupeee, ndo wanakupotezea ufe na mastress yako
 
Kuna mstaafu mmoja alishutuka but walishapiga M 7. ... Wabaya sana wale.matukio ya namna hii watu wanatakiwa kupewa matangazo ya kuwaelimisha kupitia vyombo vya habari. Police na mifuko ya hifadhi ya jamii wanatakiwa kusaidia katika hili. Mafunzo ya kujiandaa na maisha baada ya utumishi yapewe kipaumbelw.
 
Kuna mstaafu mmoja alishutuka but walishapiga M 7. ... Wabaya sana wale.matukio ya namna hii watu wanatakiwa kupewa matangazo ya kuwaelimisha kupitia vyombo vya habari. Police na mifuko ya hifadhi ya jamii wanatakiwa kusaidia katika hili. Mafunzo ya kujiandaa na maisha baada ya utumishi yapewe kipaumbelw.
 
Mtu una interest na misitu alafu unaingizwa kingi hii ni tamaa tu.
 
Back
Top Bottom