Mwelekeo wa elimu ya Tanzania

Kahise

JF-Expert Member
Jul 25, 2008
379
435
Wadau wa Elimu, kwanza naomba ku declare interest kuwa mimi nilisomea ualimu ngazi ya stashahada.

Wakati nasoma shuleni, hasa somo la Historia nilifundishwa na kuaminishwa kwamba elimu ya kikoloni ilikuwa mbaya. Kwamba wakoloni waliwasomesha watanzania wale ambao walitaka kuwatumia kuimarisha utawala wao, kwamba ilitolewa kwa ubaguzi, kwamba ilikuwa haina nia njema, n.k.

Leo nikitafakari elimu hiyo niliyoipata, nashindwa kuelewa kwanini nilifundishwa mambo yale.

Je, baada ya Tanzania kupata kujitawala elimu yetu yenyewe imekuwa na malengo madhubuti ya kuwakomboa Watanzania au mambo yameendelea kuwa HOVYO?

ANGALIA: Wakati wa elimu ya mkoloni, Kila aliyeingia shule alijua kusoma na kuandika.

Wakati huu, lengo la kujua kusoma na kuandika lipo, lakini wasiojua kusoma na kuandika wanaendelea kupanda madarasa.

Elimu ya mkoloni ilipangwa kwa malengo mahususi kwamba kila level inayofikiwa iwe imemwandaa mtoto kupata Ujuzi (skill) fulani. Hivyo, kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kulipangiwa miaka 4 tu, yaani Darasa la Kwanza mpaka la nne.

Baàda ya pale wanafunzi wanaenda Middle School kwa miaka minne tena ambapo walimaliza wakiwa na fani tofauti tofauti. Kijana aliyemaliza middle school wakati ule aliweza kuishi ndani ya jamii kwa kujiajiri. Kisha kijana aliweza kuendelea na masomo yake ya sekondari nayo ilikuwa na malengo mahususi kwa kila level.

Leo tijiangalie, kujua kusoma, kuandika na kuhesabu, kunachukua miaka 7 na wanaoweza kuujua ujuzi huo ni wachache kwa kuwa tunapata vijana wengi wanaomaliza shule bila kujua kusoma na kuandika.

Je, wadau ni kweli elimu yetu ina tija yoyote kwa watoto wetu?
 
Uhaba wa vifaa vya kufundishia,mrundikano wa watoto katika darasa moja,uhaba wa madarasa,viongozi kutokuwa na uchungu wa wananchi wao,rushwa,umimi na umaskini wa wazazi.

Wale waliobahatika kupeleka watoto wao private schools hizi changamoto haziwakabili sana
 
Ni Kwel Mkuu elimu yetu kuna Pahala tumeteleza ila si sahihi kusema wengi wanaomaliza darasa la Saba hawajui kusoma na kuandika WACHACHE ndio hawajui kusoma na kuandika.

Nasema Hivi sababu mtoto akifka darasa la nne anakuwa na mtihan YA kupandia darasa hvyo wale wasiojua kusoma na kuandika hudakwa hapo japo Wapo baadhi hubahatika kuendelea Kumbuka mtihanai wa darasa la nne ndio mtihan pekee wenye maswali mengi ya kujaza kuliko kuchagua Tofaut na darasa la Saba ambapo had hesabu hupewa maswali YA kuchagua

Jambo jingine n kuwa elimu ya mkoloni ilidahili wanafunzi wachache Sana kulingana na resources walizokuwa nazo Kama walimu vifaafunzo na darasa pia Tofaut na sasa idadi YA wadahiliwa n kubwa Sana kuliko hizo resources Njoo hapa CHARAMBE shule ya msingi iliyopo DSM watoto wanakaa chini had Leo madawati hayatoshi unategemea nn katika hilo mkuu hatuwezi fanikiwa kutoa wanafunzi bora

