Itakulipa ukiuza zile products zao. Kipengele kitakuja nani atanunua? Package unauziwa laki 5 madawa yenyewe + coffee zile ni ngumu kutuuzia watz sie.
Nahisi kutakuwa na hizo bonuse za ukimleta A nae akawaleta B na C wewe Z utapata kamisheni ya laki 3. Upuuzi mtupu tu
Si tulishawahi kualikwa kwenye semina yao pale mwenge. Tulipofika pale tukashangaa namna watu walivyokua wanafake maisha, kila mtu amevaa suti wengine na glass amchoni
Speech imeanza, tunategemea watu waanze kujadili namna global yao inavyofanya kazi wao wanajikita kuelezea magari na pesa wanazomiliki
Kuna kapambe kamoja walikapa u-mc sijui walikaahidi watakalipa shingapi maana kalikua kanawapaisha kinoma.
Jamaa akatuambia kua anamiaka 27 kaacha chuo kwa kazi hiyo now anamiliki utajiri wa milion 175 na ana gari ya kifahari ambayo inaogopwa na watu kwa ulaji wake wa mafuta
Akasema lengo la hii biashara ni kuwainua vijana wasiojiweza waweze nufaika
Akatupa mchanganuo wa upataji pesa nikaona haimake sense, mara sijui utoe laki 5 uwape wao watakupa package yenye dawa kisha watakufungulia account yenye kianzio cha 30,000 halafu sijui uanze kutengeneza pair kwa ku-invite wenzako. The more you invite tho more you earn
Nikawauliza mnauhakika hii ishu ina hela kama ambavyo nyinyi mnaipigia promo hapa? Wakasema ndiyo
Nikawauliza kwa msisitizo tena mlimaanisha mliposema lengo kuu la hii biahara ni kusapoti vijana? Wakasema ndiyo
Nikasema sawa, kutokana na wewe hapo mdau ulivyotuelezea kua umefanikiwa na una miliki utajiri mkubwa basi laki 5 kwako sio ishu hivyo tunatumaini wewe ndiye utakua nuru ya sisi kwa kuanza kutupa sapoti ya kutukopesha hiyo laki 5 ya kuanzia.
Jamaa alikua anatabasamu tabasamu na ucheshi wa hapa na pale lakini baada ya hilo swali nikaanza kuona mabadiliko taratibu huku jamaa akionekana kutofurahishwa na swali langu
Nikaendelea kukazia, nikamuambia kwenye hiyo laki tano utayotukopesha tutaanza kutengeneza pair ambayo iko chini ya management yako na account zetu zitakua chini yako ili pesa ikiingia tu utakua unaikata huko huko juu kulipa deni lako
Hamuwezi mkawa mnasema mnalengo la kuwasaidia vijana kwa kuwatoza 500,000 ya kujiendeleza wakati uhalisia mnaujua kwa mtaani mtu ambaye anaweza ku afford laki 5 huwezi kumuongelea kama ni mtu asiyejiweza wakati mtaani humo humo kuna watu wapo hawana hata senti
Nikaskia brother tunashukuru kwa swali lako ila swali lako utajibiwa privately baada ya kikao kuisha na aliye kualika