Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 13,181
- 20,471
CHADEMA yamteua Mwenda ubunge Kalenga
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemteua mwanasheria Sinkala Mwenda kugombea ubunge wa Kalenga baada ya kuwashinda wenzake 13.
Katika kinyanganyiro cha uteuzi huo kada aliyekimbia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kushindwa kura za maoni mwaka 2010, Zubery Mwachura, aliambulia kura sifuri.
Mwenda alitangazwa kuwa mshindi baada ya uchaguzi uliofanyika juzi kwa zaidi ya saa 10 mjini Iringa.
Uchaguzi huo ulisimamiwa na wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA taifa, Chiku Abwao na Benison Kigaila, ambapo kura 132 zilipitisha jina la mwanasheria huyo huku kura 122 zikimchagua Grace Tendega.
Katika uchaguzi huo, kada wa CHADEMA na muuza magazeti maarufu mjini Iringa, Aidan Pungili, aliambulia kura 2 wakati Daniel Luvanga akipata kura moja.
Wagombea wengine walioonyesha kufanya vema baada ya kujiunga na CHADEMA wakitokea CCM ni Dk. Evaristo Mtitu, aliyepata kura 32 na Ancent Sambala aliyepata kura 22.
Mgombea, Akbar Sanga, alipata kura 21; Rehema Makoga kura nne, Henry Kavina kura tisa, Mussa Mdede kura 48; Mchungaji Samweli Nyakunga kura mbili na Mwalimu Vitus Lawa akipata kura 14.
Kigaila aliwataka viongozi wa CHADEMA Jimbo la Kalenga kukijenga zaidi chama hicho na kwamba, baada ya kampeni kuanza Wana CHADEMA wilaya zote za Mkoa wa Iringa wataingia kazini katika jimbo hilo.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemteua mwanasheria Sinkala Mwenda kugombea ubunge wa Kalenga baada ya kuwashinda wenzake 13.
Katika kinyanganyiro cha uteuzi huo kada aliyekimbia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kushindwa kura za maoni mwaka 2010, Zubery Mwachura, aliambulia kura sifuri.
Mwenda alitangazwa kuwa mshindi baada ya uchaguzi uliofanyika juzi kwa zaidi ya saa 10 mjini Iringa.
Uchaguzi huo ulisimamiwa na wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA taifa, Chiku Abwao na Benison Kigaila, ambapo kura 132 zilipitisha jina la mwanasheria huyo huku kura 122 zikimchagua Grace Tendega.
Katika uchaguzi huo, kada wa CHADEMA na muuza magazeti maarufu mjini Iringa, Aidan Pungili, aliambulia kura 2 wakati Daniel Luvanga akipata kura moja.
Wagombea wengine walioonyesha kufanya vema baada ya kujiunga na CHADEMA wakitokea CCM ni Dk. Evaristo Mtitu, aliyepata kura 32 na Ancent Sambala aliyepata kura 22.
Mgombea, Akbar Sanga, alipata kura 21; Rehema Makoga kura nne, Henry Kavina kura tisa, Mussa Mdede kura 48; Mchungaji Samweli Nyakunga kura mbili na Mwalimu Vitus Lawa akipata kura 14.
Kigaila aliwataka viongozi wa CHADEMA Jimbo la Kalenga kukijenga zaidi chama hicho na kwamba, baada ya kampeni kuanza Wana CHADEMA wilaya zote za Mkoa wa Iringa wataingia kazini katika jimbo hilo.
- Source: Tanzania Daima