NINI SULUHI

Ni vema serikali ikaangalia uwiano wa wanafunzi na nyenzofunzo Kama madawati walimu na madarasa yaendane kwa uwiano sahihi

Pili maslahi ya walimu yaboreshwe ili kuwapa morali zaidi kiuhalisia Hali ya uchumi na pato lao havilingani

Tatu kuna haja ya kuangalia sera yetu ya elimu Kama inakidhi matakwa ya wakati tuliopo hasa suala la mitaala wengi wanalilalamikia hili tunajua kibadili mtaala n gharama kuwa lakn hatuna budi kulishughulikia Kwan kuchelewa kwetu ndio tunatengeneza bomu la Baadae
 
Ni Kwel Mkuu elimu yetu kuna Pahala tumeteleza ila si sahihi kusema wengi wanaomaliza darasa la Saba hawajui kusoma na kuandika WACHACHE ndio hawajui kusoma na kuandika.

Nasema Hivi sababu mtoto akifka darasa la nne anakuwa na mtihan YA kupandia darasa hvyo wale wasiojua kusoma na kuandika hudakwa hapo japo Wapo baadhi hubahatika kuendelea Kumbuka mtihanai wa darasa la nne ndio mtihan pekee wenye maswali mengi ya kujaza kuliko kuchagua Tofaut na darasa la Saba ambapo had hesabu hupewa maswali YA kuchagua

Jambo jingine n kuwa elimu ya mkoloni ilidahili wanafunzi wachache Sana kulingana na resources walizokuwa nazo Kama walimu vifaafunzo na darasa pia Tofaut na sasa idadi YA wadahiliwa n kubwa Sana kuliko hizo resources Njoo hapa CHARAMBE shule ya msingi iliyopo DSM watoto wanakaa chini had Leo madawati hayatoshi unategemea nn katika hilo mkuu hatuwezi fanikiwa kutoa wanafunzi bora

NINI SULUHI

Ni vema serikali ikaangalia uwiano wa wanafunzi na nyenzofunzo Kama madawati walimu na madarasa yaendane kwa uwiano sahihi

Pili maslahi ya walimu yaboreshwe ili kuwapa morali zaidi kiuhalisia Hali ya uchumi na pato lao havilingani

Tatu kuna haja ya kuangalia sera yetu ya elimu Kama inakidhi matakwa ya wakati tuliopo hasa suala la mitaala wengi wanalilalamikia hili tunajua kibadili mtaala n gharama kuwa lakn hatuna budi kulishughulikia Kwan kuchelewa kwetu ndio tunatengeneza bomu la Baadae
Nashukuru kwa kuwa wachache mnayaona ninayoona. Mimi Sasa nadhani sisi wadau tuendelee kutoa mawazo ili elimu inayotolewa Tanzania ibadilishwe kulingana na wakati.

Mwanzoni mwa thread hii nililinganisha elimu ya mkoloni na hapa tulipo. No kweli shule zilikuwa chache n.k., hoja yanhu ilikuwa ni mfumo: kwa nini tulitoka kwenye miaka Minne, ambayo kimsingi mtoto anajifunza KKK, na tukaenda kwenye miaka 7 ambayo kimsingi mtoto anatoka na ujuzi wa miaka ile ile minne? Hata ukuangalia miaka minne mtoto anapokuwa sekondari, anapata ujuzi gani ambao utamfanya aweze kujitegemea ndani ya jamii?

Kwa nini hatujali na kuendelea kuwapatia watoto wetu elimu isiyokuwa na tija Katina maisha?

Kwa mfano, leo kijana akimaliza Kidato Cha Sita, mwache mtaani, asiendelee na elimu ya chuo kikuu, atafanya nini ili kukidhi mahitaji yake?

MUHIMU SANA

Ni muda muafaka tuanze kufikiria kufundisha practical education kuliko theoritaical one. Naona nachanganyikiwa kila ninapofikiri kama waheshimiwa wenzetu hawayaoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom