Tunayo tayari kimsingi changamoto ya mtaji wa kutosha ipo na taasisi za fedha zinakwepa sana kusupport mambo ya tenda na tayari tulitegemea Mkopo unachelewa
Kwa kukusaidi,Nenda BOT au Banki kuu,kuna kitengo maalum,amacho ukipata Tender na wao kuidhibitisha basi unapewa pesa chap chap.
Kwa kumbukumbu zangu hata TWB Bank na wao wanamfumo huo,wiki haifiki unakula pesa.Ila iwe Tender na sio ujanja ujanja.Wanakupa mkwanja wa Kutosha wa maana.
Suala la kusema kwamba ulitegemea mkopo unaona unachelewa,hili ndio linatia shaka,sijui kwanini watu huwa hamuwi wakweli? Ukienda na Blaa Blaa za ujanja ujanja hakuna Bank itakupa Mkopo,na hapo issue sio kuchelewa issue ni kwamba vigezo hakuna.
Mfumo wa Tender na kwa umuhim wake ndio maana Banks hasa BOT wameweka Kitengo maalum kwa ajili ya watu wa Tenders tuuu,ili mhudumiwe kwa wepesi.
Hata huyo mnaemuhitaji nae pia hawezi kutoa pesa kwa haraka namna hii,lazima na yeye pia ahakiki tender kama wanavyofanya Bank,na haiwezi kuwa ndani ya muda mfupi kama mnavyofikiria.
Hapo kuna suala la kusign mkataba na Mteja wenu na lazima mkataba uwe wenye kuonyesha viti vingii kwenye vitakavyohusika katika tender na mambo ya commitments.
Hao Suppliers wakubwa unaowaona wao rafiki yao ni Banks,Sasa hapa ndio navuta picha ya uzoefu wenu na Bank katika upande wa Tenders.
Sio kwamba nataka kuharibu dili,ila mie huwa sipendi ubabaishaji kwa vitu vilivyo wazi.
Narejea:-Hakuna taasisi yoyote inayokwepa kusupport mambo ya Tenders tena wengine wanawatafuta kabisaa watu wa Tenders,ila muhim sio ujanja ujanja,lazima wajiridhishwe kwenye Tenders wanazodhamini.
Haiwezekani BOT waweke kitengo maalum halafu eti wao wenyewe wawe wanakwepa,kama ni kukwepa basi jua wanakwepa wale wapiga dili kwa kivuli cha Tenders.
Halafu neno Tender endelevu we umeliona wapi kwa bidhaa kama hizi?
Angalau ingekuwa kusupply chakula,maji au usafiri,kidogo inakuja